Siri ya maendeleo ya taifa masikini kuinuka

Maendeleo ya taifa yanategemea maemdeleo ya mtu mmoja mmoja.....na ifike hatua kila mtanzania ajue/apewe elimu ya pesa [uchumi] kulingana na uelewa wake yaani ile foundation...

Kila mwananchi awe na uweza wa kujua pato Lake,matumizi yake na faida yake...Mtu hajui hata kwa siku/wiki au mwezi anaingiza sh ngapi anatumia sh ngapi je, anaendesha maisha kihasara au kifaida...yupo tu kama mbuzi..!!

Embu fikira watu nane kati ya watu kumi...wanatumia zaid ya wanachotafuta[wanaishi kihasara],na watu wawili wana wanatafuta kingi zaidi ya wanachotumia[wanaishi kifaida]...afu wote wapo kwwnye nyumba moja,nini kitatokea apo..??
 
Kuna vitu vyengine vipo ndani ya uwezo wetu wala sio kwa sababu hatuna akili kama hao wenzetu, ni watu ambao hatuna utashi na hatupo serious tu kwenye suala la maendeleo. Kuna watu wengi waliyokuwa na elimu na wapo vizuri kichwani ila kuingia serikalini tu wanabadilika inakuwa kama wameingia ulimwengu mwengine ambao hauhitaji hizo akili zake.
Mkuu vitu gani tumeweza fanikiwa vya kujivunia kama taifa toka uhuru ?

Mtu asiye na utashi ni ishara ya kukosa akili ndio maana hana huo utashi kama sipo Sawa katika hili naomba usahihi wake maana nipo kujifunza pia

Siku zote wenye akili huwa hawana muda na mambo ya kijinga ili nao wasionekane ni wajinga na madhara yake ndo haya "wajinga kuwa viongozi na kosa kubwa la mjinga ni kujiona mwenye akili kumbe ni mjinga tu"

Ndio maana Mwanafalsafa Plato alipendekeza nadharia ya "mfalme Mwanafalsafa (philosopher king)"; kwa maana kwamba Kiongozi lazima awe mtu mwenye akili nyingi sana.
 
Siri muhimu kwa taifa masikini kuinuka kutoka katika dimbwi la umasikini.

Hii siri ambayo viongozi na wananchi wengi wa mataifa masikini hatupo tayari kuipokea na kuikubali.

Kama taifa tunataka tutoke haraka hapa tulipo kuna siri moja ya muhimu sana ambayo tunapaswa kuifahamu na kuikubali hata kama itapingana na mawazo na fikra zetu kwa kiasi kikubwa.

Maendeleo ya taifa ya haraka ni safari ya maumivu na machungu mengi sana ni safari iliyo jawa na mimba mingi sana.

Hakuna maendeleo ya taifa yayoletwa kwa sisi kupiga domo tu bila kusacrifice miili yetu na roho zetu kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.

Tunahitaji kufanya kazi kwa bidii na kwa dhati kwa mapenzi ya taifa letu liwe strong kuliko lolote ili tusirudi utumwani tena.

Mapambano haya sio kwamba yana hitaji mioyo ya dhati ya viongozi pekee la hasha hata wananchi wote kwa pamoja wakubwa kwa wadogo lazima tupambane bila kukata tamaa.

Tufanye kazi kwa bidii kwa maendeleo ya taifa kama vile kesho haipo.

Napenda kuwapa mifano ya hii jamii ya wakorea, wajapan, wachina hawa watu wanafanya kazi kuliko kawaida kama umewahi kufanya kazi na hii jamii utaelewa nini maana ya kufanya kazi kama vile kesho haipo ikiwezekana mtafute moja wapo kati ya mkorea, mjapan, mchina na uchunguze spirit yake ya kazi.

Hawa watu wanajenga nchi zao kwa dhati ya mioyo yao bila mashinikizo ya viongozi wakipanga wapambane wafanye hili au wawe pale watapambana kwa jasho na damu mpaka taifa linafanikiwa.

Kwa msaada wa kihistoria juu ya hawa watu miaka walio sacrifice maisha yao kwa maendeleo ya taifa lao umetawaliwa na maumivu na machungu mengi sana mfano:-

i. Taiwan (miaka ya 1960- 1990 )
ii. Japan (miaka ya 1860- 1990 )
iii. China (miaka ya 1950- 2000)
iv. Korea (miaka ya 1970-1990/2000)
V. Singapore (miaka ya 1960- 1990 )

Hio ni michache tu ya kugusia kwa atakae taka kujifunza.

