Baada ya msiba mzito ulioikumba bendi ya FM academia baada ya kuondokewa na mpendwa wao marehemu Malou Stonch, mengi yameibuka.
Akizungumza kwenye chombo kimoja cha habari, kiongozi wa kundi hilo Patcho Mwamba amelalamika kwamba baadhi ya wanamuziki wacongoman wanazusha kwamba yeye ni mchawi na alimloga Malou stonchi.
Pia amelalamikia familia ya marehem, haswa mkewe ambae amekuwa akieneza habari kwamba mumewe alipoanguka, hakupatiwa huduma yoyote ya kwanza bali wanamuziki wenzake waliendelea kuimba na kutoa burudani jukwaani. Jambo hilo Patcho amelipinga vikali huku akisema kwamba mashabiki pia wasingekubali kuona burudani ikiendelea huku mwanamuziki akiwa chini taabani.
Hata hivyo, mashuhuda wa tukio hilo walisema kwamba, siku ya tukio marehemu alipoanguka chini alipatiwa huduma ya kwanza haraka iwezekanavyo na kisha kupelekwa hospital na kwamba Patcho hakuwepo jukwaani siku hiyo.
Patcho pia amemlalamikia mke wa marehemu ambae alienda ktk bar ya target kuulizia mumewe alifariki vipi na hata alipoambiwa ukweli hakuukubali, huku akisisitiza mumewe alianguka na wanamuziki hawakujali na waliendelea kutoa burudani.
Tuwaombee Patcho na familia ya marehemu wapatane Ili wafanye 40 ya marehemu salama