beatboi
JF-Expert Member
- Mar 29, 2021
- 457
- 1,125
Habari zenu watoto wa mama (SSH)
Nimejikuta wiki nzima imeharibika baada ya kupokea matusi kutoka kwa mtu ambaye amejitambulisha ni mtoa huduma kwa wateja (customer care).
Nilikuwa nimepumzika zangu majira ya asubuhi ghafla nikapokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa anatoka kitengo cha halopesa hivyo akaomba nimtajie kiasi cha pesa kilichomo kwenye account yangu sababu kuna mtu amekosea bahati mbaya ikaingia kwangu.
Nilimtajia kiasi kilichopo tena akasisitiza hadi visenti vyote kisha akakata simu. baada ya hapo ikaingia sms ya kupokea huo muamala, nilivyomaliza kusoma tu jamaa akanipigia akawa ananipa maelekezo jinsi ya kurudisha hiyo pesa ya watu.
cc: unatumia simu gani?
Mimi: Samsung j2
cc: OK rudi hadi sehemu ya kupiga hapo mwanzo
Mimi: tayari.
Kuna namba akawa ananitajia niandike ila kutokana na maeneo niliopo mtandao ukawa unasumbua, sasa nikamwambia hpa nilipo mtandao unasumbua kidogo! dah nikawa nimefungua mvua ya matusi coz yule jamaa alimtukana mama yangu, mimi mwenyew na ukoo mzima na kunikatia simu kwa ghadhabu. nimefikilia nikaona kabla sijafungua kesi niwashirikishe ndugu zangu wanajfm kwa ushauri maoni nk.
Nimeambatanisha na ushahidi wa picha namba zake
Nimejikuta wiki nzima imeharibika baada ya kupokea matusi kutoka kwa mtu ambaye amejitambulisha ni mtoa huduma kwa wateja (customer care).
Nilikuwa nimepumzika zangu majira ya asubuhi ghafla nikapokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa anatoka kitengo cha halopesa hivyo akaomba nimtajie kiasi cha pesa kilichomo kwenye account yangu sababu kuna mtu amekosea bahati mbaya ikaingia kwangu.
Nilimtajia kiasi kilichopo tena akasisitiza hadi visenti vyote kisha akakata simu. baada ya hapo ikaingia sms ya kupokea huo muamala, nilivyomaliza kusoma tu jamaa akanipigia akawa ananipa maelekezo jinsi ya kurudisha hiyo pesa ya watu.
cc: unatumia simu gani?
Mimi: Samsung j2
cc: OK rudi hadi sehemu ya kupiga hapo mwanzo
Mimi: tayari.
Kuna namba akawa ananitajia niandike ila kutokana na maeneo niliopo mtandao ukawa unasumbua, sasa nikamwambia hpa nilipo mtandao unasumbua kidogo! dah nikawa nimefungua mvua ya matusi coz yule jamaa alimtukana mama yangu, mimi mwenyew na ukoo mzima na kunikatia simu kwa ghadhabu. nimefikilia nikaona kabla sijafungua kesi niwashirikishe ndugu zangu wanajfm kwa ushauri maoni nk.
Nimeambatanisha na ushahidi wa picha namba zake