Mazee hawa watu wanafanya kazi na wana spirit kutaka kuona nchi zao zinafika juu sio viongozi sio wananchi.

Hii jamii inatoa funzo kubwa sana kwetu kama tukiamua kuwa serious na kujifunza spirit yao lakini lazima tuhakikishe kweli tunaipenda nchi yetu na tunataka nchi yetu iwe giant of Africa na dunia.

Jambo la kufurahisha zaidi hawa watu hufikia mpaka hatua ya kulia kwa machozi mengi kwa uchungu juu ya nchi especially hao wachina ni mara nyingi sana nimeshuhudia hili mapenzi yalipo pitiliza kwa nchi hawa ndio wanayo.

Bila kukubali maumivu ya ujenzi ya nchi yatupitie hakika hatuwezi kufanikiwa kamwe maendeleo ya haraka hayaletwi kwa kupiga sogo na kelele za majukwaani.

"Siku zote nchi inapo piga hatua kubwa kimaendeleo wananchi wenye true spirit ulia kwa uchungu pale wimbo wa taifa unapo pigwa ukiwakilisha machungu yao katika ujenzi wa nchi".

R.I.P mashujaa (mabibi na mababu) wote mliopinga utumwa na ukoloni mpaka teno la damu la mwisho🕊️.
Ni sahihi kuwa, siri ya mafanikio kwa nchi, taasisi, kampuni, familia na hata mtu binafsi mmoja moja, kiukweli ni moja tu; yaani kufanya kazi kwa bidii tu..

Hii kanuni iliwekwa na Mungu muumba mwenyewe alipomwambia Adam Babu yetu wote mara baada ya anguko la dhambi pale bustanini Edeni, kuwa KWA JACHO LAKO UTAKULA (tafsiri yake ni utafanikiwa, utaendelea kiuchumi, utajenga nyumba nzuri, utanunua gari au magari, utamiliki mali, nk nk)...

Na Kwa kutuhakikishia kuwa kanuni yake hii (Mungu) aliyoiweka si ya adhabu wala ya kuwafanya watu wake wajute, aliongeza kusema, "..nitabariki kazi yoyote (halali) ambayo kila mtu ataamua kuifanya kwa mikono yake..."


Kama huo ndio ukweli, ni kitu gani kinatukwamisha sisi Tanganyika kama taifa tusipige hatua za haraka za maendeleo ya kiuchumi na kijamii? Je, hatufanyi kazi kwa bidii? Mifumo ya nchi yetu kutengeneza mazingira ya watu kufanya kazi zao ni mibovu? Mfano Kuna maeneo Kwa siku mbili sasa hayana umeme!!

Shida iko wapi??
 
Watu wanafanya kazi matokeo yake watawala mali za umma wanazitumia kwa anasa, bora tukose wote, unakuta DC/DED/DAS wanaenda safari moja kila mtu na V8 lake mafuta, posho yake na dereva, kwanini wasitumie gari moja na wote ni watumishi wa umma na wanaenda sehemu moja? Tanzania haina shida ya pesa ina shida ya matumizi mabaya na ufisadi, hakuna haja ya kufanya kazi
Mambo kama haya yanakatisha tamaa sana.

Nchi ambayo inaamua kuendelea ni ile ambayo viongozi na wananchi wanakuwa na mtazamo mmoja kwamba tunafanya kazi kwa bidii na tunanufaika wote.

Juzi kati katika mkutano wa raisi na bodi za mashirikka, akasema kuna wakurugenzi wa bodi wamepanda ndege kutoka Dar kwenda Arusha na wakati huo huo V8 VX yamewafuata Arusha kupitia barabara.

Hii nchi na zingine za Kiafrika ni ngumu kuendelea kwa sababu viongozi hawataki kuwa role models.

Viongozi wa umma hawawezi kueleweka kwa wananchi wenye akili timamu wanapowasisitiza wafanye kazi kwa bidii wakati wao wanaiba mali za wananchi.

Ninaamini asilimia 99% ya viongozi wa Tanzania wanawaza kujitajirisha wao na familia zao na kujenga mizizi ambapo familia na koo zao zitakuwa na uchumo imara miaka na miaka.

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Ukweli ni kwamba rasilimali watu wenye akili ndio Siri kubwa ya mataifa ya Ulaya,America na Asia kupiga hatua kubwa ya maendeleo.

