Proper recording: Nini kilimbadili Mzee Mwanakijiji?

Sipendi shindana na wewe kwa vile hata kama nilifanya kitu kidogo sana bado nitakushinda

hujafanya kitu kwa sababu huna uwezo huo; badala ya na wewe kuwa sehemu kweli ya mabadiliko kupigana na ufisadi kiukweli umebakia kudhania watu ni maajenti. Ni uongo huu ambao umepandikizwa na wale ambao wanajua tumeshawashinda na tunaendelea kuwashinda - mafisadi. Katika hili hakuna mswalia mtume; wale ambao wanataka kuja kututawala tutawasimamia na kuwapima kabla hawajaja kututawala. Hatutawapa blank check kama unavyofanya wewe. Tunavyowabana watawala wa sasa walioshindwa ndivyo ambavyo tutawabana watawala wanaokuja. Hatuamini katika haki ya watu kututawala kama unavyoamini wewe.

Kwamba CDM kisihojiwe, kiachwe na kisiulizwe. Unataka watu wakikubalie chama kwa sababu tu kinaonekana kubeba matarajio na matumaini yao. Hili linaweza kuwavutia wengine wenye mtazamo wa kishabiki na wenye fikra zilizo dhaifu kama za kwako. Kwamba, chama cha siasa kinachota kuja kuiondoa CCM madarakani hakitakiwi kuulizwa, hakitiwi kupingwa, hakitakiwi kukosolewa au kuoneshwa udhaifu wake. Sidhani kama huku ni kukitakia mema.

Nadhani, unachofanya ni kuitakia CDM mabaya; hutaki ijipime, ijiangalie na kukosolewa ili ijijenge vizuri kulekea 2015. Unatak iende ikiwa katika udhaifu ambao tumeiona mara kwa mara. Wakati wengine tumekuwa katika vita hii dhidi ya ufisadi na tumeshashinda mara kadhaa na tunaendelea kushinda unakuja kama wewe usiye fanya lolote, usiyesaidia chama kwa lolote zaidi ya kutetea tu ili utetee na badala yake unataka kishindwe ili uwe wa kwanza kutaka kijipange tena 2020.

Sera za watu kama wewe zimeshindwa, mitazamo yenu imeshindwa, mikakati yenu imeumbuliwa na inaendelea kuumbuliwa na kufunuliwa kuwa ni dhaifu. Ni mikakati ya watu wasioona mbali. Mnataka CDM ishinde lakini ishinde kama kwa zawadi badala ya kupambana na kujipanga kweli kupambana. Baada ya kukusoma kwa muda mrefu na kukupima nimejiridhisha tu huna nafasi (kama hutobadilika) ya kuwa katika mwamko wa mabadiliko ambao tumeuasisi na kuutetea kwa gharama kubwa kuliko unavyoweza hata kuota kwenye njozi zako usiku. Wimbo wa kutaka CDM isijipange kabla ya 2015 tena mapema zaidi ni wimbo usio na kibwagizo; ridhim yake inakera.

Yeyote anayeitakia CDM mema; yeyote anayetaka CDM ishinde na siyo kushinda kirahisi tu bali kushika dola 2015 anapaswa na anatakiwa kuisimamia CDM kwa karibu zaidi, kuibana, kuilazimisha na hata kuisukuma itoke katika usingizi wa sifa ili iweze kujipanga upya na kiukweli. Katika kufanya hivyo wewee huwezi; huamini kuwa CDM inahitaji mabadiliko ili ishinde. Na hili ni ni tamanio la wana CCM wote kama wewe. Watu wote ambao hawataki mabadiliko ya kweli 2015 wanataka CDM iwe hivi hivi; ili ijikute kwenye migogoro ya kijinga, ili iweze kudhoofishwa.

Wachache wetu tumedhamiria kabisa kuwa kama CDM inataka kuja kuwa chama tawala basi itapita kwenye tanuru ya moto; itassafishwa, itajipanga na tutafanya yote yaliyo ndani ya uwezo wetu kuhakikisha kuwa chama hiki ambacho kimechota fikra za Watanzania kinajipa utayari wa kuja kuwaongoza. Natumaini utakuja upande huu na wewe utasimama na wale wanaotaka mabadiliko ya kweli, na utakuwa tayari kukisaidia chama hiki kushinda uchaguzi mkuu ujao na ule wa serikali za mitaa.

The end.
 
Pengine najenga dhana zangu vibaya (but i do as an individual) na I am open to be corrected.

