Msaada jamani! Nini kifanyike?

LoyalTzCitizen

JF-Expert Member
Sep 15, 2010
2,234
883
kWANZA HABARI ZA MISHUGHULIKO WAKUU!

Najua humu kuna wakuu wenye knowledge, skills na peofessionals tofauti na ndio maana tukaitwa great thinkers. Sasa mategemeo yangu pia nitapata mawazo mazuri yanayoeleweka na yenye manufaa sababu nipo katika njia ya panda na niko desperate sana ya kuomba msaada wa kuanzia wapi ili niokoe kiwanja changu na nyumba yangu ambayo nataka kuporwa! naama! KUPORWA na waumini wa dini ya Kiislamu ambao wamenitia majonzi sana na kuninyima usingizi.

Wakuu baada ya kuhangaika sana nilibahatika kununua kiwanja KIBAHA Mkoani ( Low density) kama 18 years ago. Nika mjengea mama yangu mzazi kanyumba kadogo ili ajisitiri na aliishi hapo kama 17 years sasa. Na Ila pia nimeamua kumjengea kanyumba kakubwa kidogo( 3 bedrooms) ili ajinafasi zaidi sababu ya uzee wake.

Sasa mwisho wa mwaka jana ni akavamiwa na waumini wa dini ya kiislamu ambao walivamia hilo eneo na kumega sehemu ya mbele ya kiwanja na kuanza ujenzi haraka sana wa msikiti!. Kuniambia hivyo mimi na sister wangu mkubwa tukaanza mchakamchaka kufuatilia hilo swala maana waumini wale walikuwa hawatupi maelezo ya kueleweka na walikuwa si wakarimu. Misafara ikaanza kuanzia Ardhi, serikali za mitaa, wilayani, mkoani mpaka mahakamani!..

By the way kiwanja kina kila kitu na nyumba zinalipiwa ada ya jengo kila mwaka na ramani zote ninazo za nyumba na mtaa. Ila baada ya muda kama kati ya mwaka jana ilitoka order ya wao kusitisha ujenzi maana wamevamia hapo ni baada ya kuhangaika sana! maana maafisa wa ardhi walikuwa wanatuzungusha sana. Baada ya hapo roho ikatulia na lakini hawakuja kubomoa msingi uliojaa zege mpaka last week waliporudi tena na kasi mpya na kuanza kujenga tena. Kuwauliza wanasema wamepata kibali cha ikulu, kitu ambacho mimi binafsi kinanichanganya kama ni kweli na naomba isiwe kweli maana nitafedheheka sana.

Na leo hii kwenda Ardhi cha kushangaza docs zote za kiwanja hazionekani yaani zimetoweka na wakati kati kati ya mwaka jana zote zilikuwapo na nimepatwa na mshituko mkubwa mno! At this point sielewi nianzie wapi tena maana nachanganyikiwa na utesaji kwa kweli na kila kitu ktk hii nchi! Wakuu naomba ushauri wenu wenye mwanga! huyu bi mkubwa presha isije ikamuondoa. Nini nikifanye sasa ili haki itendeke!? sasa siamini vyombo maana naona kuna kitu kinatendeka underground! Please ktk michango naomba tuheshimu dini ya mwenzako na toa mchango wako bila kutukana au kudhihaki dini tafadhali,. Ahsanteni!

MbRpcUODbgAAAAAASUVORK5CYII=
4QAAAAABJRU5ErkJggg==
MbRpcUODbgAAAAAASUVORK5CYII=



Kama inavyoonekana ktk picha hapo mbele ni msikiti uliomega kiwanya na unajengwa ktk barabara.
 
Mkuu pole sana kwa yaliyokukuta, mimi binafsi sina ufahamu wa masuala ya ardhi ila nina imani humu jamvini kutakuwepo na wataalamu wa kukupa ushauri.
 