Taifa la watu wajinga huzalisha viongozi wajinga maana kharamu haiwezi kuwa hali, ndivyo hivyo halali haiwezi kuwa kharamu,na waafrika tuna sifa ya ujinga ndio maana kila kitu ni hovyo ukitaka kuthibitisha hili angalia Tanganyika ya mkoloni na Tanganyika ya kina Nyerere,Mwinyi,Mkapa,Kikwete,John na sasa Samia,angalia South Africa ya Makaburu na, sasa ya waafrika,angalia Zimbabwe ya mkoloni naya sasa waafrika ni mbingu ma ardhi katika nyanja zote.

Tungepata viongozi kama Emperor Meiji wa Japan au Deng wa China tungekuwa mbali sana katika bara hili.
Nilipata kutoka kwenye media kwamba, enzi za ukoloni, jiji la Harare lilikuwa limepangika mpaka kuzidi baadhi ya majiji huko Ulaya, lakini leo hii Harare baada ya uhuru imechafuka kwa ujenzi holela na mabanda.

Vivyo hivyo angalia kotazi za railway zilizojengwa na mwingereza, mitaa inaeleweka, huduma za soko, shule, viwanja vya michezo nk. Leo hii kuna makazi holela nyumba nzuri lakini hakuna huduma za msingi bali zipo mbali sana.

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Siri muhimu kwa taifa masikini kuinuka kutoka katika dimbwi la umasikini.

Hii siri ambayo viongozi na wananchi wengi wa mataifa masikini hatupo tayari kuipokea na kuikubali.

Kama taifa tunataka tutoke haraka hapa tulipo kuna siri moja ya muhimu sana ambayo tunapaswa kuifahamu na kuikubali hata kama itapingana na mawazo na fikra zetu kwa kiasi kikubwa.

Maendeleo ya taifa ya haraka ni safari ya maumivu na machungu mengi sana ni safari iliyo jawa na miba mingi sana.

Hakuna maendeleo ya taifa yayoletwa kwa sisi kupiga domo tu bila kusacrifice miili yetu na roho zetu kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.

Tunahitaji kufanya kazi kwa bidii na kwa dhati kwa mapenzi ya taifa letu liwe strong kuliko lolote ili tusirudi utumwani tena.

Mapambano haya sio kwamba yana hitaji mioyo ya dhati ya viongozi pekee la hasha hata wananchi wote kwa pamoja wakubwa kwa wadogo lazima tupambane bila kukata tamaa.

Tufanye kazi kwa bidii kwa maendeleo ya taifa kama vile kesho haipo.

Napenda kuwapa mifano ya hii jamii ya wakorea, wajapan, wachina hawa watu wanafanya kazi kuliko kawaida kama umewahi kufanya kazi na hii jamii utaelewa nini maana ya kufanya kazi kama vile kesho haipo ikiwezekana mtafute moja wapo kati ya mkorea, mjapan, mchina na uchunguze spirit yake ya kazi.

Hawa watu wanajenga nchi zao kwa dhati ya mioyo yao bila mashinikizo ya viongozi wakipanga wapambane wafanye hili au wawe pale watapambana kwa jasho na damu mpaka taifa linafanikiwa.

Kwa msaada wa kihistoria juu ya hawa watu miaka walio sacrifice maisha yao kwa maendeleo ya taifa lao umetawaliwa na maumivu na machungu mengi sana mfano:-

i. Taiwan (miaka ya 1960- 1990 )
ii. Japan (miaka ya 1860- 1990 )
iii. China (miaka ya 1950- 2000)
iv. Korea (miaka ya 1970-1990/2000)
V. Singapore (miaka ya 1960- 1990 )

Hio ni michache tu ya kugusia kwa atakae taka kujifunza.

Mazee hawa watu wanafanya kazi na wana spirit kutaka kuona nchi zao zinafika juu sio viongozi sio wananchi.

Hii jamii inatoa funzo kubwa sana kwetu kama tukiamua kuwa serious na kujifunza spirit yao lakini lazima tuhakikishe kweli tunaipenda nchi yetu na tunataka nchi yetu iwe giant of Africa na dunia.

Jambo la kufurahisha zaidi hawa watu hufikia mpaka hatua ya kulia kwa machozi mengi kwa uchungu juu ya nchi especially hao wachina ni mara nyingi sana nimeshuhudia hili mapenzi yalipo pitiliza kwa nchi hawa ndio wanayo.

Bila kukubali maumivu ya ujenzi ya nchi yatupitie hakika hatuwezi kufanikiwa kamwe maendeleo ya haraka hayaletwi kwa kupiga sogo na kelele za majukwaani.

