Sababu ya watu kuogopa kutoa ushahidi kwenye baadhi ya matukio aliyo shuhudia live na wengine baadhi hukimbia kabisa

John_Anthony

Senior Member
Mar 27, 2024
190
314
Natumaini wote mko poa ndg wana JF,, lakini poleni sana kwale wote wenye changamoto yoyote ya kiafya au maisha kwa ujumla poleni sana Mungu awasaidie mkae sawa 🙏

Ndg zangu nimeamua kuandika uzi huu kutokana na mambo yanayo fanyika kwenye jamii zetu haya mambo yanaumiza sana😭 mitaani kumekuwa na vifo vingi sana vya watu baadhi vinaeleweka vizuri na wana jamii huku vingine vikiwa ni vya kuhisiwa tu kuwa huenda amefanywa hivi au

Lakini la kusikitisha zaidi kuna kuwa na watu wanao shuhudia kabisa mwanzo wa tukio mpaka mwisho lakini wanakausha kama vile hawajaona chochote ila mtu ndio tyr kafa hivo inabaki tu minong'ono ya chini chini wakifika polisi hao watu hujitenga kabisa tena wengine huondoka kabisa eneo la tukio,,, haya yote hutokea kwa sababu ya sheria na mifumo kwa askari walio wengi, shahidi akijitokeza kutoa ushahidi wake wana shughulika zaidi na huyo shahidi kuliko kushughulikia tukio zima yani yanageuka kuwa majuto kwa mtoa ushahidi hawafikirii kuwa huyo mtu ameguswa na matukio yanayo fanywa na baadhi ya watu wao hufikiria mtoa taarifa kuwa ana kiherehere kwahiyo wanakula sahani moja na shahidi tumeshuhudia watu wengi walio jaribu kusaidiana na askari kushughulikia waharifu lakini mwisho wa siku shahidi ndio anakuwa mwaharifu yaani,, yani askari badala ya kumpongeza mtoa ushahidi lakini wao wana mchallenge kupita kawaida hadi mwisho wa siku shahidi anashindwa anakuwa mtuhumiwa mwenyewe

Kwa kifupi hiyo ndio taswira tu ya mambo yanayo endelea kwenye jamii hadi kwenye suala la vifo kutoa ushahidi inakuwa ni kiherehere

Kuna siku moja nilipita barabara flani hivi nilikuta mtu amegongwa na gari gari lililo mgonga huyo bwana lilikuwa limepitiliza haraka kwahiyo halikueleweka kuwa ni gari gani japo kuna wengine walilitambua hilo gari lakini walikausha, huyo bwana alikuwa liye gongwa alikuwa amebaki pale barabarani hakuna mtu aliye msogelea wala kumgusa na vyombo vingine vya usafiri viliendelea kumkwepa akiwa pale pale,, mimi nilivoona watu wanashangaa tu hawataki kuenda kumsaidia nilijaribu kuwa hamasisha "jamani tuendeni tumsaidie mwenzetu..." watu walisema wanaogopa wakimgusa yule bwana eti wataacha alama za vidole itaonekana wao ndio wameua 😭😭 kwahiyo tuliendelea kumshangaa pale huku wengine wakihangaika kuwaita polisi mwisho mimi uvumilivu ulinishinda niliamua kuenda hivo hivo bahati nzuri kuna jamaa mwingine alikuwa ameguswa na hilo tukio yeye alikuwa ana bajaji kwahiyo tulimbeba yule hadi hospitalini alikuwa bado hajapoteza maisha ila alikuwa amepoteza fahamu,, lakini kitu kingine cha ajabu tulivo mfikisha hospitalini tulijielezea na kueleza hali ilivo kuwa madaktari wakasema huu msalaba tunaubeba sisi tulio mpeleka pale kwa kuna gharama tulitakiwa tulipe kwa sababu haikujulikana kama ana bima au la! hivo sisi tulitakiwa kuullipia gharama zinazo husika kwenye ufunguaji wa faili bahati mbaya sana hiyo siku mimi na mwenzangu hatukuwa na hela za kutosha kulipia pale kwahiyo mgonjwa aliwekwa kando kwa muda 🥲 tukisubiri ndg zake waje na hii kesi siku sikia lolote mpaka sasa wala haikusemwa popote wala hakuna askari yeyote akijihusisha na hili tukio

