TUSHIRIKISHANE TABORA: Timu ya JamiiForums yapata ajali maeneo ya Mbaoni - Urambo

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,031
TAARIFA​

Tunasikitika kutangaza kutokea kwa ajali ya timu (2) ya wana Jamii Media, waliopo kwenye safari za mradi wa TUSHIRIKISHANE (JamiiForums yazindua rasmi mradi wa "Tushirikishane") iliyotokea hapo jana saa 5 asubuhi, maeneo ya Mbaoni - Urambo (Tabora). Timu hiyo ilikuwa na Meneja Uendeshaji na Mikakati wa Jamii Media, Bi Asha D. Abinallah na Mshauri wa Miradi Bw. Ericus Kimasha.

Timu hiyo ilikuwa ikielekea Kigoma mjini ili kukutana na wenzao ambako walikuwa na ratiba Warsha, kwa ajili ya kuendeleza shughuli za Mradi wa TUSHIRIKISHANE mara baada ya kumaliza shughuli zake hizo jimboni Nzega.

Kwa sasa hali zao si mbaya sana na wapo njiani kurudi Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.

JamiiForums tunatoa shukrani za dhati kwa wana Urambo kwa Ushirikiano, Matibabu, Ulinzi na Usalama uliyotolewa wakati na baada ya ajali hiyo.

tmp_22015-IMG-20160817-WA0024-2113068098.jpg


tmp_22015-IMG-20160817-WA0020-1711562377.jpg


tmp_22015-IMG-20160817-WA0007983277075.jpg

34bd39ab-0f07-4842-a54a-37ea9ceaf24f.jpg
Jamii Media inawashukuru Sana Bw. na Bi. Banyanga, wamiliki wa Magole Pre & Primary School kwa kuwasaidia wafanyakazi wetu waliopata ajali
82b69bf8-ce78-4faa-a8a7-ed6178700527.jpg

Jamii Media inawashukuru Afande Jonas na Afande Abdallah wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilayani Urambo kwa msaaada na huduma ya haraka kwa wafanyakazi wetu.

JamiiForums​
 
Back
Top Bottom