#COVID19 Napambana na COVID-19 deadly Delta

isajorsergio

Platinum Member
Apr 22, 2018
4,125
6,253
Habari 👋🏾

Kumekuwa na hali ya watu wengi kupuuza na kutokuchukua tahadhari ya ugonjwa wa UVIKO na wengine wakienda mbali kudai hakuna ugonjwa kama huo. Napenda kuwaambia COVID-19 deadly Delta yupo Tanzania na kila mahali, nimepatwa na ugonjwa ilhali nipo eneo lilotengwa na pembezoni katika nchi.

Toka juzi jioni najihisi vibaya, napumua kwa shida, nimebwana kifua, mafua na kikohozi. Uwezo wa kusikia na kuona umepungua sana, nahisi maumivu katika mifupa na maungio ya mwili. Homa na koo kukabwa, kuwashwa, kuhisi damu ya baridi, jaws (tezi) kuwa na maumivu makali na ngozi kuakisi rangi ya bluu na kizunguzungu ni hali ninazopambana nazo.

Namna nahisi afya yangu kwa sasa, niseme nisengelikuwa mtu wa mazoezi parapanda ingekwisha imbwa. Sio kwamba sikuchukua tahadhari lah! Nimekuwa nikizingatia taratibu zote toka mlipuko huu kutokea Wuhan lakini nimekwamishwa na jamii ya watu walionizunguka.

Nimeorodhesha dalili na hali kuweza kusaidia mamlaka na watu kufahamu hali ilivyo. Hali ikiendelea hivi itatuchukua miaka 10 kupambana na COVID-19 ikiwa tumezungukwa na watu wenye mentality za hovyo na wasiojali wala kuchukua tahadhari.

Sergio 🐰
 
Kwamba?

"....... niseme nisengelikuwa mtu wa mazoezi parapanda ingekwisha imbwa. Sio kwamba sikuchukua ...."

pole sana mkuu.

Ndiyo mazingira ya nchi tuliyopewa bila kuyasahau mamburula yote.

Mola akakusimamie upone haraka ukaendelee na shughuli zako.
 
Kwanza pole sana. Kupata hio ugonjwa haimaanishi kifo.

Kwamba uko hai hadi sasa kwa sababu ni mtu wa mazoezi?
 
Kwanza pole sana. Kupata hio ugonjwa haimaanishi kifo.

Kwamba uko hai hadi sasa kwa sababu ni mtu wa mazoezi?
Asante

Naamini kuumwa sio kifo lakini kwa hali ninayohisi na mfumo wa upumuaji kwa mtu ambaye hafanyi mazoezi au kuusumbua mwili kufungua mifumo ya hewa na upumuaji Delta anaondoka naye.
 
Awamu ya pili nilikumbana na huu ugonjwa, kiukweli ugonjwa huu unatesa sana mgonjwa, ni gharama hata kama una hela, kwa asie na hela hali yake ni ngumu sana. Nilisumbuka sana kipambania afya kipindi kile japo nilikuwa na chukuwa tahadhari sana ila watu wanaonizunguka wanaenda sehemu kama Kariakoo, bar, makanisani na mbaya zaidi wengi hawachukui tahadhari.

Serikali inatakiwa kuchukuwa hatua kali sana bila kuoneana huruma maana huu ugonjwa ukiingia kwenye familia ni janga kubwa sana. Kwa ambaye alishapata huu ugonjwa au ambaye kwenye familia yake kumeahapatikana mgonjwa ndio atakuwa anajua jinsi huu ugonjwa unavyotumia gharama kubwa kupambana nao.
 
Ikiwafikia hawa ndio watapata akili za kuongeza na kuboresha huduma za afya na kutenga fungu la kuondoa ujinga kwa taifa.
kwani haijawafikia tayari?? mbona viongozi kina Kijazi waliondoka nayo?? basi tu hatuna waziri wa afya makini..alikua anahimiza nyungu..sasa hivi Rais yuko makini ndio kaanza kuhuburi watu wachukue tahadhari...matokeo yake watu wanapuuza guidelines...chanjo inaonekana kama sijui duddu gani
 
Pole sana mkuu! Inahuzunisha sana tuchukueni tahadhari jamani 😪
zamani kufiwa ilikuwa unakaa hata miaka 5 anaondoka member 1paap!!mnatulia tena ht miaka7 ndo afatie mwingine!!

ndani ya mwezi unafiwa na members 2 halafu walikuwa wazima wa afya!bado roho iko juu juu mwezi unafuatia wengine 2 paap!

hapo mwingine akiumwa kwa mtindo ule ni mashaka yaani unakuwa moyo unakulipuka kila mda huna raha.
 
daahh rangi ya bluu ni kwamba oxgen level ilikuwa chini sana.
huu ugonjwa toka mwaka umeanza umeshaondoka na 4 family members akiwemo mamaangu!!
na hapa sshv naongea mwingine amelazwa na ventilator juu...
acheni maskhara kbs.
Nikiwambia watu hawaelewi wanadhani masikhara! Tatizo sio wapumbavu kufa tatizo wanasambaza na kuua wasio na hatia.

Huwezi kuamini eneo linalodaiwa kuwa na level au uwiano mzuri wa elimu Bukoba Municipal kwa utafiti niliofanya ni katika watu 300 ni watu 4 tu wanaovaa barakoa na watu 11 wanaonawa mikono.

Katika watu 100 ni watu wawili tu wanaonekana kuchukua tahadhari, sio benki, sokoni, nyumba za dini hata makazi ya watu. Usambazaji unafanywa na wanawake wakifuatiwa na watoto.
 
Back
Top Bottom