NetMaster
JF-Expert Member
- Sep 12, 2022
- 1,454
- 4,860
Nilienda kwenye mualiko wa sherehe ya rafiki yangu kuna dada yake alikuwa anaolewa, nikiwa najimwagia moyo na bia kadhaa ukafika muda wa kwenda kusakata rumba, mzuka niliokuwa nao ulikuwa fire 🔥💥 bum shakarakah! 💥🔥Nikajivuta hadi sehemu ya tukio na nikaanza manjonjo yangu kujiachia kwa 'confidence' kama yote. Uchezaji wangu uliibua shangwe kwa namna ya kipekee nilivyolisakata.
Nimerudi kwangu najua tayari yashapita hayo, sasa naja kushangaa kuna MC wa tukio nimeambiwa kanipost kwenye kurasa yake ya Insta, nimeingia huko na kweli nimejiona! Najiuliza kulikuwa na umuhimu gani kunipost huko bila ridhaa yangu muhusika?
Hata bar, club ama pub watu huwezi kuwakuta wanapostiana hovyo hovyo wakiwa wanafurahia starehe zao, iweje hawa ma MC wanatupost hovyo hovyo?
Nimerudi kwangu najua tayari yashapita hayo, sasa naja kushangaa kuna MC wa tukio nimeambiwa kanipost kwenye kurasa yake ya Insta, nimeingia huko na kweli nimejiona! Najiuliza kulikuwa na umuhimu gani kunipost huko bila ridhaa yangu muhusika?
Hata bar, club ama pub watu huwezi kuwakuta wanapostiana hovyo hovyo wakiwa wanafurahia starehe zao, iweje hawa ma MC wanatupost hovyo hovyo?