Utakuwa humjui Anthony Mtaka, hawezi kupata muda wa kujibu vitu vidogo hivi!. Kwa tunaomjua Mtaka, tunajua Mtaka hawezi kumtukana mtu yeyote!.
Kwa kifupi, mtu kama huyu
View: https://youtu.be/Ed7c9aEw8-Y?si=RcVTCoB_eom6d54C ataanzia wapi kumtukana mtu?.
View: https://youtu.be/bKobi1sGjQ4?si=0Qh3vJg7hWbFQdqv
View: https://youtu.be/sOv_cJSC9As?si=_QRpMw_Rp1rh8C5h
View: https://youtu.be/-f10kAUh7ik?si=h-eJ70koa8_PUcQ9
P
Sawa japo ukumbuke ya kuwa mlalamikaji anatakiwa kuwa na ushahidi usioacha shaka ya aina yoyote ile. Mahakama haipokei ushahidi wa maneno tupu bila ushahidi wenye mashiko.Ndg lukasi
Tayari unaandaliwa utaratibu murwaaa wakumtimbisha mtaka kotini , tusubirie
Jifunze kuwa na ustaarabu unapojibu hoja au kujadili hoja.Kwanini tu usiendelee kulamba Makalio ya Mtaka nini kimekusibu?Bahasha zimekata?!
Chawa wa Mama tokea lini ukawa na Hoja zenye mashiko?!Jifunze kuwa na ustaarabu unapojibu hoja au kujadili hoja.
Sawa nashukuru sana.Chawa wa Mama tokea lini ukawa na Hoja zenye mashiko?!
Thank you very much indeed😃😃😃Amani ya Bwana iwe pamoja nawe
Ole wake nife nieende jehanam nimkute ntqfira vibaya sanaNa rungu limeshawashukia ndiyo maana leo hii yule mwovu mkuu kuwahi kutokea katika ardhi ya Tanzania yuko Jehannam anapokea kibano kwa uovu wake uliokithiri
Lucas mbona unamkaanga Mtaka mwana ccm mwenzako? Mtakatana mapanga safari hiiNdugu zangu Watanzania,
Nimeendelea kuisikiliza video ya muuguzi aliyedai kuwa ni miongoni mwa wauguzi waliompokea Lissu hospitalini siku alipokimbiziwa hapo baada ya kushambuliwa kwa Risasi na watu wasiojulikana 2017.
Ambapo katika mazungumzo hayo na Lissu muuguzi huyo ambaye anadai alishafukuzwa kazi kwa madai ya utoro kazini .anasema kuwa siku ya sheria Dunia mwaka 2022 aliingilia hotuba ya Mheshimiwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hasssan ili aweze kusikilizwa .ambapo hata hivyo muuguzi huyo anadai ya kuwa Rais aliamuru aende kwa wasaidizi wake ili wamchukue maelezo na wao watayawasilisha kwake.
Ambapo baada ya kuwa amekaa kwenye gari pale chini kwa ajili ya kusikilizwa ,anadai kuwa aliitwa mkuu wa mkoa wa Dodoma wa wakati huo Mheshimiwa Antony Mtaka ambaye kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa Njombe,ambapo muuguzi huyo anadai ya kuwa baada ya Mheshimiwa Mtaka kuja alimtukana kwa kumwambia FALA WEWE. Ambapo muuguzi huyo anasema akasema yeye siyo fala na kwamba amefanya hivyo kwa kuwa amekuwa hasikilizwi. Anasema akamwambia Mheshimiwa Mtaka kuwa hata wewe utaondoka hapa yaani Dodoma.
Ameendelea kueleza kuwa alitoa maelezo kwa wasaidizi wa Mheshimiwa Rais ambapo anaamini pengine ni katika maelezo yake yale ndio maana Mheshimiwa Mtaka alipewa kama adhabu kwa kupelekwa mkoani Njombe. Ameendelea kusema kuwa Mheshimiwa Mtaka alimuweka central police kwa Amri kwa siku tatu wakati alikuwa anaumwa na kwa muda wote huo hakupewa dawa wala maji na kuendelea kupata maumivu makali sana Mwilini mwake yaliyotokana na kukosa dawa alizokuwa anazitumia kwa wakati huo.
