uzio usio onekana
JF-Expert Member
- Apr 21, 2019
- 776
- 2,404
Marehemu Nyaisuka Chacha Mohono.
Aliuawa na askari wa wanyamapori 11/03/2024 kwa kupigwa risasi saa nne asubuhi nyumbani kwao kitongoji cha Jerumani, Machochwe, Serengeti.
Askari walifika nyumbani na kutaka kupora ng’ombe ambao walidai kwamba waliingia katika hifadhi ya Serengeti (Serengeti National Park - SENAPA)
Nyaisuka Chacha Mohono akajaribu kuzuia ng’ombe wao wasitolewe zizini (wafugaji watanielewa), ndipo akapigwa risasi na kufariki papo hapo.
Askari wakaubeba Mwili wake na kuupakia katika gari yao na kuondoka nao hadi leo haujapatikana. Muhono alikuwa ni kijana mdogo sana wa miaka 21.
Chanzo: Chadema in Blood