Ngoja nisubiri wataalamu!
Kuna NGO inaitwa HAKIARDHI. Ni mchanganyiko wa wanasheria na wanaharakati katika maswala ya ardhi. Sina uzoefu nao vizuri lakini ungewasiliana nao kwa ushauri. Hao waislamu wanasema wana kibali cha Ikulu. Hivi Ikulu sasa ni ofisi ya kugawa ardhi? Mimi ninavyoona hata kama Ikulu ingekuwa imeingilia swala hilo ingetoa amri/maelekezo kwa Maofisa Ardhi Makao Makuu ya Wizara husika au Mkoani washughulikie swala hilo kwa taratibu zinazoeleweka. Kwa vile unasema nyaraka hazionekani huko Wizarani ni wazi kuwa ni rafu zinatendeka, huenda kwa nguvu ya rushwa. Lakini kwa upande mwingine inaonekana siku hizi kuna dini ya kitaifa. Tusishangae.
 
Kuna njia mbili katika kutatua mgogoro wa ardhi ama unafuata mkondo wa kiutawala kwa maana ya kuwaona watu wa idara ya ardhi hasa ama serikali ya mtaa,sana sana idara ya ardhi kwasababu wao tunatarajia watakuwa na kumbukumbu zote muhimu za kiwanja husika na njia ya pili ni mkondo wa mahakama kwa maana ya Baraza la ardhi na nyumba kutegemeana na thamani ya ardhi husika au Mahakama Kuu kitengo cha ardhi,naona wewe kwa sehemu kubwa umeegemea njia moja nayo ni utawala....sasa kama watawala wanakuchakachua fuata mkondo wa mahakama,kashtaki idara husika ya ardhi hapo sasa atakuwa ni Mkurugenzi wa Manispaa, hao jamaa waliokuvamia, hakuna kitu kinachoitwa amri ya rais kwenye land administration ili hyo iwepo ama rais ametwaa ardhi yako na ulipaswa kupewa taarifa na masuala mengineyo kama fidia nk....ebu fuatilia vizuri naona kama kuna harufu ya matumizi mabaya ya madaraka katika ishu yako. Na sio vibaya ukajitafutia kopi ya sheria za ardhi hasa sheria ya ardhi namba 4 maana wewe upo mjini pamoja na sheria ya utatuzi wa migogoro ya ardhi,sheria ya Mipango miji kama rejea za msingi ili uzitambue vizuri haki zako na vyombo mbalimbali vinavyohusika.
 
Pole ndugu kama una vielelezo vyote muhimu basi pia jitahidi umuone Mufti kwani ninavyojua mimi nyumba ya Mungu haijengwi katika ardhi ya dhulma ni makosa makubwa. Wapo waislamu ambao wanafanya mambo pasi na kufuata taratibu za dini na hili hupatikana kwa waumini wa dini nyengine pia sasa pengine umekutana na watu wa aina hii ambao wanaihataji mjuzi awafahamishe. Maana kama nyumba ya ibada itajengwa mahala pasipostahili basi kwa wenye kujua hawawezi kusali hapo. Kwa hiyo mbali ushauri uliopewa jaribu kutizama na huu. Nasema kuwa pengine umekutana na watu wasioelewa kutokana na kauli yao ya kusema kibali kimetoka Ikulu kauli ambayo inaonesha jinsi walivyo na uelewa mdogo.
 
Wakuu hapo juu nashukuru sana tena sana kwa misaada yenu, ni dhahiri kuwa rushwa imetendeka na inaendelea kutendeka huko ndani kwa ndani na hii ndiyo inanitatiza sana maana mahakama ya wilaya walishatoa msimamo wao lakini cha kushangaza hawa ndugu zangu wanakuwa vichwa maji na ni kitu ambacho kinaathiri sana victims ambao ni huyu bi mkubwa. Nitaanza tena kufuatilia kutumia mkondo wa mahakama kuumaana naona hapa Kibaha wananizungusha mpaka nachanganyikiwa, pia wazo la kumuona Mufti pia ni spot on! Mkuu nashukuru na nitafuatilia huko pia na pia nitaweka matokeo ya developments as i go along ili wakuu muone mauzauza yanayotokea nchi hii!! Samahani picha zimegoma sasa nitazisave upya ili muone! Shukrani kwa ushauri wenu mzuri sana.
 
Back
Top Bottom