Hoja yangu mimi ni kuwa hoja na tuhuma hii ni nzito sana ,kwa kuwa Mheshimiwa Mtaka amejijengea heshima kubwa sana hapa nchini juu ya utendaji wake ambao umejengwa katika taswira ya uchapa kazi.ambapo amekuwa akipongezwa na kusifiwa na viongozi wengi sana pamoja na wananchi mbalimbali nikiwepo mimi mwenyewe Mwashambwa Lucas mwanachama na kada kindaki ndaki wa CCM.
Kwa sababu inamchafua sana Mh Mtaka hasa kwa namna jina lake lilivyo kubwa miongoni mwa wakuu wa mikoa waliopo hapa nchini. Maana hata leo ukimwambia mtu akutajie wakuu wa mikoa walau watatu tu wachapa kazi ,basi jina la Mh Mtaka lazima litakuwepo. Sasa siamini kama Mheshimiwa Mtaka anaweza kuacha na kushindwa kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kwenda kumsikiliza mwananchi mwenye shida ili apatiwe majibu , na badala yake Mh Mtaka aende kumtukana huyo mwananchi kuwa ni FALA. Jambo ambalo naamini si sahihi kwa sababu hata fala anayo nafasi ya kusikilizwa katika ufala wake. Maana katika ufala wake kunaweza kukawa na maumivu katikati yake yanayohitaji msaada.
Najuwa kuwa kiongozi huwezi ukajibu kila kitu kinachotokea na kuendelea mitandaoni,najuwa siyo kila jambo linaloibuliwa mitandaoni linaweza kuwa la kweli. Lakini katika hili jambo zito la tuhuma tena ambalo lilitolewa maagizo na Mheshimiwa Rais natamani Mheshimiwa Mtaka angelitolea hata majibu kidogo tu hata kupitia mtandao wake wa kijamii kama vile kupitia twitter au njia yoyote ile. japo tamaa yangu siyo lazima kutimizwa au kupata majibu au kujibiwa.maana inategemea na mhusika atakavyojisikia na kulichukulia jambo hili. Maana hata kukaa kimya nako ni jibu na ni haki ya mtu na sehemu ya mbinu za kiuongozi na kuwa kama kiongozi siyo lazima uzungumze kila kitu na kutolea ufafanuzi kwa kila kitu.
Lakini pia suala la kupelekwa Njombe ningependa kusema kuwa ni jambo la kawaida katika utumishi wa umma au uongozi.maana hata Njombe ni sehemu ya Tanzania na ina watanzania wanaohitaji viongozi bora na wachapa kazi ili kuinua mkoa huo. na siyo kwamba ni mkoa wa kutumikia adhabu kwa wenye makosa na wala siyo Magereza ya viongozi waliotenda makosa sehemu nyingine za utumishi wao.. Kwa hiyo hoja ya kupelekwa Njombe siichukulii kama hoja ya msingi au adhabu bali naichukulia kama mabadiliko ya kawaida tu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Umeacha kumshukutu Samia kwa kila jambo?Sawa nashukuru sana.
haha sahihi kabisa hata bashite analijua hilo.CCM hatujawahi kuunga mkono Vitendo vinavyokiuka na kuvunja haki za binadamu. CCM na wana CCM tunapenda haki nakutaka kuona kila mtanzania akitendewa haki. Ndio maana hata mwenyekiti wetu na Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mama Samia ameendelea kusisitiza na kuvisihi vyombo vya dola kama vile jeshi la polisi kutenda haki kwa watu.
