Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 11,275
- 19,112
Nimeshangazwa sana na habari iliyopo kwamba Rais Samia alimuagiza Mkuu wa Polisi Mwanza kuzuia watu kufanya kongamano juu ya Katiba ya Jamhuri ya Tanzania; kwa malaka gani aliyo nayo Samia juu ya Katiba? Je Rais Samia haelewi kwamba japo ana mamlaka ya Uraisi wa Tanzania, uraisi wa Tanzania haumpi mamlaka au umiliki juu ya Katiba kwa kuwa Katiba ya ni ya kila mtanzania?
Na kama Katiba haina mmiliki anaewazidi umiliki Watanzania wengine, suala la Raisi Samia kuzuia watu kukutana na kujadili katiba yao, linatoka wapi? Je, Rais Samia inawezekana kwamba kutoa kiapo cha kuisimamia na kuilinda Katiba ya Tanzania anafikirri maana yake atailinda watu wasiijadili? Ikiwa ndivyo, basi kuna uhitaji wa haraka sana wa kumwelimisha Raisi Samia nini maana ya kuisimamia na kuilinda katiba ya Tanzania. Rais anapaswa kuelimishwa kwamba kuilinda Katiba ya Tanzania maana yake ni kuhakikisha Tanzania kama nchi inaendeshwa kulingana na misingi iliyo ndani ya Katiba, na pale inapoonekana kuna watu wanakiuka hiyo msingi basi anapaswa kuchuka hatua.
Kitendo cha Raisi Samia kuzuia watu kujadili katiba ambayo wana haki na umiliki nayo huko si kuilinda Katiba hata kidogo, na asije akadhani anailinda. Kwa kuwa kila mtu ana haki ya Katiba ya Tanzania, kila mtu ana haki ya kuijadili na mtu mwingine aliye tayari kuijadili pamoja nae, iwe ni watu wawili au maelfu, ili mradi katika kufanya hivyo hawavunji sheraia na wanafanya kwa amani na utulivu. Kitu ambacho hakitaruhusiwa ni mtu yeyote kulazimisha watu wengine waibadili Katiba kulingana na anavyotaka yeye. Lakini ikiwa atataka kuijadili Katiba akiwa na watu wengine kwa lengo la kupendekeza mabdailiko kupitia utaratibu unaokubalika wa kubadili Katiba, si Raisi wala Mkuu wa Polisi wa Mkoa, au hata waziri wa Katiba na Sheria ana mamlaka ya kumzuia huyo mtu.
Kwa hiyo basi, wito kwa Raisi Samia, usijmilikishe Katiba ya Tanzania, na usidhani kwamba kiapo ulichofanya cha kuilinda Katiba maana yake uwazuie wale wanaotaka kuiongelea wasiiongelee. Na pia unapaswa kuelewa wazi sana kwamba kuwa kwako Raisi wa Tanzania kupitia CCM hakuipi CCM mamalaka juu ya Katiba ya Tanzania kuzidi Chadema, au TLP au chama kingine chochote cha siasa. Vyama vyote vya siasa vina haki sawa juu ya Katiba kama vile tu ilivyo kwa Mtanzania moja mmoja.
Umiliki wako Raisi Samia wa Katiba ya Tanzania hauongezewi nguvu na wewe kuwa Raisi wa Tanzania, kwa kuwa una haki sawa juu ya umiliki wa Katiba na mtanzania mwingine yeyote. Tofauti ni kwamba wewe una mamlaka ya kuhakikisha mambo yanafanyika nchini kwa kufuata misingi ya Katiba. Kwa hiyo kama ambavyo mimi sina mamlaka ya kumzuia mtu kujadili Katiba na mtu mwingine, ndivyo na wewe hupaswi kuwa na mamlaka hayo, kwa kuwa mimi na wewe sio wamiliki wa hii Katiba kuliko Watanzania wenzetu.
Kwa hiyo Raisi Samia tafadhali usilete matatizo pale ambapo matatizo hayapo. Kama watu wameamua kujadili katiba ambayo kimsingi ni ya kwao waache wajadili kwa uhuru. Na kama watakuwa na jambo la kuwaambia Watanzania wengine ni kitu gani wamejadili na wanapendekeza nini, tutawasikiliza, na tunaweza kukubaliana na mawazo yao au kutokubaliana, kwa sababu wao hawana umiliki wa Katiba tofauti na sisi wengine ambao hatukuwapo kwenye mjadala wao, na wala haitulazimu kuwapo kwenye mjadala wao.