Hii ndio hali halisi zinazo endelea kwenye jamii, watu wanaogopa kushiriki kwenye kutoa ushahidi hatakama mtu amepatika amekatwa katwa mapanga ikionekana tu uwezekano wa kupona huyo mtu ni mdogo watu wanakula kona,,

Mimi nimeandika tu huu uzi wala sifahamu kama unaweza kubadilisha chochote 🥲 lakini huku kwenye jamii zetu kumejaa maovu sana kama kuna mtu upo kwenye cheo fulani huko serikalini au upo kwenye harakati hizo nawaombeni mlitazame hili pia 😐 raia wanateseka sana watu wanapoteza ndugu zao bila sababu zozote za msingi HII AMANI INAYOSEMEKANA KUWA NCHI INA AMANI TUNATAMANI IWE NI AMANI YA KWELI KWA RAIA WOTE

Asanteni sana kwa kuvumilia kusoma huu uzi 🙏🙏 naamini nimeeleweka maana yangu ni ipi
 
Moja kati ya uzi bora kwa mwezi huu. Umeandika ukweli kabisa ndugu. Police ni maigizo sana, kiasi kwamba raia wanashindwa kuwapa ushirikiano kwenye mambo mengi tu. Na hili jambo ni la muda mrefu sana, sijui hata viongozi wao huwa wanalichukuliaje aisee. Inawezekana kuna uchawi huko Police kiasi kwamba ukiingia basi na akili zako zinakuwa tope kabisa maana hawabadiliki.
 
Moja kati ya uzi bora kwa mwezi huu. Umeandika ukweli kabisa ndugu. Police ni maigizo sana, kiasi kwamba raia wanashindwa kuwapa ushirikiano kwenye mambo mengi tu. Na hili jambo ni la muda mrefu sana, sijui hata viongozi wao huwa wanalichukuliaje aisee. Inawezekana kuna uchawi huko Police kiasi kwamba ukiingia basi na akili zako zinakuwa tope kabisa maana hawabadiliki.

Hii hali inasumbua sana wanyonge yani ukiwa choka mbaya afu unataka utoe ushahidi basi wewe ndio unageuka kuwa mwaharifu hii inatesa sana
 
Hii hali ni mbaya sana. Juzi uswahili kwetu huku tulisikia makelele ya watoto "Baba ana mchinja Mama" muda wa jioni tu kama saa kumi na moja kasoro.Watoto wamepiga kelele wee hadi wanaita majina ya jirani zao lakini waliotoka nje waliishia milangoni mwao tu hakuna aliyesoge

Mimi nikatoka nikasogea eneo ambalo kuna jamaa ni mafundi seremala. Nikiwaomba twende tukaamlie ugomvi watoto wamepiga kelele muda mrefu

Lengo langu na mimi ilikuwa kukwepa "kiherehere" kama mtoa mada alivyosema ili angalau tuwe wengi wengi

Ile kuingia ndani tukakuta "Hamadiii" mama wa watu yuko uchi kama alivyozaliwa kamakalia jamaa kifuani anaminya shingo jamaa katoa macho kuhema hawezi. Watoto wanalia "Baba anamchinja Mama" kumbe Mama ndo anamchinja Baba na kweli tusingeingia ndani muda ule huenda madhara makubwa yangetokea maana jamaa alikuwa kalewa hana uwezo wa kujitete na kisa cha ugomvi jamaa amerudi kalewa wakati familia kaiacha bila chakula ndani Mama hasira zikampanda akaona ampe adabu kidogo

