Mathanzua
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 16,011
- 20,935
Pension za wastaafu za kila mwezi kutoka hazina mpaka leo tarehe 4 May hazijalipwa. Je,zimepelekwa sikukuu ya wafanyakazi Mei Mosi?
Hakuna asiyejua adha ya wastaafu,hasa wale wanayopata pension zao za kila mwezi kutoka Hazina.Pension yao ni kidogo mno,na kupigia kwenye bandiko hili,ningeshauri pension hizi ziongezwe, ili angalau zifikie Sh.450,000 kwa mwezi, kwa maana ya Sh.15,000 kila siku.Hela hiyo haitoshi kumuwezesha mstaafu kuishi,lakini angalau ikifika Sh.450,000, itamuwezesha kupata mahitaji ya msingi.Naomba niseme wazi ukweli huu kwamba,kwa nchi yenye rasilimali nyingi kama Tanzania,hii inawezekana kabisa na hata zaidi,shida ni wizi,matumizi mabaya ya fedha na kuifanya nchi yetu kuwa shamba la bibi.
Lakini naomba pia nizungumzie swala la malipo ya pension hizi za wastaafu kutoka Hazina.Pension hizi ni ndogo sana kama ambavyo nimeainisha,lakini malipo yanakumbwa na changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na kuchelewa kulipwa kwa pesion zenyewe.Inawezekana kabisa malipo ya pension hizi yanachelewa kwa sababu nilizokwisha zitaja hapo juu, yaani wizi,matumizi mabaya ya fedha na kuifanya Tanzania kuwa shamba la bibi,mambo ambayo hayana budi kudhibitiwa.
Vyovyote vile iwavyo,pension hizi zinapaswa kulipwa kwa wakati,hasa kwa vile ni ndogo sana.Unamlipa mstaafu kiduchu,halafu kama hiyo haitoshi, unamcheleweshea kumlipa,hapana ni mbaya,ni kukosa utu,unfair na lack of moral values.
Mwisho niseme hivi, tatizo hili limekuwa sugu hasa kunapokuwa na sherehe za kitaifa,hii si mara ya kwanza.Mbona mishahara ya wafanyakazi inalipwa kwa wakati,hata kukiwa na sherehe za kitaifa,kwa nini isiwe hivyo kwa wastaafu?Hii ni dharau kwa wastaafu,ambao wamelitumikia taifa letu kwa muda mrefu,na jambo hili halipaswi kuwa entertained.Wafanyakazi wa hazina wanaowafanyia wastaafu uovu huu, wakumbuke kwamba ipo siku nao watastaafu.
Hakuna asiyejua adha ya wastaafu,hasa wale wanayopata pension zao za kila mwezi kutoka Hazina.Pension yao ni kidogo mno,na kupigia kwenye bandiko hili,ningeshauri pension hizi ziongezwe, ili angalau zifikie Sh.450,000 kwa mwezi, kwa maana ya Sh.15,000 kila siku.Hela hiyo haitoshi kumuwezesha mstaafu kuishi,lakini angalau ikifika Sh.450,000, itamuwezesha kupata mahitaji ya msingi.Naomba niseme wazi ukweli huu kwamba,kwa nchi yenye rasilimali nyingi kama Tanzania,hii inawezekana kabisa na hata zaidi,shida ni wizi,matumizi mabaya ya fedha na kuifanya nchi yetu kuwa shamba la bibi.
Lakini naomba pia nizungumzie swala la malipo ya pension hizi za wastaafu kutoka Hazina.Pension hizi ni ndogo sana kama ambavyo nimeainisha,lakini malipo yanakumbwa na changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na kuchelewa kulipwa kwa pesion zenyewe.Inawezekana kabisa malipo ya pension hizi yanachelewa kwa sababu nilizokwisha zitaja hapo juu, yaani wizi,matumizi mabaya ya fedha na kuifanya Tanzania kuwa shamba la bibi,mambo ambayo hayana budi kudhibitiwa.
Vyovyote vile iwavyo,pension hizi zinapaswa kulipwa kwa wakati,hasa kwa vile ni ndogo sana.Unamlipa mstaafu kiduchu,halafu kama hiyo haitoshi, unamcheleweshea kumlipa,hapana ni mbaya,ni kukosa utu,unfair na lack of moral values.
Mwisho niseme hivi, tatizo hili limekuwa sugu hasa kunapokuwa na sherehe za kitaifa,hii si mara ya kwanza.Mbona mishahara ya wafanyakazi inalipwa kwa wakati,hata kukiwa na sherehe za kitaifa,kwa nini isiwe hivyo kwa wastaafu?Hii ni dharau kwa wastaafu,ambao wamelitumikia taifa letu kwa muda mrefu,na jambo hili halipaswi kuwa entertained.Wafanyakazi wa hazina wanaowafanyia wastaafu uovu huu, wakumbuke kwamba ipo siku nao watastaafu.