"Siku zote nchi inapo piga hatua kubwa kimaendeleo wananchi wenye true spirit ulia kwa uchungu pale wimbo wa taifa unapo pigwa ukiwakilisha machungu yao katika ujenzi wa nchi".

R.I.P mashujaa (mabibi na mababu) wote mliopinga utumwa na ukoloni mpaka teno la damu la mwisho🕊️.
Muhimu ni matumizi ya sayansi na teknolojia. Uwe na wazalishaji wengi kuliko walaji.
Nchi masikini hutumia watu wao waliosoma kudhibiti/kuzuia uzalishaji mali badala ya kuzalisha directly.
Punguza kazi za walaji, ongeza kazi za uzalishaji mali, hakuna zaidi ya hapo.
 
Ukweli ni kwamba rasilimali watu wenye akili ndio Siri kubwa ya mataifa ya Ulaya,America na Asia kupiga hatua kubwa ya maendeleo.

Taifa la watu wajinga huzalisha viongozi wajinga maana kharamu haiwezi kuwa hali, ndivyo hivyo halali haiwezi kuwa kharamu,na waafrika tuna sifa ya ujinga ndio maana kila kitu ni hovyo ukitaka kuthibitisha hili angalia Tanganyika ya mkoloni na Tanganyika ya kina Nyerere,Mwinyi,Mkapa,Kikwete,John na sasa Samia,angalia South Africa ya Makaburu na, sasa ya waafrika,angalia Zimbabwe ya mkoloni naya sasa waafrika ni mbingu ma ardhi katika nyanja zote.

Tungepata viongozi kama Emperor Meiji wa Japan au Deng wa China tungekuwa mbali sana katika bara hili.
Ni kweli kabisa kwamba viongozi hutokana na jamii.
Wajinga hutoa viongozi wajinga.
Hivyo kimsingi tunahitaji watu au wananchi wenye akili nzuri ambao watasabisha viongozi wawe wenye akili nzuri kwa kutokubaliana na wajinga au wapuuzi.
 
Mambo kama haya yanakatisha tamaa sana.

Nchi ambayo inaamua kuendelea ni ile ambayo viongozi na wananchi wanakuwa na mtazamo mmoja kwamba tunafanya kazi kwa bidii na tunanufaika wote.

Juzi kati katika mkutano wa raisi na bodi za mashirikka, akasema kuna wakurugenzi wa bodi wamepanda ndege kutoka Dar kwenda Arusha na wakati huo huo V8 VX yamewafuata Arusha kupitia barabara.

Hii nchi na zingine za Kiafrika ni ngumu kuendelea kwa sababu viongozi hawataki kuwa role models.

Viongozi wa umma hawawezi kueleweka kwa wananchi wenye akili timamu wanapowasisitiza wafanye kazi kwa bidii wakati wao wanaiba mali za wananchi.

Ninaamini asilimia 99% ya viongozi wa Tanzania wanawaza kujitajirisha wao na familia zao na kujenga mizizi ambapo familia na koo zao zitakuwa na uchumo imara miaka na miaka.

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Hatuna viongozi tuna majangili tupu
 
Ni kweli kabisa kwamba viongozi hutokana na jamii.
Wajinga hutoa viongozi wajinga.
Hivyo kimsingi tunahitaji watu au wananchi wenye akili nzuri ambao watasabisha viongozi wawe wenye akili nzuri kwa kutokubaliana na wajinga au wapuuzi.
Aibu kubwa sn
 
Tanzania hata tuchukuliwe tupelekwe huko Japan tutakula vya huko vitaisha tutabaki makapuku tena,tumezoea anasa na starehe za kuzidi uwezo kutoboa ni ngumu
Sure hata tupelekwe Marekani, kwa aina ya viongozi hawa wa hovyo tutavimaliza mapema sn hata mwaka 1 hautaisha
 
Watu wanafanya kazi matokeo yake watawala mali za umma wanazitumia kwa anasa, bora tukose wote, unakuta DC/DED/DAS wanaenda safari moja kila mtu na V8 lake mafuta, posho yake na dereva, kwanini wasitumie gari moja na wote ni watumishi wa umma na wanaenda sehemu moja? Tanzania haina shida ya pesa ina shida ya matumizi mabaya na ufisadi, hakuna haja ya kufanya kazi
Umemaliza, tujikite katika matumizi sahihi ya fedha na rasilimali tulizonazo
 
Back
Top Bottom