mgt software
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 13,767
- 7,117
Wana JF.
Si kwa nia mbaya maana waturuki wametoa ajira lakini kuna haya.
Waturuki wamekuwa wakizunguka mitaani na bajaji wakikopesha vyombo mbali mbali. Msala wangu kwao ni kwamba, nani ametoa kibali cha ukaguzi wa vyombo vyao vya umeme?
Kama kuna mtu wa TBS na FCC inabidi kwa pamoja kuchunguza vifaa vinavyosambazwa na waturuki wanaofanya kazi zao kama wamachinga. Waturuki wana bajaji nyingi zinazunguka mjini nyumba kwa nyumba wakikopesha vifaa mbali mbali vya umeme.
Hasa Rice Cooker na Multicooker. Vifaa vingi vinavyotumia moto, hasa wakati wa kupika vimekuwa nyaya za machine zinapata moto kiasi cha kuyeyuka na kusababisha hatari ya kuunguza nyumba. Ni kweli Tanzania ni dampo kuu la vifaa vilivyoigiziwa na kufanywa original , lakini vingi vinaingizwa kwa njia ya panya.
Hipo haja ya kupita nyumba kwa nyumba na kukagua vifaa vya umeme vya majumbani. Hapa tutaepusha nyumba kuwa zinaungua hovyo na kusababisha uharibifu mkubwa wa vitu. Kama FCC na TBS wasipochunguza vifaa vya umeme vinavyoingizwa nchini. Basi tutegemee nyumba nyingi kuungua.
Si kwa nia mbaya maana waturuki wametoa ajira lakini kuna haya.
Waturuki wamekuwa wakizunguka mitaani na bajaji wakikopesha vyombo mbali mbali. Msala wangu kwao ni kwamba, nani ametoa kibali cha ukaguzi wa vyombo vyao vya umeme?
Kama kuna mtu wa TBS na FCC inabidi kwa pamoja kuchunguza vifaa vinavyosambazwa na waturuki wanaofanya kazi zao kama wamachinga. Waturuki wana bajaji nyingi zinazunguka mjini nyumba kwa nyumba wakikopesha vifaa mbali mbali vya umeme.
Hasa Rice Cooker na Multicooker. Vifaa vingi vinavyotumia moto, hasa wakati wa kupika vimekuwa nyaya za machine zinapata moto kiasi cha kuyeyuka na kusababisha hatari ya kuunguza nyumba. Ni kweli Tanzania ni dampo kuu la vifaa vilivyoigiziwa na kufanywa original , lakini vingi vinaingizwa kwa njia ya panya.
Hipo haja ya kupita nyumba kwa nyumba na kukagua vifaa vya umeme vya majumbani. Hapa tutaepusha nyumba kuwa zinaungua hovyo na kusababisha uharibifu mkubwa wa vitu. Kama FCC na TBS wasipochunguza vifaa vya umeme vinavyoingizwa nchini. Basi tutegemee nyumba nyingi kuungua.