Twaweza: 61% ya wananchi hawapati taarifa kuhusu masuala ya siasa nchini

Sauti za Wananchi

Senior Member
Sep 2, 2014
113
138
Ripoti ya Twaweza iliyozinduliwa leo tarehe 15.09.2016 inayotoa Tathmini na matarajio ya wananchi kwa serikali ya awamu ya Tano imekuja na matokeo kuwa 61% ya wananchi wanasema hawapati taarifa kuhusu masuala ya siasa nchini, huku idadi ndogo (4%) wakisema wanapata taarifa za kutosha. 35% wamesema wana taarifa kidogo kuhusu masuala hayo.

Screenshot from 2016-09-15 11:17:05.png



Miongoni mwa wale ambao wanasema wanapata taarifa za kutosha ama wana taarifa kwa kiasi fulani, 61% wanapata taarifa kuhusu masuala ya kisiasa kutoka kwenye radio, 15% wanapata taarifa kwa kusikia kwa watu na 14% kupitia kwenye luninga. 1% pekee wametaja mitandao ya kijamii.

Screenshot from 2016-09-15 16:59:42.png


Unadhani idadi hii ya wananchi wanafanya maamuzi sahihi iwapo hawapati taarifa za masuala ya kisiasa? Toa maoni yako.
 
Ilo ni tatizo kubwa sana by the way watajifunza tu siasa kama maisha yatawabana kama walivyokuwa wameacha kunywa chai Kwa sababu ya siasa
 
Na kuna watu wanaamini jamiiforums ndio Tanzania na wana mpaka rais wa mioyo yao humu .. Wanakesha humu kupotosha na kuchafua watu.. Hata ukuta ulikuwa maarufu sana mitandaoni.. Huko mtaani watu wapo bize kupiga kazi ili kwenda na kasi ya kipenzi chao Magufuli.
Ndio hivyo hawana habari na hata hiyo "hapa kazi tu",wapo wapo tu!
 
Kweli, watanzania wengi hawapo aware na mambo ya kisiasa, hata kuchagua wanachagua kwa kufuata mkumbo tu
Hapa lawama zote mimi nazielekeza kwa wanasiasa. Wao ndio wanajua kila kitu kuhusu taifa hili..lakini hawapo tayari hata siku moja kuweka mambo hadharani,wanatuhubiria ujinga tu sijui sisiyemu mbele kwa nyuma lakini ipo siku watu watasanuka tu.
 
Mimi sielewi kuhusu mambo ya utafiti lakini nafikiria Kwa akili zangu ambazo mambo haya sio mbobezi.

Kwamba magu anaungwa mkono zaidi kuliko marais 128 wa Africa. Nashangaa Ni matatizo yangu au Africa siku hizi imekuwa Na nchi nyingi kiasi hicho? Nazo pia zilishirikishwa katika utafiti huu?

Magu aliingia mwaka Jana Kwa kupata asilimia 58 ya Kura leo pamoja Na changoto zote utafiti waonyesha anaungwa mkono Na zaidi ya asilimia 95!

UtAfiti unaonyesha asilimia 61 hawapati taarifa lakini hao hao ndio wamefikisha 96 ya kuungua mkono serikali hii! Kwa lipi Na ili Hali hawapati taarifa?

Upande wa huduma. Najaribu kujiuliza walioshiriki wanaishi Tanzania hii? Hospitali hazina dawa Na vifaa tiba, maduka ya msd yaliyofunguliwa kwa mbwbwe hayana kitu. Shule nyingi hazina mwalimu wa kutosha huku nyingine kama mwambani mza, baadhi ya wanafunzi wameazimwa ili wasomee shule jirani ya ilemela Kwa ukosefu wa madarasa Na yaliyopo yanajaaa pomoni hata mwalimu hana sehemu ya kupita! Halafu unakuja Na matokeo haya! Huu utafiti huu.
 
Ripoti ya Twaweza iliyozinduliwa leo tarehe 15.09.2016 inayotoa Tathmini na matarajio ya wananchi kwa serikali ya awamu ya Tano imekuja na matokeo kuwa 61% ya wananchi wanasema hawapati taarifa kuhusu masuala ya siasa nchini, huku idadi ndogo (4%) wakisema wanapata taarifa za kutosha. 35% wamesema wana taarifa kidogo kuhusu masuala hayo.

