Paul Makonda Special Thread: Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Paul Makonda; Make Arusha Great Again

Nilijua kuwa Makonda kwa staili na hulka yake hasingeweza kubaki kwenye nafasi ya Katibu mwenezi wa CCM kwa muda mrefu na imetokea.

Pia Makonda kubaki RC wa Arusha ni suala la muda tu.

Makonda ameshawekwa kati na kamati ya maadili ya CCM na hiyo ni dadili mbaya kwake.

Cha msingi zaidi ni washauri wa kisiasa wa rais Samia ambao ni dhahiri hawamshauri vizuri katika mambo mengi.

Sasa hivi Makonda atabaki madarakani kwa kitambo kidogo kuondokana na aibu ya teua tangua lakini mwishoni ataachwa mazima. Tusubiri muda ufike.
MAKONDA ni maji ya kunywa, usipoyanywa madhara yake ni makubwa kikiwemo na kifo, hivyo endelea kumtaja ili usife
 
Kwenda mbali wapi unapotaka afike ?!!!!

Kwa alipofika sasa hata akifa kesho alichofanya sio kidogo kutokana na alipota (unaweza kusema ni against the odds)

School Failure, a boy from the village kutokukata tamaa na kujishusha na kupata connection za watu tofauti bila kutumia surname.... (Sio wote wanaweza hilo)

Kwahio all in all ukizingatia politics ni ulaghai, uongo na unafiki - nachoweza kusema the guy has done pretty well all things considered..., ndio maana wewe hapa umemuweka yeye (an individual) kama (issue).
 
Huyo jamaa, hata Marekani wamempiga marufuku kuingia nchini mwao, Kwa kuwa WANAZO taarifa za kiintelejensia kuwa anawanyima wananchi wake haki yao ya kuishi!
Nasahihisha kidogo: Anawanyang'anya haki ya kuishi. Anayetoa haki hiyo ni Mungu tu wengine kama DAB wanachofanya ni unyang'anyi wa haki hiyo.
 
Akitolewa pale anaenda Bungeni au nafasi za Rais zimeisha. ?!
Kama zimeisha anapelekwa Ubalozi 😅😂🙏 !
Kumtupa kabisa haiwezekani maana Abracadabra nyingi anazijua kwahiyo ni lazima ahofiwe asije akamwaga mboga ! 😅😅 !

LLakini ngoja tusubiri tuone na hizi speculations zinazoendelea !

Makonda Bomayee !!
 
Makonda vs Chawas again.
Ukiona hivi, kuna mjadala wanataka kuufunika.
iu
 
Makonda hana tofauti na hao anaowataja ndiyo maana wenzake wanambadilikia kwa kujiona yeye ni msafi
 
Sifa kubwa ya mwanasiasa ni kuwa na uwezo wa kutunga na kubuni sera nzuri bila kusahau kuwa na ushawishi au umaarufu kwa watu, sera nzuri peke yake haitoshi.

Si mtazami makonda kama mwanasiasa bali namtazama kama mwanasaikolojia wa siasa na kijana anayetafuta ridhiki ili ajikimu kimaisha, Licha ya kutokea ktk familia masikini na skendo alizopitia huyu mwamba ila bado anapambana na hakauki midomoni mwa watu kwa kuja na style ndogo ndogo ambazo wengi huziona za kijinga ila ndizo zinazompa umaarufu na kumfanya apate trend
GridArt_20240426_105535359.jpg


Mwaka 2015 wakati Raisi Magufuli kachukua nchi alitamka kuwa ktk orodha yake ya wakuu wa mikoa itakayotoka mtu pekee ambaye tayari ananafasi kwenye mkeka ni Paul Makonda.

Huyu ndiye mwamba pekee anaeweza kumuweka raisi yeyote close akawa kama mshikaji wake licha ya kuwa na cheo kidogo. Wengi mtachukulia poa lakini ni kazi ngumu sana.

Huyu ndiye mtu pekee Tanzania mwenye uwezo wa kiutrend mwaka mzima.

Yeye siku zote huanzisha trend na ni mjanja mjanja sana anawazidi wanasiasa wengi sana hapo CCM

Mnaikumbuka kauli yake ya juzi kwa raisi samia kuhusu mawaziri wanaolipa watu wamchafue taisi mtandaoni kuwa anawajua na ayawatataja na kuwaonya waache! Ile ni mbinu ya kivita ya kumuweka close mama, wazungu wanasema The enemy of your enemy is your friend

wanasiasa wasaka fursa mnachakujifunza kwa Makonda yule ni mwanasaikolojia wa siasa hawezi kulala njaa mjini.
 
Back
Top Bottom