Kwahiyo hata huyo anaewauzia (Ridhwani) naye atakuwepo?Rais Kikwete amefanya mazungumzo na vijana wabwia unga (Mateja) Ikulu jijini Dar es salaam na kuwataka waachane na tabia ya kubwia unga badala yake wawe raia wema kwa faida ya Taifa.
Mkutano huo wa JK na wabwia unga umefanyika jumanne Ikulu jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na mfadhili wa kituo kimoja cha kurekebisha wabwia Unga aitwaye Zacharia Hans Poppe.
Kweli Rais tunaye watanzania.
Mkuu nguvumali hata wewe unamshabikia Kagame? Tuanze kufuatilia faili la urai wako?
Itakapof£¿ka zamu ya akina dada poa mniambie..., tutashtuka kuambiwa na mabwabwa waliitwa wakaambiwa waache tabia hizo wakaze viuno wajenge taifa.. My shoes
bibikuku sikiliza,
kama huna uhakika na kitu unachokiandika usiwe unakurupuka kwa ajili ya
kuwapa watu hasira ili waelekeze lawana kwa rais.
Hivi moderators ........ Paw mnawezaje kuangalia mada kama hii inayoanzishwa ikiwa imepotosha kabisa lengo la rais kukutana na hawa jamaa ikulu jana.
Nazidi kufunguka kuwa mambo mengi yanayosemwa kuhusu rais ni ya uongo na uzushi.
copy Ritz
Wengi wao ni vijana wasio na kazi.Alichotakiwa ni kufanya uchunguzi wa sababu za vijana hao kujiingiza kwenye matumizi ya madawa hayo.Na katika uchunguzi,ndipo pia angefikia kwenye conclusion inayolenga pande zote,za hao aliopewa majina yao,pamoja na watumiaji kupewa counseling,reharbs na pia kujenga mazingira ya vijana kujiajiri ama kuajiriwa,na siyo kuspend pesa kudhibiti upinzani na nyingine kupeleka kwenye akaunti za nje.
Kweli kabisa maana anawafahamu kwani alishatangaza kuwa anawafahamu na orodha yao anayo!Kwanini asikutane na wauza unga pia?