Nmb bank house kielelezo cha uvivu na wavivu

Mi naona wateja ndio wamezidi capacity ya bank.
Not necessarily. Ni uvivu tu. Kingine Kinachowapa kichwa ni kwamba, serikali inapitishia huko mishahara ya watendaji wake na malipo mengine kama leseni za biashara na vyombo vya moto, kwa hiyo wana uhakika na customer base ya namna hiyo, mbali ya sisi ambao hatutegemei mishahara ya serikali. Ingekuwa hawana base hiyo nadhani wangetuhudumia vyema tu.
 
Teheh! Mleta mada alisema JUZI mkuu,jana hakuna benki zilifunguliwa....nadhani huwa hawafungui public holidays! Sijui jana umeipata wapi Rejao!
Ameedit...mwanzoni kaandika jana, naona kaona abadilishe! hata post yake inaonyesha kuwa ame edit!!
 
juzi katika mihangaiko yangu hapa jijini dar es salaam ilinifikisha katika bank nmb tawi la bank house makutana ya samora na mtaa wa pamba.

Nilipoingia ndani ya bank nikashangaa kukuta watu kama mia moja hivi wakiwa katika foleni zisizotembea, na nilipochunguza nikagundua kulikua na madirisha ya huduma zaidi ya 10, lakini yanayofanya kazi ni madirisha 2 tu......moja kwaajili ya cash deposit na mengine kwaajili ya cash withdraw .

Bahati mbaya zaidi kwenye chumba cha kuweka cha wateja wakubwa hakukuwa na mfanyakazi na taa ilikua imezimwa.

Nikamfuata meneja wao wa huduma kwa wateja kwakua nilikua na pesa nyingi za deposit na isingekua hekima kusimama nazo mda mrefu kwenye dirisha ambalo ni moja, na wakati huo kuna wateja wanasubiri, alinijibu kirahisi kuwa atafuatilia kujua nini kinaendelea.

Kwa udadisi wangu , nilichogundua hiyo benki inawatu wavivu , wasiojituma, wanaona raha kuona foleni ndefu .

Nampango wakuacha kuitumia hii bank , maana naona wafanyakazi wake hawajajua thamani ya muda na kwakua nmb si baba yangu acha niende kwa benki zingine.

nilikuwa na akaunti ya mtoto niliamua kuifunga kwa sababu ya kero zao.
 
Teheh! Mleta mada alisema JUZI mkuu,jana hakuna benki zilifunguliwa....nadhani huwa hawafungui public holidays! Sijui jana umeipata wapi Rejao!

Msamehe bure amepitiwa si unajua jana ilikuwa nusu weekend?
 
Jana kumbuka ilikuwa Mei Mosi, yaelekea ni wafanyakazi wachache tu ndio walikuwa kazini. Tusipende kulaumu kila kitu



AHH WAP KWA NMB acha kabsa ..sikukuuu si sababu
wazembe ,wanaringa wpao wapo tu yaan km mazuzu

last yr nilienda kufungua akaunt pale ahh bas nikajaza fomu yaan folen ata kumpa uyo c.care wao aangalie km ipo sawa bas yule baba akaangalia ile form afu akanambia ahh umesahahu kusain..afu akaichora chora kwa nyuma dah nilikasirika alivyoichafua form jaman ..nkapandwa na hasira na mimi nkamrushia nkamwambia wat if ungesema tu sain apa mbona kitui kdg sana sasa kuichafua fom ili nianze upya?maprocess mia?


na jinsi alivyokuwa anawajibu wale wadau wengne pale ahh yaan km mbwa....

pale makao makuu ni vbwengo kabsa yaaan...awajui kuelekeza watu mtu anamwelekeza kwa kumfokea mama muuza samak dahh mpk unataman kulia..mtu elimu yake darasa la pili yabidi aelekezwe lakin anavyokemewa utazan kafanya makusudi kutokujua procedures...WAMEKAA KUDINYANA TU WAO KWA WAO NA NGOMA ITAWACHUKUA PAMBAFUUUUUUUUUUUUUUU:bored:ebu nkale mie
 
Juzi katika mihangaiko yangu hapa jijini Dar es salaam ilinifikisha katika Bank NMB tawi la Bank House makutana ya Samora na Mtaa wa Pamba.