Baada ya kuamlia ule ugomvi na kufikisha taarifa kwa mjumbe wa mtaa, jamaa alienda kuwashukuru wale fundi seremali kwa kuokoa uhai wake kwasababu ndio wanaofahamika zaidi pale kitaa. Wakamwambia wao waliogopa kuingilia ugomvi wasioujua wakasema mshukuru fulani aliyekuja kutushawishi (wakinitaja mimi) vinginevyo kwa hali tuliyoikuta ungekuwa historia sasa hivi

Ukiuliza kwanini watu hawakwenda kuamlia, ni kukwepa kutoa ushahidi tu hakuna kingine.

Kuna haja sana ya polisi na vyombo vya sheria kubadili mindset zao juu ya mashuhuda ili watu wasaidiane huku kitaa
 
Hakuna Idara HOVYO hapa Tanzania kama idara ya Polisi, Serikali imeshindwa kabisa kudhibiti idara hii, imeacha idara hii iendelee kuumiza watu badala ya kusaidia watu.

Hii inasikitisha na kuumiza sana mkuu watu walikuwa na moyo mzuri tu kusaidiana na polisi lakini wanajikuta wamefungwa wao badala yakwamba wasifiwe kwa kujitoa kwao inakuwa kinyume kbs
 
Hii hali ni mbaya sana. Juzi uswahili kwetu huku tulisikia makelele ya watoto "Baba ana mchinja Mama" muda wa jioni tu kama saa kumi na moja kasoro.Watoto wamepiga kelele wee hadi wanaita majina ya jirani zao lakini waliotoka nje waliishia milangoni mwao tu hakuna aliyesoge

Mimi nikatoka nikasogea eneo ambalo kuna jamaa ni mafundi seremala. Nikiwaomba twende tukaamlie ugomvi watoto wamepiga kelele muda mrefu

Lengo langu na mimi ilikuwa kukwepa "kiherehere" kama mtoa mada alivyosema ili angalau tuwe wengi wengi

Ile kuingia ndani tukakuta "Hamadiii" mama wa watu yuko uchi kama alivyozaliwa kamakalia jamaa kifuani anaminya shingo jamaa katoa macho kuhema hawezi. Watoto wanalia "Baba anamchinja Mama" kumbe Mama ndo anamchinja Baba na kweli tusingeingia ndani muda ule huenda madhara makubwa yangetokea maana jamaa alikuwa kalewa hana uwezo wa kujitete na kisa cha ugomvi jamaa amerudi kalewa wakati familia kaiacha bila chakula ndani Mama hasira zikampanda akaona ampe adabu kidogo

Baada ya kuamlia ule ugomvi na kufikisha taarifa kwa mjumbe wa mtaa, jamaa alienda kuwashukuru wale fundi seremali kwa kuokoa uhai wake kwasababu ndio wanaofahamika zaidi pale kitaa. Wakamwambia wao waliogopa kuingilia ugomvi wasioujua wakasema mshukuru fulani aliyekuja kutushawishi (wakinitaja mimi) vinginevyo kwa hali tuliyoikuta ungekuwa historia sasa hivi

Ukiuliza kwanini watu hawakwenda kuamlia, ni kukwepa kutoa ushahidi tu hakuna kingine.

Kuna haja sana ya polisi na vyombo vya sheria kubadili mindset zao juu ya mashuhuda ili watu wasaidiane huku kitaa

Hongera pia kwa ulicho kifanya maana ungeenda kichwa kichwa na wewe ingekuwa
 
Moja kati ya uzi bora kwa mwezi huu. Umeandika ukweli kabisa ndugu. Police ni maigizo sana, kiasi kwamba raia wanashindwa kuwapa ushirikiano kwenye mambo mengi tu. Na hili jambo ni la muda mrefu sana, sijui hata viongozi wao huwa wanalichukuliaje aisee. Inawezekana kuna uchawi huko Police kiasi kwamba ukiingia basi na akili zako zinakuwa tope kabisa maana hawabadiliki.
Saidi Mwema (Rtd Igp) alitaka kuliboresha Jeshi la Polisi kwa sera zake za Polisi jamii na 'shirikishi' lakini nadhani waliziona haziwaletei chakula mezani.
 