View attachment 400809


Miongoni mwa wale ambao wanasema wanapata taarifa za kutosha ama wana taarifa kwa kiasi fulani, 61% wanapata taarifa kuhusu masuala ya kisiasa kutoka kwenye radio, 15% wanapata taarifa kwa kusikia kwa watu na 14% kupitia kwenye luninga. 1% pekee wametaja mitandao ya kijamii.

View attachment 400810

Unadhani idadi hii ya wananchi wanafanya maamuzi sahihi iwapo hawapati taarifa za masuala ya kisiasa? Toa maoni yako.
Hapa hakuna maamuzi sahihi..labda upotoshaji sahihi.
 
Mimi sielewi kuhusu mambo ya utafiti lakini nafikiria Kwa akili zangu ambazo mbo haya sio mbobezi.

Kwamba magu anaungwa mkono zaidi kuliko marais 128 wa Africa. Nashangaa Ni matatizo yangu au Africa siku hizi imekuwa Na nchi nyingi kiasi hicho? Nazo pia zilishirikishwa katika utafiti huu?

Magu aliingia mwaka Jana Kwa kupata asilimia 58 ya Kura leo pamoja Na changoto zote utafiti waonyesha anaungwa mkono Na zaidi ya asilimia 95!

UtAfiti unaonyesha asilimia 61 hawapati taarifa lakini hao hao ndio wamefikisha 96 ya kufungua mkono serikali hii! Kwa lipi Na ili Hali hawapati taarifa?

Upande wa huduma. Najaribu kujiuliza walioshiriki wanaishi Tanzania hii? Hospitali hazina dawa Na vifaa tiba, maduka ya mad yaliyofunguliwa kwa mbwbwe hayana kitu. Shule nyingi hazina lakini wa kutosha huku nyingine kama mwambani mza baadhi ya wanafunzi wameazimwa ili easier shule jirani ya ilemela Kwa ukosefu wa madarasa Na yaliyopo yanajaaa pomoni hata mwalimu hana sehemu ya kupata! Huu utafiti huu.
Mkuu maigizo hayo
 
Hapa lawama zote mimi nazielekeza kwa wanasiasa. Wao ndio wanajua kila kitu kuhusu taifa hili..lakini hawapo tayari hata siku moja kuweka mambo hadharani,wanatuhubiria ujinga tu sijui sisiyemu mbele kwa nyuma lakini ipo siku watu watasanuka tu.
Serikali inazuia bunge, imezuia mikutano ya siasa, imekataza siasa vyuoni kisha inafungia vyombo vinavyoihoji kwa madai ya kichochezi
 
Serikali inazuia bunge, imezuia mikutano ya siasa, imekataza siasa vyuoni kisha inafungia vyombo vinavyoihoji kwa madai ya kichochezi
But hata upinzani nao naona wanazingua. Hivi wakishindwa wao kupambana na serikali kwa hoja zao,wananchi tutawezaje? Wanayo kazi ya kuhakikisha mambo yanakwenda inavyotakiwa unless watuambie lao moja.
 
Ripoti ya Twaweza iliyozinduliwa leo tarehe 15.09.2016 inayotoa Tathmini na matarajio ya wananchi kwa serikali ya awamu ya Tano imekuja na matokeo kuwa 61% ya wananchi wanasema hawapati taarifa kuhusu masuala ya siasa nchini, huku idadi ndogo (4%) wakisema wanapata taarifa za kutosha. 35% wamesema wana taarifa kidogo kuhusu masuala hayo.

View attachment 400809


Miongoni mwa wale ambao wanasema wanapata taarifa za kutosha ama wana taarifa kwa kiasi fulani, 61% wanapata taarifa kuhusu masuala ya kisiasa kutoka kwenye radio, 15% wanapata taarifa kwa kusikia kwa watu na 14% kupitia kwenye luninga. 1% pekee wametaja mitandao ya kijamii.

View attachment 400810

Unadhani idadi hii ya wananchi wanafanya maamuzi sahihi iwapo hawapati taarifa za masuala ya kisiasa? Toa maoni yako.
Nani yupo tayar kufa njaa kisa habar za kisiasa? Mulo wa usiku nautafuta mchana, unategemea nini???? Nchi zetu bado sana
 
Mimi sielewi kuhusu mambo ya utafiti lakini nafikiria Kwa akili zangu ambazo mambo haya sio mbobezi.

