Rais Samia: Ili kudhibiti rushwa barabarani, trafiki waondoke barabarani, kamera na taa ndio zifanye kazi

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
44,991
51,833
Rais Samia ameagiza kuanza kuondolewa Kwa Matrafiki ambao walijigeuza Wala Rushwa Barabarani badala yake ametaka zifungwe Kamera na Taa Ili Kuongoza magari.

---
Rais Samia Suluhu Hassan amesema katika kukabiliana na rushwa nchini, trafiki barabarani wanapaswa kuondolewa badala yake taa na kamera zitatumika kuongoza barabarani.

Rais Samia ameyasema hayo leo, Ikulu jijini Dar es Salaam katika hafla ya kuapisha viongozi wateule wa ngazi mbalimbali za uongozi nchini

“Usalama barabarani, tunataka kuondoa trafiki barabarani kukomesha rushwa. Tuyaache mambo ya pita wewe nenda wewe”


My Take
Naunga mkono hoja ya Mh.Rais.

Trafiki waligeuza usalama Barabarani kuwa mradi wa kuvuna pesa za Rushwa Kwa maderva huku ajali na makosa mengine yakizidi kuongezeka.

Kenya wameweza na sisi tuanze maana tulichepewa sana.

Tukitoka hapo tufungue kamela kwenye Mahospitali na kuwavalisha kamela maafisa wa TRA.
 
KWa taa hiz hiz zinazotegemea solar na maintenance ya kuunga unga?.
Nafikiri tuboreshe kwanza maeneo muhimu ila automation ifanye kazinkwa ufanis kurahisisha maisha
Tatizo dogo sana hilo kwa serikali kama itaamua. Mikoa yote mikubwa wafanye hii kitu. Makosa ya barabarani yatambuliwe kwa Camera. Polisi kazi yao iwe kukamata magari yenye fain sio kuziingiza hizo fain.
 
Zitatengewa pesa ya kutosha ya maintenance.

Dunia yote inatumia taa za solar Wala hakuna shida.
Ni sahihi. Umeme wa uhakika na ubora wa vifaa tumika ni preliquisites muhim sana kwenye hili na hilo wenzetu hilizingatia ndio maana wakisha hama huko.

Sisi mambo yale ya 10% kwenye tendering bado yanatutafuna sana
 
Tatizo dogo sana hilo kwa serikali kama itaamua. Mikoa yote mikubwa wafanye hii kitu. Makosa ya barabarani yatambuliwe kwa Camera. Polisi kazi yao iwe kukamata magari yenye fain sio kuziingiza hizo fain.
Hapo kwenye kuamua ndio ulipo mzizi wa fitina.
Ujue kama tungeamua, tusingekua hapa leo hii kama taifa. Ni kama China au Singapore walivyoamua
 
Rais Samia ameagiza kuanza kuondolewa Kwa Matrafiki ambao walijigeuza Wala Rushwa Barabarani badala yake ametaka zifungwe Kamera na Taa Ili Kuongoza magari.

View: https://www.instagram.com/p/C5VjILqt4nW/?igsh=eXJuZWZwZGI2MWlw

My Take
Naunga mkono hoja ya Mh.Rais.

Trafiki waligeuza usalama Barabarani kuwa mradi wa kuvuna pesa za Rushwa Kwa maderva huku ajali na makosa mengine yakizidi kuongezeka.

Kenya wameweza na sisi tuanze maana tulichepewa sana.

Tukitoka hapo tufungue kamela kwenye Mahospitali na kuwavalisha kamela maafisa wa TRA.


FW9WY_7WAAAAxoa.jpeg

FuZjb2aXwAQYywO.jpeg
 
Hapo kwenye kuamua ndio ulipo mzizi wa fitina.
Ujue kama tungeamua, tusingekua hapa leo hii kama taifa. Ni kama China au Singapore walivyoamua
Kwenye hili uwezekano ni mkubwa litafanyika sababu ni chanzo cha mapato. Kuna faini nyingi sana zinaishia mikononi mwa trafic.
 
Hapa kwetu ni mapato na huenda yapo kwenye bajeti. Hujawahi sikia askari mbele ya camera anasema tumevuka lengo la makusanyo barabarani?
Kamera hazitazuia faini kuwa Mapato,swala ni kuondoa Trafiki
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Back
Top Bottom