Form four failures unawapa majukumu ya kuangalia usalama wa wananchi na kulinda sheria za nchi halafu utegemee kutakuwa na weledi wa kutosha kwenye kazi....!!!!!!!🤒 😎

😂😂 Ni hatari yaani mimi naona kuna umuhimu wa hawa polisi kusomea saikolojia maana hawawezi kumtambua mtu nia yake nini kwa kujitoa kwake
 
Hii hali ni mbaya sana. Juzi uswahili kwetu huku tulisikia makelele ya watoto "Baba ana mchinja Mama" muda wa jioni tu kama saa kumi na moja kasoro.Watoto wamepiga kelele wee hadi wanaita majina ya jirani zao lakini waliotoka nje waliishia milangoni mwao tu hakuna aliyesoge

Mimi nikatoka nikasogea eneo ambalo kuna jamaa ni mafundi seremala. Nikiwaomba twende tukaamlie ugomvi watoto wamepiga kelele muda mrefu

Lengo langu na mimi ilikuwa kukwepa "kiherehere" kama mtoa mada alivyosema ili angalau tuwe wengi wengi

Ile kuingia ndani tukakuta "Hamadiii" mama wa watu yuko uchi kama alivyozaliwa kamakalia jamaa kifuani anaminya shingo jamaa katoa macho kuhema hawezi. Watoto wanalia "Baba anamchinja Mama" kumbe Mama ndo anamchinja Baba na kweli tusingeingia ndani muda ule huenda madhara makubwa yangetokea maana jamaa alikuwa kalewa hana uwezo wa kujitete na kisa cha ugomvi jamaa amerudi kalewa wakati familia kaiacha bila chakula ndani Mama hasira zikampanda akaona ampe adabu kidogo

Baada ya kuamlia ule ugomvi na kufikisha taarifa kwa mjumbe wa mtaa, jamaa alienda kuwashukuru wale fundi seremali kwa kuokoa uhai wake kwasababu ndio wanaofahamika zaidi pale kitaa. Wakamwambia wao waliogopa kuingilia ugomvi wasioujua wakasema mshukuru fulani aliyekuja kutushawishi (wakinitaja mimi) vinginevyo kwa hali tuliyoikuta ungekuwa historia sasa hivi

Ukiuliza kwanini watu hawakwenda kuamlia, ni kukwepa kutoa ushahidi tu hakuna kingine.

Kuna haja sana ya polisi na vyombo vya sheria kubadili mindset zao juu ya mashuhuda ili watu wasaidiane huku kitaa
Ila safi huyo baba kunyooshwa, unaacha familia iteseke njaa afu hela unaenda kunywea pombee? Ilimbidi huyo mama amminye hilo tumbo atapike pombe yotee.

Shenzzzy zake.
 
Ukitoa taarifa polisi ya labda muhalifu wa mtaani, na wao wanamfata mhalifu wanamwuliza unaishi vipi na wenzako mtaani! Maana ndio wametupa taarifa zako.
Hapo ni baada ya kuchukua hela ya kiwi.

Ni hatar sana
 
Hakuna Idara HOVYO hapa Tanzania kama idara ya Polisi, Serikali imeshindwa kabisa kudhibiti idara hii, imeacha idara hii iendelee kuumiza watu badala ya kusaidia watu.
Jeshi lilioundwa ili kumtumikia mkoloni bado sera ni hizo hizo utegemee mabadiriko?? Si bora kidogo hata Kenya kwa sasa kuna unafuu!! Jeshi linaloamini vitisho zaidi
 
Back
Top Bottom