Suhendra
JF-Expert Member
- Nov 25, 2023
- 1,196
- 2,669
Kwa mwislam anae jiekewa wala hawezi kula hata ukimkaribishaKuheshimu imani ya mtu, hasa katika nchi isiyo na dini, ni suala nyeti sana. Ndiyo maana Watanzania wengi wanapotaka kufanya sherehe, kama si Waislamu, huhakikisha kuwa mchinjaji wa nyama itakayotumika ni Muislamu.
Lakini itakuwaje ikiwa wewe si Muislamu na ukatembelewa ghafla na rafiki Muislamu wakati unamla kuku uliyemchinja mwenyewe?
1. Utamkaribisha kujumuika nawe pamoja na kuwa unajua ulichinja bila kuzingatia imani ya Kiislamu?
2. Utamjulisha ukweli kuwa ulimchinja wewe mwenyewe ili aamue mwenyewe?
3. Utamwambia asubirie umwandalie cha kwake?
Upi utakuwa uamuzi wa busara?