Msaada wa namna ya kuendesha biashara ya mgahawa ambao ni Classic, ingawa siyo sana

Bwanamaya

Member
Mar 14, 2017
72
93
Wapendwa kama ambavyo nimeandika hapo, naomba msaada wa kitaalamu jinsi ya kuendesha biashara hii.

Sijafungua ila nimesha fanya maandalizi ya chumba pamoja na vifaa baadhi, ishu kubwa itakuwa kwenye ku-manage pesa na wafanyakazi nk.
 
Sina ujuzi sana ila acha nijaribu. Mtu wa kumanage fedha anatakiwa awe mwaminifu na ni nzuri ukamuweka mke ama ndugu wa karibu. Sometimes wanaweza wasiwe watu bora, basi vyema ukamuweka mtu mzima kidogo maana vijana bado wanatafuta maisha. Asije akanyanyuka na wewe huku wewe mwenyewe unataka kunyanyuka.

Upate m/wapishi wazuri. Vyombo vyako viwe vizuri. Mazingira yawe safi so ununue dawa za kufanyia usafi kuepusha wadudu mbalimbali. (Kuna sehemu nilishawahi kwenda kula Mwenge, mende walikua wanatoka chini ya meza). Sali upate wahudumu wazuri kuanzia muonekano mpaka kauli hasa kauli. Mhudumu akiwa na hekima utapata raha sana. Na pia kuwe na daftari maalum la kuonyesha mauzo yanayotoka na bei ili kila siku ufunge na kufungua hesabu. Hii itakusaidia kuona wapi panahitaji umakini na adjustments za kufanya.

Mwisho kwa sabbu ndo unaanza kama vipi jitahidi sana uwepo kila siku atleast kwa miezi 3 ya mwanzo ili uone mambo yataendaje katika hiyo biashara. Chanzo cha pesa chochote kinalelewa kama mtoto. Umakini na Uthabiti plus juhudi vinahitajika mno.

NB: Natafuta kazi.
 
Migahawa inalipa sana,kazi ngumu ni kubalance chakula na wale wasaidizi wako wasikuibie hela na wasisahau kuchukua hela kwa wateja maana kuna wakati huwa naona wanabug hesabu

Mfano wahudum wengi wameshazoea ukiagiza chai na chapati wanajua chapati zilikuwa mbili hata kama uliagiza tatu
 
Sina ujuzi sana ila acha nijaribu. Mtu wa kumanage fedha anatakiwa awe mwaminifu na ni nzuri ukamuweka mke ama ndugu wa karibu. Sometimes wanaweza wasiwe watu bora, basi vyema ukamuweka mtu mzima kidogo maana vijana bado wanatafuta maisha. Asije akanyanyuka na wewe huku wewe mwenyewe unataka kunyanyuka.

Upate m/wapishi wazuri. Vyombo vyako viwe vizuri. Mazingira yawe safi so ununue dawa za kufanyia usafi kuepusha wadudu mbalimbali. (Kuna sehemu nilishawahi kwenda kula Mwenge, mende walikua wanatoka chini ya meza). Sali upate wahudumu wazuri kuanzia muonekano mpaka kauli hasa kauli. Mhudumu akiwa na hekima utapata raha sana. Na pia kuwe na daftari maalum la kuonyesha mauzo yanayotoka na bei ili kila siku ufunge na kufungua hesabu. Hii itakusaidia kuona wapi panahitaji umakini na adjustments za kufanya.

Mwisho kwa sabbu ndo unaanza kama vipi jitahidi sana uwepo kila siku atleast kwa miezi 3 ya mwanzo ili uone mambo yataendaje katika hiyo biashara. Chanzo cha pesa chochote kinalelewa kama mtoto. Umakini na Uthabiti plus juhudi vinahitajika mno.

NB: Natafuta kazi.
Nashukuru sana kwa ushauri mzuri nimekuelewa vyema...sema hapo mwisho sasa
 
Migahawa classic bongo hailipi,watu wanapenda sehemu kocal za kawaida ndio utapata wateja,ukizidisha mbwembwe wanakimbia ,zingatia sana huu ushauri
Barikiwa sana mkuu, hili nalo linafikilisha sana nashukuru
 
Kama una mtaji, location ya biashara yako ndio factor nyingine kwakuwa huyo itaonyesha kuwa umelenga ku capture wateja wa aina gani na kama utawapata.

