Rais Samia, hii Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ina ukakasi kidogo

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,727
29,970
Amani iwe kwako mkuu wangu wa nchi.

Nimeweka heading hiyo kuweza kukuvutia kusoma usuli wa hoja yangu.

Sote tunafahamu kwa Mujibu wa Katiba kuwa tasisi unayoiongoza imepewa mamlaka ya kuunda, kupangua ama kufuta wizara mbalimbali za serikali hasa kutokana na mahitaji ya nchi kwa wakati husika.

Umeunda wizara mahususi ya kushughulika na hitaji kubwa la ustawi na maendeleo ya kisekta kwa kulenga jamii hususan makundi yaliyo kwenye wskati mgumu kijamii ambayo ni wanawake, watoto na wenye ulemavu. Naongekea wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wanawake na Makundi Maalum. Nimeweka hapa chini screenshot ya banner la wizara lililopo kwenye interface ya tovuti ya wizara
Screenshot_20230312_102147_Chrome.jpg


UKAKASI
Nimetafakari jina la Wizara ni kama linaleta ukakasi zaidi kwa muktadha wake.

Je neno JINSIA lilimaanisha nini ama aina gani ya jinsia zilizopo ndani ya neno hilo? Nimeona Jinsia imetajwa kisha mbeleni naona Wanawake wanatajwa nje ya jinsia. Ingesomeka wanaume badala ya jinsia ili kubeba mantiki ya neno wanawake mbeleni hapo.

Neno lingine ni makundi maalumu. Ambapo sisi raia wako tunaamini makundi maalumu ni wanawake, watoto na wenye ulemavu. Najiuliza kama jinsia lipo, wanawake wapo hapo kwenye makundi maalumu tunamaanisha makundi gani?

USHAURI
Nikiulizwa kuwa napendekeza jina lisomekaje nitajibu Jina la Wizara litapendeza likisomeka WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WATOTO NA WENYE ULEMAVU.

Nimetoa hoja
 
Jina la kimchakato tu hilo, usijali sana.

We umeshawahi kudhani kuwa neno RAIS ni sahihi? Au ni neno la lugha gani?
Mkuu njoo na hoja sahihi kuhusu neno Raisi.

Mimi naongelea jina la Wizara ambapo hubeba majukumu, malengo na matarajio ya sekta husika.

Katika uundaji wa sentensi au aya huwa tunaona kurudiarudia neno ni kukosa ubunifu sahihi na kuishiwa kwa vocabularies
 
Uko sahihi mkuu ukisema jinsia ni wanawake na wanaume halafu pi makundi maalum vilema watoto wazee na wanawake pia kwa hyo?? Hyo jinsia inasimamia Nini wabadilishe kwa kwel
Inawezekana kuna makundi maalum hawana jinsia au kwenye jinsia labda kuna zaidi ya wanaume na wanawake
 
Mleta mada umeongea jambo lenye mantiki. Pia chini ya ofisi ya Waziri Mkuu, kuna component ya "wenye ulemavu" hivyo ni vizuri serikali ikayaweka vizuri haya kuepuka utata.
 
Neno ‘walemavu’ ni political incorrect dunia ya leo.

Walemavu lina negative connotation ya watu wasiojiweza na kuchochea stigma ndani ya jamii zinazochangia hilo kundi kutopata ajira, waajiri kutoweka mazingira ya ku accommodate walemavu and so on.

Wakati kundi lenye watu wenye mahitaji maalum ni more positive lina ashiria serikali ikitengeneza sera nzuri, so called walemavu wanaweza ishi independent lives with minimal support, mfano ukiweka rump kila jengo la ofisi na lift ata mlemavu anaweza fanya kazi, mabasi yakiwa na eneo la walemavu na rumps wanaweza safiri wenyewe.

Story ni ndefu mzizi wa neno kundi la watu wenye ‘mahitaji maalum’, badala ya kuita walemavu ni ‘social model of disability’ ukipatia arguments zao utaona kwanini neno walemavu ni somewhat political incorrect; but then hizo ni siasa za first world on moral issues na wana hela ya ku implement hizo sera zao na ku-reinforce.
 
Amani iwe kwako mkuu wangu wa nchi.

Nimeweka heading hiyo kuweza kukuvutia kusoma usuli wa hoja yangu.

Sote tunafahamu kwa Mujibu wa Katiba kuwa tasisi unayoiongoza imepewa mamlaka ya kuunda, kupangua ama kufuta wizara mbalimbali za serikali hasa kutokana na mahitaji ya nchi kwa wakati husika.

Umeunda wizara mahususi ya kushughulika na hitaji kubwa la ustawi na maendeleo ya kisekta kwa kulenga jamii hususan makundi yaliyo kwenye wskati mgumu kijamii ambayo ni wanawake, watoto na wenye ulemavu. Naongekea wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wanawake na Makundi Maalum. Nimeweka hapa chini screenshot ya banner la wizara lililopo kwenye interface ya tovuti ya wizara
View attachment 2547166

UKAKASI
Nimetafakari jina la Wizara ni kama linaleta ukakasi zaidi kwa muktadha wake.