Nilipoingia ndani ya Bank nikashangaa kukuta watu kama mia moja hivi wakiwa katika foleni zisizotembea, na nilipochunguza nikagundua kulikua na madirisha ya huduma zaidi ya 10, lakini yanayofanya kazi ni madirisha 2 tu......moja kwaajili ya cash deposit na mengine kwaajili ya cash withdraw .

Bahati mbaya zaidi kwenye chumba cha Kuweka cha wateja wakubwa hakukuwa na Mfanyakazi na taa ilikua imezimwa.

Nikamfuata Meneja wao wa huduma kwa wateja kwakua nilikua na pesa nyingi za DEPOSIT na isingekua hekima kusimama nazo mda mrefu kwenye dirisha ambalo ni moja, na wakati huo kuna wateja wanasubiri, Alinijibu kirahisi kuwa atafuatilia kujua nini kinaendelea.

Kwa udadisi wangu , nilichogundua hiyo Benki inawatu wavivu , wasiojituma, wanaona raha kuona foleni ndefu .

Nampango wakuacha kuitumia hii Bank , maana naona wafanyakazi wake hawajajua thamani ya muda na kwakua NMB SI BABA YANGU ACHA NIENDE KWA BENKI ZINGINE.

Mimi niliiacha account yangu ikiwa na laki na ishirini, baada ya kuomba ruhusa kazini kwenda banki saa nne kuchukua hela ya ada ya watoto, nikakuta foleni nikakaa mpaka saa tisa, kufika kazini nikapewa warning letter. Mpaka leo nina kitambulisho chao , sijarudi hapo tangu 2004, naamini na hiyo hela ilikwisha isha.Lakini naona tatizo hili pia sasa linaanza kuwapo CRDB, Yaani wanaboa....:disapointed:
 
chakushangaza ni kuwa hawastuki wala hawastuliwi na idadi ya wateja katika foleni isiyotembea , wanafanya kazi kijamaa


Nafikiri ulikuwa unataka Kusema Wanafanya Kazi Kijima,ha ha ha,sasa hapo uliza Cv za Mamanager,utaona Uzoefu Miaka 10,sasa sijui uzoefu huo umeleta tija gani,aah Booooooongo!!
 
Kiukwel hata kama wateja ni weng kuonekane kuna juhud za kupunguza folen. Mi ilinikuta nikauliza nkaambiwa wako meeting mara kama 3 hv.Nikahoj ina maana hawajali wateja kwa kuweka vikao muda wa kaz hasa kwa telers! Uhalisia,Nmb wana upungufu wa workers.Sijawah kukuta madirisha yote yanafanya kaz tokea nianze ku2mia benk hii. CRDB wanajitahid sana hasa kujipanua,nikiwa dar napenda ku2mia taw la premier la mkapa tower no folen at all cjui wa2 hawajajua kwamba ndan kuna benk.Weng wanadhan ni atm's 2.


Hata mm nilikuwa sijui kama pale kuna tawi,nilijua ni Atms tu,senx for info mkuu!!
 
nilishawahi kwenda na wife yeye ana akaunti nmb kuweka pesa mingi kidogo hapo hapo eti teller mwanamke ananiuliza pesa zote hizi mmezitoa wapi? Aisee sijazoea kuulizwa kitu km hiyo kwenye ma benki binafsi temper ikanipanda lkn wife kawazoea akanituliza. Yaani huwa hawana haraka kabsaa na wanawaona wateja km usumbufu flani
 
NMB ni kero kwa kwenda mbele. Wanafikiri bado wapo wenyewe "monopoly".
 
Hata wasipoingiza faida wanalipwa, haina hasara, be ashamed of ur services plz
 
Hata wasipoingiza faida wanalipwa, haina hasara, be ashamed of ur services plz

na nimeambiwa leo kuwa NMB wanapokea zaidi ya Billion 3, Tsh. kama malipo ya kuhamisha fedha za serikali kupeleka vituoni . kwakua wanapokea pesa nyingi hivi kwa mwaka , zinawaongezea faida inayowapa kiburi.
 
TaiJike Kumbuka lakin NMB ndio bank yenye wateja wengi, vile vile ni bank yenye matawi mengi nchini. Mi naona wateja ndio wamezidi capacity ya bank.
Sasa kama wateja wengiwanashindwa kuwahudumia kwa nini wasisitishe kuandikisha wateja wapya au kuongeza resources (human or otherwise) ili kuwahudumia wateja kwa namna bora zaidi?
 
Back
Top Bottom