Lakini maswali ni suala la lazima kwenye kutaka kufahamishwa (from my perspective of gaining information), CCM ni kundi la wahuni silikatai hilo. Na kuitoa madarakani kutokana na ufisadi ni motive tosha kwa jinsi inavyo behave kiubabe na kushindwa kuendesha Taifa.

Lakini I also need to be informed what those changes would look like realistically, kuitoa CCM ni mwanzo lakini pia kuna whole lot bunch of fisadi's in many sectors of our government organs. Some of whom who are not direct CCM members, you may find even CDM followers. The only different between these groups is they differ in the amounts they embezzle depending on their positions.

Maana kuna mpaka walimu wakuu wa primary kwenye shule za serikali ambao ni mafisadi wizi unaanzia hapo lakini unapanda mpaka kwa wakuu wa wizara to the Main players. The size of their taking will differ, but the habit is the same (sasa hao wa chini sio tatizo kweli).

The question still remains how are CDM going to end this mess, maana huwezi sema ufisadi wa mwl mkuu wa primary hau affect the services za hiyo shule.

Hapo sasa ndipo wengine wanapoiangalia CDM, people expect politics ambazo sasa zinazungumzia marekebisho kisera na si lawama za ufisadi, unaweza kumtoa CCM ukamwacha mwl akiendelea kupeta tu, tukawa pale pale for the most part in terms of improving the government services.

What policies are there do address this, huo ni mfano moja kwenye mia moja. Ndio sababu za kusema wasifiwe kwa jitihada zao but much is not in the open.

Mkuu hapo kwenye RED unafanya kosa moja kubwa sana. You are regarding CDM as a ruling party. Kuna roles za kuwa played na chama tawala na zingine zinabaki kuwa za opposition tu.

Ndiyo maana katika mjadala unaoendelea msimamo wangu ni wazi, CDM lazima ijipange na kuonesha beyond doubt kwamba iko tayari kutawala lakini hili lifanyike in covert. Kwa sasa wajikite kwenye general promises kwa wananchi juu ya mabadiliko makubwa nchini huku wakifichua maovu ya watawala na chama chao na ikiwezekana kuchukua hatua za kiharakati.
 
4881558 said:
watu wenye hasira za kitoto!, Wakikataliwa wafikiria kuua wengine! utakuwa utawala wa ajabu huo!
Japo siamini hili, ila pia sio la kuupuuzia!, nalitafakari sana haswa kwa kuzingatia ZZK is like a friend, (one has a duty to act on "what friends are for"!)
P.
 
Wachache wetu tumedhamiria kabisa kuwa kama CDM inataka kuja kuwa chama tawala basi itapita kwenye tanuru ya moto; itassafishwa, itajipanga na tutafanya yote yaliyo ndani ya uwezo wetu kuhakikisha kuwa chama hiki ambacho kimechota fikra za Watanzania kinajipa utayari wa kuja kuwaongoza. Natumaini utakuja upande huu na wewe utasimama na wale wanaotaka mabadiliko ya kweli, na utakuwa tayari kukisaidia chama hiki kushinda uchaguzi mkuu ujao na ule wa serikali za mitaa.
The end.
Siku zote nimekuwa nikisema humu jukwaani, kuwa Chadema ina wanachama, wafuasi, waumini na washabiki, miongoni mwao ni "washabiki maandazi" ambao kwao Chadema ni chama mkombozi na malaika, kimeshushwa duniani kutikomboa Watanzania kama yule MKOMBOZI, ambaye hata yeye alijaribiwa na kupitishwa kwenye tanuru la moto!.

At the end of the day, mtakuja kukuta, watu hasa wanaoisadia Chadema kiukweli, ni hawa wanaoikosoa na kuipitisha kwenye tanuru la moto, kuliko hata hawa wanaoiimbia nyimbo za sifa, shangwe na mapambio!.

Kwa upande wangu, mimi naendelea kuwa huru, sina chama, ila naendelea kusimama na mgombea wangu EL na ikishindikana ni Membe, Chadema angalieni mtamleta nani zaidi ya ZZK maana msimamo "Dr" mimi naujua!.
Pasco.
 
I like this last cry...louder than anything...!those who cry last cry the loudest....u cdm? kilio kama umenyng`anywa kadi..?si bure.wewe ni kama pasco tuuau umenyang`anywa ulaji? !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!ciao
 
Mkuu Nico, asking questions pia its an art!, hata ningekuwa mimi nisingejibu!, kuna watu wanatoa "statements" na kuziwekea question mark ili kuziita ni maswali, na kuanza kulazimishia majibu hizo statements!. MMKJ amekuheshimu sana kukujibu, mimi huwa sijibu kabisa!.
P.
 