Je neno JINSIA lilimaanisha nini ama aina gani ya jinsia zilizopo ndani ya neno hilo? Nimeona Jinsia imetajwa kisha mbeleni naona Wanawake wanatajwa nje ya jinsia. Ingesomeka wanaume badala ya jinsia ili kubeba mantiki ya neno wanawake mbeleni hapo.

Neno lingine ni makundi maalumu. Ambapo sisi raia wako tunaamini makundi maalumu ni wanawake, watoto na wenye ulemavu. Najiuliza kama jinsia lipo, wanawake wapo hapo kwenye makundi maalumu tunamaanisha makundi gani?

USHAURI
Nikiulizwa kuwa napendekeza jina lisomekaje nitajibu Jina la Wizara litapendeza likisomeka WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WATOTO NA WENYE ULEMAVU.

Nimetoa hoja
Makundi maalum kwasasa kwenye medani za kimataifa sio walemavu, wanawake na watoto tena bali ni LGBTQ
 
Kwanza kwanini iwepo wizara ya wanawake?
Kiuhalisia kunajambo gani hasa ambalo linawagusa mojakwamoja mpaka kulitengea wizara?
Siniwakati wa haki sawa? Sasa mbona tena wanaundiwa wizara yao?

Au niridhiketu kwa kua hata siku yao ipo inatambulika kimataifa?
Changamoto za wanawake ni nyingi kwanza ndio primary carers ndani ya family, baba akitoroka mtoto ana baki na mama; sasa hapo kunakuwa na welfare ya mtoto pia.

Fanya research yako utagundua asilimia kubwa ya watoto wanaoenda ovyo utabaini hakuna malezi ya baba.

Pili wanawake ni weak na most likely to receive abuse so kunahitajika special intervention approaches za kupambana na abuse at work na majumbani.

Anyway haya mambo ni moral issues za developed nations, na sehemu kubwa ya uendeshaji wa hiyo wizara ni team work ya wizara yenyewe, afya, elimu, jeshi la polisi na local government; kubwa zaidi media propaganda hii shughuli ndio asilimia kubwa ya mafanikio and how messages are packaged.

Sina shaka Dorothy Gwajima ni very clever afya, lakini hapo ukiona wanavyofanya kazi ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu abuse aziwezi punguzwa bila heavy investment on propaganda na adhabu kali sana kila mtu ajue.
 
Hivi serikali kupitia hii wizara haiwezi kuwapa makazi na shughuli hat za kilimo hawa ombaomba wote walio barabarani, wauza tissue, wanaokimbilia kusafisha vioo vya magari kwa maji machafu yenye sabuni.

Societal welfare system fulani itumike kuwaondoa hata kwa nguvu kwenye traffic lights
 
Changamoto za wanawake ni nyingi kwanza ndio primary carers ndani ya family, baba akitoroka mtoto ana baki na mama; sasa hapo kunakuwa na welfare ya mtoto pia...
Nimefurahia sana mrejesho wako ambao umejibu baadhi ya hoja mkuu, barikiwa kila uchao na uchwao.

Sema wizara yenye makundi maalum nayo ina waziri anayeendana na wizara yake
Hongera mh. Rais kwa kuona mbali
 
Kwanza kwanini iwepo wizara ya wanawake?
Kiuhalisia kunajambo gani hasa ambalo linawagusa mojakwamoja mpaka kulitengea wizara?
Siniwakati wa haki sawa? Sasa mbona tena wanaundiwa wizara yao?

Au niridhiketu kwa kua hata siku yao ipo inatambulika kimataifa?
Ni muhimu ikawepo kwa malengo chanya ya kujenga usawa kwenye jamii.
Kuna shida kubwa eneo la familia ambapo savages wanalelewa kuwa future fathers na kuja kuwatesa wake zao.

uwepo wa wizara hii ni matokeo ya failures za serikali na jamii kwa kuamua kufuta mafunzo ya awali ya kimila kwa vijana na badala ya kuyaboresha waliyafuta kabisa. tunahitaji kujitafakari
 
Neno ‘walemavu’ ni political incorrect dunia ya leo.

Walemavu lina negative connotation ya watu wasiojiweza na kuchochea stigma ndani ya jamii zinazochangia hilo kundi kutopata ajira, waajiri kutoweka mazingira ya ku accommodate walemavu and so on.

Wakati kundi lenye watu wenye mahitaji maalum ni more positive lina ashiria serikali ikitengeneza sera nzuri, so called walemavu wanaweza ishi independent lives with minimal support, mfano ukiweka rump kila jengo la ofisi na lift ata mlemavu anaweza fanya kazi, mabasi yakiwa na eneo la walemavu na rumps wanaweza safiri wenyewe.


