TAFAKURI CHOKONOZI: Baada ya Ugaidi nadhani CHADEMA tutasingiziwa kumiliki KIFARU cha kijeshi

Dec 11, 2010
3,321
6,328
Wakuu

Jana RPC wa Mbeya Bwana Ahmed Msangi ambaye pia kama mnamkumbuka alikuwa mtuhumiwa baada ya kutekwa na kuteswa ikiwa ni pamoja na kung'olewa kucha kwa koleo kwa Dr Stephen Ulimboka alitoa kituko cha mwaka ambacho wenye akili wanajua kuwa ni kuendeleza msaada wa kuisaidia ccm.

Nakumbuka hata tukio la kutekwa kwa Dr Ulimboka walitafuta exit na kujitahidi kuihusisha Chadema na tukio hilo ndipo mtego ukaanza kutegwa wa kumhusisha John Mnyika na madai kwamba ndio alitumiwa na Chadema kumshawishi Dr Ulimboka ili madaktari wagome kwa kuwa huduma ni mbovu na vifaa vya tiba vilikuwa haba.

Kituko cha jana cha RPC Msangi tunajua kuwa ni njia ya kuelekea tunako kujua kama ambavyo wamekuwa wanafanya hivyo siku zote. Walianza na ugaidi tukashinda kesi zote mbili, mahakama ikawaonya kuwa kutumia neno ugaidi litafukuza watalii wa nje maana hakuna hata shtaka lenye sura ya ugaidi. Jana RPC mzima anasema manati, visu na T shirt mpya ya chama ni zana za kivita!

Kwa akili ya RPC Msangi ni sawa na kutegemea siku moja kuona uwanja wa taifa manati, bendera na T shirt za Chama zikitumika kama zana za kivita! Kwa akili hiyo hiyo kina mama wenye visu majumbani nao wana zana za kivita za kuchinjia Nyanya na vitunguu, vijana wawinda ndege wenye manati au ukiwa na manati nyumbani ni sawa na kumiliki AK47 maana ni zana za kivita sawa na kumili KIFARU au bunduki.

Baada ya ugaidi kukwama, na hili la manati na kisu kukwama nadhani baadae tutasingiziwa kumiliki KIFARU au kombati tunazo vaa tutaambiwa ni mali ya jeshi na hivyo tuanze kuvaa mashati ya Bahama na suruali za mchelemchele.

Naweza tu kwa Sauti maana jamaa wanaposingizia zana za kivita wanasahau kuwa wauwaji wa ndugu zetu albino hawajakamatwa na waliomuua Mwangosi wako nje na Kamuhanda aliyekuwa RPC na kushuhudia mauwaji hayo kupandishwa cheo achilia mbali yule kada wa ccm aliye mchinja Msafiri Mbwambo kwa mashine ya kukatia mbao na baadae kutoroka akiwa mikononi mwa polisi mwenye silaha ya kivita naye yuko mtaaani ana dunda.
 
Ninategemea pia huyu jamaa kwa matatizo yake, kesho atasema ni marufuku Watanzania kufanya mazoezi ya viungo kwa kuwa ni kujifunza ujeshi.

Umesahau pia kamba za kuruka zinazouzwa madukani nazo ni zana za mafunzo ya kijeshi. Gym ambako kuna vifaa zaidi ya vyuma vya push-ups, zinatakiwa kufungwa kwa kuwa vinafundisha mazoezi ambayo ni mafunzo ya kijeshi.

Huyu jamaa ana matatizo ya akili.

Anapokataza watu kufundishwa ukakamavu na kwamba kazi ya ulinzi ni ya polisi tu, anasahau kwamba serikali imekuwa ikilia lia kila mara kwamba ulinzi ni jukumu la Watanzania wote.

Anasahau kwamba idadi ya polisi ni ndogo mno kuwa kila mahala Tanzania nzima.

Anasahau kwamba mara nyingine watu wanapohitaji ulinzi wa polisi wanalazimishwa kubadili ratiba zao kwamba polisi hawapo wakutosha.

Anasahau kwamba serikali imeanzisha mgambo kwa kuona polisi hawapo.

Anasahau namna serikali ilivyozindua mpango wa sungusungu ili kuimarisha ulinzi kwa kuwa polisi hawatoshi.

Anasahau kwamba kuna polisi jamii na polisi kata mara shirikishi ili tu kuimarisha ulinzi ambao polisi wameshindwa kutoa.

Kwa kweli kuwa na viongozi kama huyu jamaa ni janga kwa taifa!.
 
Mkuu,Msangi alivyoalivyo eti ndo RPC ..
Heshima ya cheo hicho kilichojengwa na akina WENCESLAUS MAGOHA,TIBAIGANA,KOMBE,ZELOTHE,CELINA KALUBA INAPOTEZWA MBAYA.
 
Kwa hili la jana limewaacha watu wengi midomo wazi!! jamani kama ni Siasa basi tuache wanasiasa wafanye kazi yao, na sisi tusio wanasiasa tutekeleze ya kwetu.

CCM wanahaha kwani mafunzo ya vijana wa CDM yamewachanganya mno kiasi sasa wanaomba msaada toka jeshi la Police kuyazuia.
 
