Riba ya Benki Kuu yaongezwa hadi 6% kukabiliana na Mfumuko wa Bei

Dalton elijah

JF-Expert Member
Jul 19, 2022
213
474
1712248069807.jpg

Katika hatua muhimu ya kukabiliana na shinikizo la mfumuko wa bei linalotokana na mwenendo wa uchumi duniani, Kamati ya Sera ya Fedha (MPC) imetangaza ongezeko la Kiwango cha Riba ya Benki Kuu (CBR) kutoka asilimia 5.5 hadi asilimia 6.

Uamuzi huu, umefikiwa wakati wa kikao cha MPC kilichofanyika tarehe 3 Aprili 2024 kwa kuzingatia tathmini ya mwelekeo wa uchumi iiliyofanyika mwezi Machi 2024.

Akitoa taarifa ya kamati hiyo katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya Benki Kuu Dar es Salaam mbele ya wakuu wa taasisi za fedha na vyombo vya habari, Gavana wa Benki Kuu, Bw. Emmanuel Tutuba amesema marekebisho ya CBR yatakayotekelezwa kwa robo ya pili ya mwaka huu, yaani Aprili hadi Juni 2024, yamo ndani ya wigo wa asilimia 2 juu na chini.

Hatua hii inaonyesha azma ya benki kuu katika kudumisha utulivu katika mabadiliko ya uchumi.

Tathmini ya MPC kuhusu hali ya uchumi duniani inaonyesha mwelekeo mzuri, huku uchumi wa nchi zilizoendelea na zinazoibukia ukiwa na mwenendo bora.

Akizungumza baada ya kutangazwa kwa CBR, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabenki Tanzania, Bw. Theobald Sabi, aliipongeza Benki Kuu ya Tanzania kwa kuja na kiwango hicho kinachozingatia mazingira ya sasa hivi.

Pia aliishukuru Benki Kuu ya Tanzania kwa ushirikiano wake inaotoa katika maeneo mbalimbali yenye changamoto katika sekta ya mabenki, likiwemo tatizo la upatikanaji wa fedha za kigeni.
 
Bank za biashara zinafaidikaje?

Kwamba wakikopeshwa na BOT KWA 5.5% ikiwa ni ongezeko la 0.5% na wao hiyo pesa watawakopesha Watu KWA riba ya juu tofauti na zamani? Mfano 13% mpaka 15% ?

Maana huyo jamaa Theobald kutoka NBC ameshukuru na kupongeza hatua hiyo
 
Katika Hali ya kushangaza leo April 4 Gavana wa bank kuu ndugu Emanuel Tutuba ameongea na wahariri wa vyombo vya habari na kueleza hatua zinazochukuliwa na bank kuu kudhibiti mfumuko wa bei yani inflation ) na hii riba nikwa bank zinazokopa pesa kwake husasan hzi bank za biashara

Imepandisha kutoa asilimia tano 5% Hadi kufika 6% na hii itabaki Hadi july 24 2024 na lengo kubwa ni kudhibiti tu mfumo wa Bei kwa miez hi Happ

Sasa nauliza wasomi wanauchumi kutoka UDSM na UDOM walioko hapa ambapo naamini kbsa wako manguli wa Mambo ya uchumi humu wanaweza kunieleza au kufafanua Kama Hili Ni sawa au BOT wamezingua

Nin. Maanake kiuchumi

Kama hujui Mambo ya uchumi kaa pembeni subiria mada zingine au sepa kbsa Niko na wanauchumi wa udsm na udom
 
Wameongeza kupunguza mzunguko wa fedha huku nje!

Kwamba pesa ni nyingi kiasi hiki? Mbona watu tunazitafuta hatuzioni na hali ni ngumu watu hatununui vitu hovyo sababu pesa hatuna...

Labda sababu ya mfumuko wa bei, wanataka kushusha.

Hii njia walioichagua itazidi kutuumiza wananchi, atleast wangetumia njia ya kuuza goverment securities.
 
katk Hali ya kushangaza leo April 4 gavana wa bank kuu ndugu Emanuel Tutuba ameongea na wahariri wa vyombo vya habari na kueleza hatua zinazochukuliwa na bank kuu kudhibiti mfumuko wa bei yani inflation ) na hii riba nikwa bank zinazokopa pesa kwake husasan hzi bank za biashara

Imepandisha kutoa asilimia tano 5% Hadi kufika 6% na hi itabaki Hadi july 24 2024 na lengo kubwa Ni kudhibiti tu mfumo wa Bei kwa miez hi Happ

SAS nauliza wasomi wanauchumi kutoka UDSM NA UDOM walioko hapa ambapo naamini kbsa wako manguli wa Mambo ya uchumi humu wanaweza kunieleza au kufafanua Kama Hili Ni sawa au BOT wamezingua

Nin. Maanake kiuchumi

Kama hujii Mambo ya uchumi kaa pembeni subiria mada zingine au sepa kbsa Niko na wanauchumi wa udsm na udom
Kwa ufinyu wa akili yako unajua wasomi wapo udam na udom tu???!!!
 
When there's inflation a government through it's central bank it can reduce money circulation by implementing fiscal and monetary policies in an economy.

Monetary policy may include increasing interest rates in borrowing money by commercial banks , which may increase rates to reduce money in an economy hence curbing of inflation.

Fiscal policy implementation may include selling of Govt stocks, securities, treasury bill, bonds at lower rate to reduce money supply in an economy hence reduction of inflation rate.

Also inflation may be reduced by increasing production in an economy to increase exports and reduce imports at the same time to strengthen the balance of payments.
 
Back
Top Bottom