Story ni ndefu mzizi wa neno kundi la watu wenye ‘mahitaji maalum’, badala ya kuita walemavu ni ‘social model of disability’ ukipatia arguments zao utaona kwanini neno walemavu ni somewhat political incorrect; but then hizo ni siasa za first world on moral issues na wana hela ya ku implement hizo sera zao na ku-reinforce.
hapo kwenye bold

Unyanyapaa ni hata kujikataa ulivyo na kujisikia inferior kwa hali halisi uliyonayo.
Unapofikia mahala neno disabled likaonekana negative basi hata mtu mzima nalo ni neno dhalili kabisa.
Kwa mfano neno Zeruzeru ambapo ni mtu mwenye ulemavu wa ngozi tumeliona ni tusi badala yake tunasema albinism ambapo tafsiri yake ni zeruzeru.

Kutojitambua na kukubaliana na hali yako hakukuweki mbali na kujinyanyapaa
 
Mleta mada umeongea jambo lenye mantiki. Pia chini ya ofisi ya Waziri Mkuu, kuna component ya "wenye ulemavu" hivyo ni vizuri serikali ikayaweka vizuri haya kuepuka utata.
Naamini kwa busara ya Taasisi ya Rais iangalie namna ya kuyaweka sawa haya mambo kimfumo wa kutawala
 
Amani iwe kwako mkuu wangu wa nchi.

Nimeweka heading hiyo kuweza kukuvutia kusoma usuli wa hoja yangu.

Sote tunafahamu kwa Mujibu wa Katiba kuwa tasisi unayoiongoza imepewa mamlaka ya kuunda, kupangua ama kufuta wizara mbalimbali za serikali hasa kutokana na mahitaji ya nchi kwa wakati husika.

Umeunda wizara mahususi ya kushughulika na hitaji kubwa la ustawi na maendeleo ya kisekta kwa kulenga jamii hususan makundi yaliyo kwenye wskati mgumu kijamii ambayo ni wanawake, watoto na wenye ulemavu. Naongekea wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wanawake na Makundi Maalum. Nimeweka hapa chini screenshot ya banner la wizara lililopo kwenye interface ya tovuti ya wizara
View attachment 2547166

UKAKASI
Nimetafakari jina la Wizara ni kama linaleta ukakasi zaidi kwa muktadha wake.

Je neno JINSIA lilimaanisha nini ama aina gani ya jinsia zilizopo ndani ya neno hilo? Nimeona Jinsia imetajwa kisha mbeleni naona Wanawake wanatajwa nje ya jinsia. Ingesomeka wanaume badala ya jinsia ili kubeba mantiki ya neno wanawake mbeleni hapo.

Neno lingine ni makundi maalumu. Ambapo sisi raia wako tunaamini makundi maalumu ni wanawake, watoto na wenye ulemavu. Najiuliza kama jinsia lipo, wanawake wapo hapo kwenye makundi maalumu tunamaanisha makundi gani?

USHAURI
Nikiulizwa kuwa napendekeza jina lisomekaje nitajibu Jina la Wizara litapendeza likisomeka WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WATOTO NA WENYE ULEMAVU.

Nimetoa hoja
😁 ngoja nicheke kwanza. Ok kwahiyo watoto hawana jinsia, walemavu sio watoto... wizara ya mchongo
 
hapo kwenye bold

Unyanyapaa ni hata kujikataa ulivyo na kujisikia inferior kwa hali halisi uliyonayo.
Unapofikia mahala neno disabled likaonekana negative basi hata mtu mzima nalo ni neno dhalili kabisa.
Kwa mfano neno Zeruzeru ambapo ni mtu mwenye ulemavu wa ngozi tumeliona ni tusi badala yake tunasema albinism ambapo tafsiri yake ni zeruzeru.

Kutojitambua na kukubaliana na hali yako hakukuweki mbali na kujinyanyapaa
Sa mazeruzeru waende ulaya ndo waitwe hivo
 
Inawezekana kuna makundi maalum hawana jinsia au kwenye jinsia labda kuna zaidi ya wanaume na wanawake
Kuna mtu hana jinsia japo mwenyewe amejiweka kwa wanawake lakini ukweli sio mwanamke wala sio mwanaume kwa sababu hana sehemu ya siri ya mwanamke wala mwanaume bali ana kitundu tu cha kutolea haja ndogo.
 
Ni muhimu ikawepo kwa malengo chanya ya kujenga usawa kwenye jamii.
Kuna shida kubwa eneo la familia ambapo savages wanalelewa kuwa future fathers na kuja kuwatesa wake zao.

uwepo wa wizara hii ni matokeo ya failures za serikali na jamii kwa kuamua kufuta mafunzo ya awali ya kimila kwa vijana na badala ya kuyaboresha waliyafuta kabisa. tunahitaji kujitafakari
Serikali inabugi mambo mengi sana.. serikali iko na mambo ya ajabu sana. Upigaji tu
 
Back
Top Bottom