Sio unaenda kufungua hiyo classic restaurant uswahili wakati watu wa huko menu yao ni utumbo na speed/reki za kuku.
Sahihi mkuu nashukuru
 
Biashara ya mgahawa inahitaji umakini sana wa mtunza fedha, hakikisha unamuweka mtu wako wa karibu sana au ndugu kama inawezekana
 
Habari mkuu,
Hongera kwa wazo Bomba kabisa
Wazo Hilo ni mojawapo Kati ya mawazo yangu


Fanya hivi broo,
1, tafuta wafanyakazi wenye Nia ya kufanya kazi, dispiline, na wanaojali kazi
Tengeneza menu Pana (vyakula vya Bei RAHISI na vya Bei ghali pia)
Kuwa tofauti na washindani wako kw promotion za mara kwa mara
Ukiweza weka free wi-fi Ila yenye limit time
Tafuta mpishi anayejua kupika vizuri ili uwe tofauti na wenzio
2:funga CCTV camera kwa ajili ya usalama wa Mali zako na za wateje

3; jua udhaifu wa washindani zako

4 usafi ni jambo ambalo kila mteja atataman kuwa sehemu safi kuanzia
Watu wa service na mazingira kwa ujumla

Wapende wafanya kazi wako hasa kwa kuwapa mishahara kwa wakati
Wajali pia kwa kuwapa offa kila wanapofanya vizuri kwa kufanya hivyo utakuwa karibu nao kila jambo kabla halijatendeka utajulishwa

Tengeneza loyalty card kwa ajili ya wateja wako wa kila mara kupitia loyalty card utawapa offa hasa kahawa, au chai



Ni hayo tu
 
Habari mkuu,
Hongera kwa wazo Bomba kabisa
Wazo Hilo ni mojawapo Kati ya mawazo yangu


Fanya hivi broo,
1, tafuta wafanyakazi wenye Nia ya kufanya kazi, dispiline, na wanaojali kazi
Tengeneza menu Pana (vyakula vya Bei RAHISI na vya Bei ghali pia)
Kuwa tofauti na washindani wako kw promotion za mara kwa mara
Ukiweza weka free wi-fi Ila yenye limit time
Tafuta mpishi anayejua kupika vizuri ili uwe tofauti na wenzio
2:funga CCTV camera kwa ajili ya usalama wa Mali zako na za wateje

3; jua udhaifu wa washindani zako

4 usafi ni jambo ambalo kila mteja atataman kuwa sehemu safi kuanzia
Watu wa service na mazingira kwa ujumla

Wapende wafanya kazi wako hasa kwa kuwapa mishahara kwa wakati
Wajali pia kwa kuwapa offa kila wanapofanya vizuri kwa kufanya hivyo utakuwa karibu nao kila jambo kabla halijatendeka utajulishwa

Tengeneza loyalty card kwa ajili ya wateja wako wa kila mara kupitia loyalty card utawapa offa hasa kahawa, au chai



Ni hayo tu
Mtaji kiasi gani wa kuanza nao hususani Arusha na ni maeneo gani hot kwa Arusha?
 
Wapendwa kama ambavyo nimeandika hapo, naomba msaada wa kitaalamu jinsi ya kuendesha biashara hii.

Sijafungua ila nimesha fanya maandalizi ya chumba pamoja na vifaa baadhi, ishu kubwa itakuwa kwenye kumanage pesa na wafanyakazi nk.
Ukipata muda nenda singida nyuma ya TRA ulizia karestaurant ka mama mmja anaitwa mama clare nenda ufanye survey utajifunza kitu pale
 
Wapendwa kama ambavyo nimeandika hapo, naomba msaada wa kitaalamu jinsi ya kuendesha biashara hii.

Sijafungua ila nimesha fanya maandalizi ya chumba pamoja na vifaa baadhi, ishu kubwa itakuwa kwenye ku-manage pesa na wafanyakazi nk.

Kama wewe sio mfanyakazi au kama ndio unaanza ni vyema kuwapa somo la nini unataka katika biashara yako, wafanyakazi waonr biashara katika jicho lako.
Kama sio mfanyakazi sehemu nyingine unahitaji muda mwingi maana unaweza ukawa na idea ila soko likakupa kitu tofauti so ukiwa pale utagundua mengi na u can flow na utakayokumbana nao
 
Mtaji kiasi gani wa kuanza nao hususani Arusha na ni maeneo gani hot kwa Arusha?
Inategemea na ukubwa na standard ya mgahawa wako
Kuhusu eneo ambalo ni hot

Kama ni mgahawa wa chakula Cha 3000-5000 maeneo ya stand kubwa na maeneo jirani yatakuwa Bora zaidi,

Kama ni migahawa ya Hadhi ya juu
Labda chakula 15000- 90,000 kwa mlo mmoja
Maeneo ya clock tower na maeneo ya jirani yatakuwa Bora zaidi

Kuhusu mtaji siyo fixed
Mfano Mimi nikitaka kufungua mgahawa maeneo ya stand nikiwa na milioni 5-7 itatosha

Ila ikiwa ni maeneo ya clock tower
Mtaji angalau milion 100 na kuendelea
Kwa nini
Kuna vitu vingi mna vya kununua
Mfano
Friza kubwa
Friji za jikoni na za bar
Mashine ya kahawa
Setting na design
Mashine nyinginezo, mfano ice cream machine juicer
Meza za Hadhi ya juu
Majiko makubwa
Salamanda kwa ajili ya kupashia sahani muda wote
Matank Zaid ya moja kwa ajili ya kuhifadhi maji
Microwave
Meza za jikoni
Utengenezaji wa menu na kulipa wafanya kazi
Hasa barista, barman na wapishi
Mishahara Yao Huwa juu kidogo Kati ya 400k -1m+
 
Back
Top Bottom