DOKEZO Mkurugenzi Mtendaji Magu na wenzako, mmetupiga milioni 40 za EP4R Shule ya Msingi Magu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Hagwila

Member
Apr 18, 2019
80
97
Jana tarehe 25/1/2022 wazazi wenye watoto Shule ya Msingi Magu walikuwa na kikao ambacho kiliitishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Shule kwa taarifa kupitia kwa watoto.

Kikao kilihudhuriwa na wazazi wengi (japo siyo wote); lakini mwitikio ulikuwa wenye kuridhisha.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mhe. Diwani na Afisa Mtendaji wa kata ya Magu mjini.

Mengi yalizungumzwa kwa mujibu wa agenda zilizokuwepo; na kwa ufupi mengi yalikwenda vizuri isipokuwa mawili matatu ambayo hayakuafikiwa.

Moja ya masuala ambalo lilikuwa mwiba wa kikao hicho ni kuhusu VYUMBA VITATU VYA MADARASA VILIVYOJENGWA KWA NGUVU ZA WANANCHI KUPOKWA NA MKURUGENZI MTENDAJI H/W MAGU NA KUFANYIA UMALIZIAJI (FINISHING & FURNISHING) KWA KUTUMIA FEDHA SHS MILIONI 40 ZA EP4R

Kwa faida ya wote, EP4R ni kifupi cha Education Program for Results. Hii program inafadhiliwa na Benki ya Dunia (WB), ambapo fedha kwa ajili ya maendeleo ya shule (kupitia mfumo wa fedha wa kiserikali), zinaelekezwa moja kwa moja kwenye eneo husika ili kuepusha uchepushaji.

Shule nyingi zimenufaika na program hii ikiwa ni pamoja na urekebishaji wa ikama (idadi ya waalimu vituoni), ujenzi wa vyumba vya madarasa, vyoo vya wanafunzi na waalimu n.k.

Kwa bajeti ya EP4R, chumba kimoja cha darasa lililokamilika kuanzia ujenzi mpaka kuweka madawati ni Tshs milioni 20, hivyo kwa vyumba viwili vya madarasa Shule ya Msingi Magu zililetwa Tshs milioni 40 ambazo zilikadiriwa kukamilisha ujenzi wa vyumba hivyo viwili vya madarasa mpaka kuweka madawati.

CHA KUSHANGAZA, baada ya fedha hizo milioni 40 kupokelewa, badala ya kujengwa madarasa mapya mawili, Mwalimu Mkuu aliyekuwepo wakati ule Mary Maganga kwa kushirikiana na viongozi wa ofisi ya Elimu (W) Magu pamoja na DED aliyekuwepo wakati huo Lutengano Mwalwiba akishauriwa na Mhandisi wa wilaya ya Magu, waliamua kutumia fedha hizo za EP4R milioni 40 kumalizia vyumba viwili vya madarasa kati ya vyumba vitatu ambavyo tayari vilikuwa vimejengwa KWA NGUVU NA MICHANGO YA WANANCHI KWA 100% mpaka hatua ya kukamilika kwa maboma.

Walibomoa kona mbili na ukuta wa upande mmoja, wakaongeza upana kidogo, wakapunguza idadi ya madirisha, wakaongeza pavement, wakapiga lipu, wakaweka tiles, wakapaua, wakapiga rangi, wakaweka milango na madirisha; milioni 40 kwisha!!😮😮

Hayo yakifanyika, Mwalimu Mkuu aliiweka pembeni Kamati ya Shule, akawa anafanya kazi ya kusimamia mafundi mwenyewe na baadhi ya waalimu wake, huku akipata backup ya ofisi ya Elimu (W) na ofisi ya DED Magu, hususani Mhandisi wa wilaya; na baada ya kumaliza kazi hiyo, madarasa hayo mawili yakaandikwa "DONATED BY EP4R 2021"

Huo ni wizi wa kimachomacho, ambao umefanywa na huyo Mwalimu Mkuu aliyekuwepo kwa kushirikiana na viongozi wa wilaya wa idara ya Elimu na ofisi kuu ya DED Magu.

Diwani wa Kata ya Magu mjini Mhe. Mashaka amelipambania sana suala hili, maana nguvu za wananchi wake zimepokwa na hao niliowataja hapo juu; wametumia kiasi kidogo cha pesa kupoka kazi ya wananchi, badala ya kuanzisha kazi yao mpya kwa pesa ambazo walipokea kama utaratibu wa EP4R unavyoelekeza.
Darasa moja limetelekezwa kati ya hayo matatu.