Hazina tafauti na propaganda za Mahita kipindi kile na visu vya CUF.......cha kushangaza kuna watu wanaamini haya mambo......
 
ni vituko vitupuuuu RPC kuja na manati na visu mbele ya waandishi eti zana za kivita ....hivi watu wakamatwe momba ambako kuna mapolisi aje atangaze yeye ..ni vichekesho vitupu
 
Hawana dogo wale! Yaweza hata kuzushwa ile nyambizi ya kinyuklia iliyozama kule Arctic Circle ni ya Chadema ilikuwa inaenda kuifanyia ujasusi Marekani. Ukistaajabu ya Musa.
 
Mkuu Mohamedi Mtoi,mambo hayo si mageni katika siasa za Tanzania. Hukumbuki walichoaminishwa watanzania kuhusu CUF? Umeshasahau kuhusu chain ya tuhuma kwa CHADEMA yenu? Usitishike wala kuvunjika moyo. Yote yatapita lakini siasa za nchi hii zitasonga mbele
 
Last edited by a moderator:
image.jpg image.jpg

Magaidi wakiwa kwenye mazoezi ya kivita huko Bukoba chini ya kamanda Lwakatare
 
Hawana dogo wale! Yaweza hata kuzushwa ile nyambizi ya kinyuklia iliyozama kule Arctic Circle ni ya Chadema ilikuwa inaenda kuifanyia ujasusi Marekani. Ukistaajabu ya Musa.

hahaha......polisi wamechanganyikiwa ccm wamechanganyikiwa maana silaha pekee ya ccm ni kuwatumia polisi sasa polisi wenyewe wameshapotezwa wanatamani waiteke mahakama ili kesi wasikilize wao na waamue wao maana wanatumia fedha nyingi kutengeneza kesi halafu wanashindwa kama zile za ugaidi....chadema hawafai imewapoteza polisi na ccm ...yaani RPC mzima unakuja na manati na kisu mbele ya waandishi eti zana za kivita
 
Wakuu

Jana RPC wa Mbeya Bwana Ahmed Msangi ambaye pia kama mnamkumbuka alikuwa mtuhumiwa baada ya kutekwa na kuteswa ikiwa ni pamoja na kung'olewa kucha kwa koleo kwa Dr Stephen Ulimboka alitoa kituko cha mwaka ambacho wenye akili wanajua kuwa ni kuendeleza msaada wa kuisaidia ccm.

Nakumbuka hata tukio la kutekwa kwa Dr Ulimboka walitafuta exit na kujitahidi kuihusisha Chadema na tukio hilo ndipo mtego ukaanza kutegwa wa kumhusisha John Mnyika na madai kwamba ndio alitumiwa na Chadema kumshawishi Dr Ulimboka ili madaktari wagome kwa kuwa huduma ni mbovu na vifaa vya tiba vilikuwa haba.

Kituko cha jana cha RPC Msangi tunajua kuwa ni njia ya kuelekea tunako kujua kama ambavyo wamekuwa wanafanya hivyo siku zote. Walianza na ugaidi tukashinda kesi zote mbili, mahakama ikawaonya kuwa kutumia neno ugaidi litafukuza watalii wa nje maana hakuna hata shtaka lenye sura ya ugaidi. Jana RPC mzima anasema manati, visu na T shirt mpya ya chama ni zana za kivita!

Kwa akili ya RPC Msangi ni sawa na kutegemea siku moja kuona uwanja wa taifa manati, bendera na T shirt za Chama zikitumika kama zana za kivita! Kwa akili hiyo hiyo kina mama wenye visu majumbani nao wana zana za kivita za kuchinjia Nyanya na vitunguu, vijana wawinda ndege wenye manati au ukiwa na manati nyumbani ni sawa na kumiliki AK47 maana ni zana za kivita sawa na kumili KIFARU au bunduki.

Baada ya ugaidi kukwama, na hili la manati na kisu kukwama nadhani baadae tutasingiziwa kumiliki KIFARU au kombati tunazo vaa tutaambiwa ni mali ya jeshi na hivyo tuanze kuvaa mashati ya Bahama na suruali za mchelemchele.

Naweza tu kwa Sauti maana jamaa wanaposingizia zana za kivita wanasahau kuwa wauwaji wa ndugu zetu albino hawajakamatwa na waliomuua Mwangosi wako nje na Kamuhanda aliyekuwa RPC na kushuhudia mauwaji hayo kupandishwa cheo achilia mbali yule kada wa ccm aliye mchinja Msafiri Mbwambo kwa mashine ya kukatia mbao na baadae kutoroka akiwa mikononi mwa polisi mwenye silaha ya kivita naye yuko mtaaani ana dunda.

Lakini kibaya zaidi siku hizi wananchi wanajua kuchagua pumba na mchele mimi mwenye ile habari ukiichokonoa utajua tu kuna kamchezo kamechezwa maana sii wote waliopo c.d.m ni wema kuna wakina zito masalia.
 
Kwa sasa Ukawa Tunahitaji kura Milioni 14.5 tu kushinda Urais, kura yangu ni ya kwanza, Urais...Ukawa...Ubunge...Ukawa..na Diwani..Ukawa...we waache hao Polisi wahangaike na Mfa maji wao CCM, lakini hawataamini macho yao October...uzuri ni kwamba, Sisi wananchi wenye akili timamu tunajua na tunaelewa kuwa huu ni zaidi ya Upuuzi...
 
Back
Top Bottom