This is very personal...duuh!

Hivi mods si wangefunga tu huu uzi....Nicholas and MMM should agree on disagreeing. Tumeshajua jinsi mlivyo na misimamo

yenu, msije anza matusi ya nguo sasa khaa!.
 
i like those who cry last cry the loudest...!!!!!!!!!!
The same applies to "he who laugh last, laugh most...!. The end justifies the means, its the end results that maters most not the means, 2015 inakuja, kuna watu watacheka na kuna watu watalia, atakaye cheka mwisho ndiye atakacheka zaidi na atakaye lia mwisho ndiye atakaye lia sana!.
 
This is very personal...duuh!

Hivi mods si wangefunga tu huu uzi....Nicholas and MMM should agree on disagreeing. Tumeshajua jinsi mlivyo na misimamo

yenu, msije anza matusi ya nguo sasa khaa!.

Kitwage, ni wasiwasi wako tuu, hawa wote ni ma great thinkes na wanapingana kwa hoja!, ila pia hujanote wote wawili wameshaanga rasmi?.

Alianza kuaga Mwanakijiji kwa kumkaribisha Niko upande wa mabadiliko!.
Natumaini utakuja upande huu na wewe utasimama na wale wanaotaka mabadiliko ya kweli, na utakuwa tayari kukisaidia chama hiki kushinda uchaguzi mkuu ujao na ule wa serikali za mitaa.

Ndipo akafuatia na Niko na kuaga Kiitaliano

i like this last cry...louder than anything...!those who cry last cry the loudest....u cdm? !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!ciao

Ni matumaini ya WOWOWO apost kuwa ameridhika tuendelee na mengine, ila kwenye mabishano haya, wa kujifunza, tumejifunza mengi!.

Pasco.
 
ala.. utoto ni upi sasa kama siyo wendawazimu huu; kuna namna ya kulipa uzito suala la ufisadi zaidi ya kuufichua na kuhakikisha watu wanawajibishwa? wewe unalipa vipi uzito suala la ufisadi? kuuchukia moyoni?

Hata kutembea na wake za watu ni ufisadi.
 
Hivi nyie mnao majdili Mwanakjiji hivi mnamjua mnamjadili nani?Huyo Mwanakijiji ana fananaje vile?Jina halisi ni nani?Mnataka awe afisa habari sijui mshauri wa Chadema akija hapa Tanzania au akiwepo Chadema atakuwa anatambulishwa kama Mwanakijiji au atakuwa off camera?Atakapo kuwa anataoa taarifa za Chadema atavaa mask?
 
Teh teh...mwenzetu ana theories nyingi sana,ila hajui ufisadi tuu wenyewe unatosha ondoa chama madarakani.Ndio maana nilimwambia kuondoa minyoo tuu kunatosha mfurahisha victim na kumpa uhuru kufikiria ajenge vipi afya yake.CCM wapo kama minyoo iliyokaa pale chakula kilichochunjwa kinapotakiwa nyonywa na mwili wa host.Wao hukuchukua chote.Hawezi pata picture kama anaishi maisha ya filamu na mizaha kama ya Michuzi wakati wengine wanaishi maisha ya kweli.Hapo juu mchangiaji kamuhesabia matawi mangapi kashiriki fungua...ila huyu jamaa hata kutumia hii platform na kalamu yake kuleta mabadiliko anakuwa mzuia mabadiliko.Im happy siku anaamka atakuta CCM haipo impe ujira wake.
Mushi na wadau wengine. Mimi binafsi kwa sehemu nakubaliana na MMKijiji kuhusu issue ya ufisadi kuiondoa ccm madarakani kuwa ni vigumu. Ni vema kujua kuwa, kwenye jamii kama ya kwetu ambayo maadili yameachwa kwa sehemu kubwa, ni vigumu kuitumia issue ya ufisadi pekee kama ndo TURUFU kuiondoa ccm madarakani. Si ajabu kuwasikia watu wakisema 'na sio fisadi nchi hii'. Ama the other time, baadhi ya viongozi wa dini walisema 'wale wanaopiga kelele za ifisadi ni kwa sababu wao wenyewe wamekosa fursa ya kufisidi ndo maana wanapiga kelele'. Whatever the case there is a need to find other issues which are very critical. Otherwise, neno ufisadi linaweza kuwa demystified kwa kueleza madhara yake kwa lugha nyepesi zaidi kuliko ilivyo sasa. Kwa watz walio wengi vijijini, ukimwambia ufisadi ataelewa but then swali litakuwa 'wwhat has that to do with me mtanzania wa kawaida kijijiji?". Na hao ndo majority wapiga kura!
 
kwamba congressmen/women wana access ya informaton ZOTE ZA NCHI, with all due respect Nicholas, hii sio kweli, hata romney kapata briefing kutoka US intelligence kuanzia september 17 not before.