Kwamba magu anaungwa mkono zaidi kuliko marais 128 wa Africa. Nashangaa Ni matatizo yangu au Africa siku hizi imekuwa Na nchi nyingi kiasi hicho? Nazo pia zilishirikishwa katika utafiti huu?

Magu aliingia mwaka Jana Kwa kupata asilimia 58 ya Kura leo pamoja Na changoto zote utafiti waonyesha anaungwa mkono Na zaidi ya asilimia 95!

UtAfiti unaonyesha asilimia 61 hawapati taarifa lakini hao hao ndio wamefikisha 96 ya kuungua mkono serikali hii! Kwa lipi Na ili Hali hawapati taarifa?

Upande wa huduma. Najaribu kujiuliza walioshiriki wanaishi Tanzania hii? Hospitali hazina dawa Na vifaa tiba, maduka ya msd yaliyofunguliwa kwa mbwbwe hayana kitu. Shule nyingi hazina mwalimu wa kutosha huku nyingine kama mwambani mza, baadhi ya wanafunzi wameazimwa ili wasomee shule jirani ya ilemela Kwa ukosefu wa madarasa Na yaliyopo yanajaaa pomoni hata mwalimu hana sehemu ya kupita! Halafu unakuja Na matokeo haya! Huu utafiti huu.

Marais 128 ni kutokana na tafiti zilizoanza mwaka 1999.

Mtu anaweza asipate taarifa ya mambo ya siasa lakini akapata taarifa za Utendaji wa Serikali.

Matokeo ya Utafiti yanaonesha majibu ya watu kuhusu huduma za Umma na si matokeo ya utafiti kuhusu hali ya huduma za Afya. Pia matokeo hayo hayaoneshi kuboreka huko kwa huduma za Umma ni kwa kiasi gani bali inaonesha kuboreka kwa ujumla.
 
Marais 128 ni kutokana na tafiti zilizoanza mwaka 1999.

Mtu anaweza asipate taarifa ya mambo ya siasa lakini akapata taarifa za Utendaji wa Serikali.

Matokeo ya Utafiti yanaonesha majibu ya watu kuhusu huduma za Umma na si matokeo ya utafiti kuhusu hali ya huduma za Afya. Pia matokeo hayo hayaoneshi kuboreka huko kwa huduma za Umma ni kwa kiasi gani bali inaonesha kuboreka kwa ujumla.
Ndugu siamini unachotaka Watanzania kutueleza kama kwamba tunaishi kisiwani kama mnavyotaka tuamini.

Tangu 1999 kama unavyodai bara hi ili limekuwa Na marais wengi wa kupigiwa mfano kuliiko mnavyotaka tuamini. Tuwataje kwa majina? Huyu wa sasa unayetaka tusadiki kuwa Ni Bora anaweza kupata tuzo ya Mo Ibrahim? Na hao wengine unaodai walipimwa kwa vigezo kama hivi? Na kupigiwa Kura Na nani? Nani aliendesha huo UtAfiti?

Pia sielewi unavyodai mtu hawezi kuwa Na taarifa za siasa lakini afahamu utendaji wa serikali. Hii serikali inapatikana vipi?

Hoja yako ya tatu inanitaka nitake wewe kutueleza zaidi. Hivi kwako wewe huduma za umma zina tafsiri gain?, Afya sio mojawapo?. Sielewi kwanini umechukua afya pekee wakati Mimi nilitaja pia Na elimu Na kutoa mfano!

Wakati mwingine Ni vizuri ukatangaza maslahi yako katika suala linalokuhusu vinginevyo haiingii akilini kuwajibia twaweza.

Halafu hujaeleza kilichompandisha hiyo kiwango hicho wakati mwaka mmoja uliopita ailiungwa mkono Na asilimia 58 ya wapiga Kura. Leo kimetokea nini? Itapendeza utupe japo mifano michache.
 
Kweli, watanzania wengi hawapo aware na mambo ya kisiasa, hata kuchagua wanachagua kwa kufuata mkumbo tu
Na jinsi bunge limefungwa na vyombo vya habari vinavyohoji serikali kufungiw nadhani serikali huwa inafurahi sana wananchi wasiwe politically active
Haswaa!

Huo ndio mpango mzima. Lakini wajue tu iko siku yenye jina na kila kitu hakitakuwa kama kilivyo sasa.
 
Back
Top Bottom