Hapana ndugu yangu wala simkaangi bali nina mashaka na ukweli wa tuhuma zilizoelekezwa kwake na yule Nesi.ndio maana nikatamani kama angeweza kutoa neno la kukanusha au kuelezea juu ya tuhuma zile.Lucas mbona unamkaanga Mtaka mwana ccm mwenzako? Mtakatana mapanga safari hii
Kesi kisa kuitwa fala au kufukuzwa kazi au kutolipwa mafao ama ni kipi hasa?Anasema kwa sasa anahitaji msaada wa kisheria ili aweze kufungua kesi mahakamani.ambapo amemuomba Lissu amsaidie kufungua kesi mahakamani.
Anasema Anahitaji msaada wa kisheria kuhusiana na kufukuzwa kwake kazi kwa kosa la utoro.wakati yeye anadai kuwa alikuwa ni mgonjwa na anayobarua ya madaktari kutoka muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu.Kesi kisa kuitwa fala au kufukuzwa kazi au kutolipwa mafao ama ni kipi hasa?
BTW: Hizo lugha kwa hawa miungu watu ni kawaida sana sitoshangaa ikiwa ni tuhuma ya kweli.
Mtaka is overrated,kuna takwimu zozote za huo uchapakazi kuanzia Simiyu hadi huko alipo sasa?
Uwe na adabu kwa Mheshimiwa Rais wetu.sihitaji hata kukujibu kwa kuwa umekosa adabu kabisa kwa Rais. Rais wa nchi usifananishe na mtu wa kawaida.kwanini usingeuliza kwa lugha ya staha na adabu ili uweze kujibiwa kuliko kuandika kwakutumia lugha chafu,ya kejeli na dharau?Nikisema hapa kizimkazi hana muda na watanganyika ona alishindwa nn yy kumckiliza? Tena ni mwanamke mwenzie!! Huyu kizimkazi hakuna anacho weza zaidi y kuteua na kutengua TU. Watanganyika tujipange sana kuhusu kizimkazi.
Na bado hata sikilizwa kwa uongozi w kizimkazi ila ingekua kwenda nje kuombaomba misaada yuko vzr au kuuza mali za watanganyika Yuko POA MNO.
KAZI ni kipimo cha UTU
Rais ambaye aliwalaumu walengaji kupiga risasi 16 bila kuua?Raisi angemwambia tu huyo mkuu wa mkoa aende nyumbani akapumzike.
Utakuwa humjui Anthony Mtaka, hawezi kupata muda wa kujibu vitu vidogo hivi!. Kwa tunaomjua Mtaka, tunajua Mtaka hawezi kumtukana mtu yeyote!.
Kwa kifupi, mtu kama huyu
View: https://youtu.be/Ed7c9aEw8-Y?si=RcVTCoB_eom6d54C ataanzia wapi kumtukana mtu?.
View: https://youtu.be/bKobi1sGjQ4?si=0Qh3vJg7hWbFQdqv
View: https://youtu.be/sOv_cJSC9As?si=_QRpMw_Rp1rh8C5h
View: https://youtu.be/-f10kAUh7ik?si=h-eJ70koa8_PUcQ9
P
Ni kweli uongo ukisemwa sana, na kuachwa ukarudiwa rudiwa, hugeuka ukweli, lakini sio uongo wa kijinga!. Dawa ya uongo wa kijinga ni kuupuuzia tuu, utajifia wenyewe!. Mfano shetani kakupitia, ukapita na dada zetu wale wa ile biashara, kisha akataka pesa zaidi na wawe huna, akaamua kukuchafua kwa kusema hujafanyiwa sunna!, vipi wewe ili kukanusha, utafungua zipu kuonyesha kuwa sii kweli?. Vitu vingine vya kujinga mno ni vya kupuuzwa tuu!.Nimezungumza hayo kwa kuwa najuwa ya kuwa uongo ukizunguka sana na kuenea pasipo kupata majibu unageuzwa kama ndio ukweli wenyewe hasa kwa watu wasiopenda kuangalia mambo kwa jicho la tatu. Nafikiri hata wewe mwenyewe Mheshimiwa Mayalla umekuwa ukizungumza juu ya jambo hilo katika baadhi ya makala zako.