Pia, kama naelewa vizuri nilichosoma, (unaweza kuona hii kwenye machapisho mbalimbali) hizo intelligence briefing hazipo kisheria, ni utamaduni tu wa wenzetu.
 
mapenzi ya kitu kwa binadamu yana ukomo usihukumu eti mtu 2006 alishabikia upande ule leo huu ukamuona msaliti vitu vinabadilika elimu inaongezeka maono yanapanuka maslahi ni ishu binafsi naomba nisimkwaze mtu hayo ni yangu kwa upeo wangu
 
Madai ya rafiki yangu mwanakijiji kuhusu Chadema naona yanafanana sana na ya Ndugu yetu Obama (failing president). Huwezi kuwa nje ya madaraka na ukasema every details of your plan kwa sababu unahitaji mechanism kubwa ( Gov machine ) kuweza kufanya hivyo. Serikali pamoja na kuwa kuwa na civil sevant kama laki tatu na ushee bado wanaleta budget mbovu isiyo na details wala ku add up. Leo mwanakijiji anataka Chadema waje na detailed plan ya hata usalama wa taifa watafanya wakati hawajawahi hata kupewa briefing kama wanavyofanya wenzetu kwa credible challengers.

Chadema tunachoitaji kutoka kwenu sasa hivi ni Vision yenu na detailed plan tutafanya watanzania wote. kuhusu nini tunataka kama nchi na sio nini viongozi wa chadema wanataka kama ilivyo sasa kwa CCM. Detail plan bila machinery na information itafanya wakina Pasco wapate cha kuongea na posho kubwa!


Tunachohitajikutoka kwa Chadema sasa, ni Vision, safu ya uongozi na nini wanakiamini kama chama(values)!
 
Mzee Mwanakijiji bandiko lako lote nimelisoma na kuna machache ya kuchangia kwani mengi yake ni ya kweli kabisa. Wengi wetu tunashindwa kujua kwamba kanuni ni kitu kinachojisimamia chenyewe na ukitaka kuifuata inakubali na ukiipinda yenyewe haipindiki bali kivuli chake ndicho kinachopindika!! Rules never bend!!

Kama taifa tunaposema kwamba tunachukia ufisadi tunakuwa tumeweka kanuni kwamba ufisadi hautakiwi Tanzania. Kwa hiyo haijalishi ni nani anatenda ufisadi bali ufisadi wenyewe ndiyo tatizo.

Kama kuna mtu ndani ya CHADEMA anapewa fedha za kufanya kitu fulani na mtu huyo akazitumia fedha hizo kwa matumizi yake binafsi basi bila shaka naye ni fisadi hata kama yuko CHADEMA.
 
Hivi CHADEMA hawana watu wengine wazuri zaidi wanaoweza kuitetea? Hoja ya Mzee Mwanakijiji ni kwamba CHADEMA wautumie mtaji wa watu walio nao kuwaeleza watafanya nini pindi watakapoingia madarakani. Kwa mfano mimi naiunga mkono CHADEMA kwenye sera yake ya utawala wa Majimbo lakini ni kina nani wanaweza kuja humu na kutueleza kwamba CHADEMA wakishika nchi wataigawanya nchi yetu katika majimbo mangapi na kigezo cha kugawa huko kitakuwa nini!!?

Haiwezekani kusema itajulikana mbele kwa mbele kwani uongozi wa nchi si sawa na tamthiliya ambamo waigizaji wanaokufa hufa ili igizo libebe maana halisi lakini wanaouwezo wa kufa mara nyingi kadri wanavyoshiriki kwenye Filamu au tamthiliya. Lakini madhara ya kuchagua uongozi wa nchi kwa sababu ya kuwa na "haki" yakupiga kura ni uendawazimu.

Lazima wanaotaka kututalawa waeleze wao wanasimamia nini kwenye maslahi ya makundi.
 
Last edited by a moderator:
Ndio nilikuwa najiuliza throughout the discussion.Kumbe umeliona eh?Punguza basi washupalia CDM, hamia pia kwa CCM na NCCR,CUF na wengine. Ndio usawa na haki ndugu yangu.

Hii comment imenishtua sana. Ulihitaji kujiuliza mara mbilimbili kabla ya kuandika hiki.
 
Back
Top Bottom