Na kama Katiba haina mmiliki anaewazidi umiliki Watanzania wengine, suala la Raisi Samia kuzuia watu kukutana na kujadili katiba yao, linatoka wapi? Je, Rais Samia inawezekana kwamba kutoa kiapo cha kuisimamia na kuilinda Katiba ya Tanzania anafikirri maana yake atailinda watu wasiijadili? Ikiwa ndivyo, basi kuna uhitaji wa haraka sana wa kumwelimisha Raisi Samia nini maana ya kuisimamia na kuilinda katiba ya Tanzania. Rais anapaswa kuelimishwa kwamba kuilinda Katiba ya Tanzania maana yake ni kuhakikisha Tanzania kama nchi inaendeshwa kulingana na misingi iliyo ndani ya Katiba, na pale inapoonekana kuna watu wanakiuka hiyo msingi basi anapaswa kuchuka hatua.
Kitendo cha Raisi Samia kuzuia watu kujadili katiba ambayo wana haki na umiliki nayo huko si kuilinda Katiba hata kidogo, na asije akadhani anailinda. Kwa kuwa kila mtu ana haki ya Katiba ya Tanzania, kila mtu ana haki ya kuijadili na mtu mwingine aliye tayari kuijadili pamoja nae, iwe ni watu wawili au maelfu, ili mradi katika kufanya hivyo hawavunji sheraia na wanafanya kwa amani na utulivu. Kitu ambacho hakitaruhusiwa ni mtu yeyote kulazimisha watu wengine waibadili Katiba kulingana na anavyotaka yeye. Lakini ikiwa atataka kuijadili Katiba akiwa na watu wengine kwa lengo la kupendekeza mabdailiko kupitia utaratibu unaokubalika wa kubadili Katiba, si Raisi wala Mkuu wa Polisi wa Mkoa, au hata waziri wa Katiba na Sheria ana mamlaka ya kumzuia huyo mtu.
Kwa hiyo basi, wito kwa Raisi Samia, usijmilikishe Katiba ya Tanzania, na usidhani kwamba kiapo ulichofanya cha kuilinda Katiba maana yake uwazuie wale wanaotaka kuiongelea wasiiongelee. Na pia unapaswa kuelewa wazi sana kwamba kuwa kwako Raisi wa Tanzania kupitia CCM hakuipi CCM mamalaka juu ya Katiba ya Tanzania kuzidi Chadema, au TLP au chama kingine chochote cha siasa. Vyama vyote vya siasa vina haki sawa juu ya Katiba kama vile tu ilivyo kwa Mtanzania moja mmoja.
Umiliki wako Raisi Samia wa Katiba ya Tanzania hauongezewi nguvu na wewe kuwa Raisi wa Tanzania, kwa kuwa una haki sawa juu ya umiliki wa Katiba na mtanzania mwingine yeyote. Tofauti ni kwamba wewe una mamlaka ya kuhakikisha mambo yanafanyika nchini kwa kufuata misingi ya Katiba. Kwa hiyo kama ambavyo mimi sina mamlaka ya kumzuia mtu kujadili Katiba na mtu mwingine, ndivyo na wewe hupaswi kuwa na mamlaka hayo, kwa kuwa mimi na wewe sio wamiliki wa hii Katiba kuliko Watanzania wenzetu.
Kwa hiyo Raisi Samia tafadhali usilete matatizo pale ambapo matatizo hayapo. Kama watu wameamua kujadili katiba ambayo kimsingi ni ya kwao waache wajadili kwa uhuru. Na kama watakuwa na jambo la kuwaambia Watanzania wengine ni kitu gani wamejadili na wanapendekeza nini, tutawasikiliza, na tunaweza kukubaliana na mawazo yao au kutokubaliana, kwa sababu wao hawana umiliki wa Katiba tofauti na sisi wengine ambao hatukuwapo kwenye mjadala wao, na wala haitulazimu kuwapo kwenye mjadala wao.