Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 926
- 4,343
Mobhare Matinyi nipo hapa kukumbusha majukumu yako ila siyo kushurutisha ukafanye kwa mbinu gani. Napenda kukumbusha kwamba wananchi wanasema ofisi yako haina mchakamchaka wa ubunifu kuelekea uchaguzi. Ofisi imekaa kimya kama wizara ya mambo ya Nje. Hapana changamsha nchi kwa makala na habari sisimuzi kuhusu utendaji wa serikali
Sijaja kukumbusha kazi ila nimekuja kukuwazisha uone ni wapi unafanya vizuri na wapi ufanyi vizuri. Apparently, upepo wa kisiasa umeongezeka na miundombinu imeharibika sana kwa mvua. Wenzenu wanaokosoa serikali wapo kazini wakitembea kwenye shida za wananchi na kuzipigia kelele. Amsha maafisa habari wakafanye kazi yao.
Bunge linaendelea lakini ni kama vile hakuna bunge ; si suala zuri sana kiafya ya uchumi na kisiasa. Waulize wenzako katika Muhimili wa nne kwanini bunge limekosa mvuto mtaani? Kwanini matangazo ya bunge yamesusiwa? Kama na wizara ya habari mjiulize lakini kusanyeni maoni ya wananchi na kufahamu wanachotaka
Mwisho; ni hatari kisiasa kuwa na jamii iliyokinai habari za serikali. Lazima urudishe morali ya jamii kuangalia na kufuatilia habari za serikali . Tengenezen hata midahalo ya kimkakati itakayovuta hisia.....oohooo sory; sitaki kukupa mbinu nafahamu unazo nyingi
Sijaja kukumbusha kazi ila nimekuja kukuwazisha uone ni wapi unafanya vizuri na wapi ufanyi vizuri. Apparently, upepo wa kisiasa umeongezeka na miundombinu imeharibika sana kwa mvua. Wenzenu wanaokosoa serikali wapo kazini wakitembea kwenye shida za wananchi na kuzipigia kelele. Amsha maafisa habari wakafanye kazi yao.
Bunge linaendelea lakini ni kama vile hakuna bunge ; si suala zuri sana kiafya ya uchumi na kisiasa. Waulize wenzako katika Muhimili wa nne kwanini bunge limekosa mvuto mtaani? Kwanini matangazo ya bunge yamesusiwa? Kama na wizara ya habari mjiulize lakini kusanyeni maoni ya wananchi na kufahamu wanachotaka
Mwisho; ni hatari kisiasa kuwa na jamii iliyokinai habari za serikali. Lazima urudishe morali ya jamii kuangalia na kufuatilia habari za serikali . Tengenezen hata midahalo ya kimkakati itakayovuta hisia.....oohooo sory; sitaki kukupa mbinu nafahamu unazo nyingi