Jana kikao cha wazazi kimempa DED Magu siku 7 akamilishe umaliziaji wa darasa hilo.
Tunajua DED aliyeko Magu sasa siye aliyekuwepo wakati madudu haya yakifanyika; lakini kwa sababu hiyo ni kazi ya kiofisi ni lazima achukue hatua, bila kujali mtangulizi wake alijikoroga vipi.
Tunajua pia kwamba TAKUKURU Magu wanachunguza suala hilo; lakini pamoja na uchunguzi huo ukiendelea, ni lazima DED Magu achukue hatua ili kuepuka kuwavunja moyo wananchi.

Lakini pia, mamlaka zinazohusika na uchunguzi huo wakiwemo TAKUKURU na Wakaguzi wa OR TAMISEMI ambao walifika kuangalia hali halisi na kubaini kwamba ni kweli wahusika ambao wote ni watumishi wa umma akiwemo Mwalimu Mkuu aliyekuwepo (Mary Maganga) na baadhi ya watumishi wengine wa idara ya Elimu na ofisi kuu ya DED Magu, ni lazima wawajibishwe.

Madudu ni mengi sana ofisi ya Elimu Magu, lakini kwa leo niishie tu hapa. Povu ruksa!!😏
 
Bahati mbaya sina uhakika/matarajio ya kwamba watachukuliwa hatua kama ilivyokuwa kwa utawala wa kiongozi alie pita kwasasa Marehemu. Hivi sasa wameruhusiwa kwa dhati kabisa kutoka ndani ya moyo wa mtawala kwamba wajipimie ila wasivimbiwe. Zaidi zaidi watahamishwa vituo vya kazi waendelee kujipimia.
 
Wakubwa wa elimu msingi Magu ni wababaishaji na wapiga dili tu. Ndiyo maana hayo ya kupiga milioni 40 yametokea magu. Huyo injinia ndiyo waliosimamia ubazilifu ukafanyika. Mkurugenzi alidanganywa na injinia wake hela zikaliwa.

Huyo diwani Mashaka hawezo kusimamia maendeleo, ni mtu wa dili na makesi tu.

Hili la Magu S/Msingi amelisimamia kwa sababu mwalimu maganga alikula na injinia na mabosi wa elimu na mkurugenzi yeye Mashaka akaachwa, anaumwa roho.

Mbona alikula hela milioni mbili zilizotolewa na stregomena tax alipokuwa sadec kwa ajili ya choo cha Nyalikungu hakijaisha mpaka leo ni pagale tu na hakuna kilichofanyika? (Picha chini).

Nafanya kazi za mashule na hela zangu silipwi, nababaishwa tu.

Takukuru Magu fatilieni hivi vitu na mje na suluhisho kabla hatujachukua hatua kwa walimu wakuu na maofisa wao, injinia na mkurugenzi.

IMG_20220203_182851_6.jpg
 
Wakubwa wa elimu msingi Magu ni wababaishaji na wapiga dili tu. Ndiyo maana hayo ya kupiga milioni 40 yametokea magu. Huyo injinia ndiyo waliosimamia ubazilifu ukafanyika. Mkurugenzi alidanganywa na injinia wake hela zikaliwa...
BigWanyamela hawa mabosi wa Magu DC kama wanakubabaisha na pesa zako dawa ni kuwashtaki tu kwa mabosi wao TAMISEMI ilimradi una ushahidi.

Kumbe Diwani Mashaka alikula milioni 2 alizotoa Mhe. Stragomena Tax kwa ujenzi wa choo ambacho mpaka leo hakijaisha na limebaki pagale kama linavyoonekana pichani?

Hivi huyu mama wa watu anajisikiaje anapoona hali hiyo na Magu ni kwao?

BigWanyamela, shitaki hao watu TAMISEMI kwa Naibu Katibu Mkuu Msonde ambaye ni mchapakazi sana.

Nakumbuka alipokuwa NECTA alileta mapinduzi mengi chanya kwenye taasisi hiyo ikazidi kuheshimika.

Namwona hata sasa kwenye vyombo vya habari anavyopambana na wabadhirifu wa mali ya umma na wazembe.

Nikiwa mdau na mkereketwa wa Elimu, namwomba Naibu Katibu Mkuu Msonde aimulike sana idara ya Elimu msingi Magu maana imeoza; siyo kwa sababu ya DEO Hapana; DEO anapambana sana, lakini kuna maofisa wala rushwa pale (tunamshukuru Nyagabona amehamishwa Magu kwenda Misungwi) Lakini Afisa Taaluma aliyepo hapo (JOHARI MWASHA) ni mnyanyasaji sana wa waalimu, anawadharau, anawabeza na kuwanyanyasa sana, kiasi kwamba Mwalimu akiwa na suala la kwenda ofisi ya Elimu wilayani hatamani kabisa kukutana na JOHARI MWASHA; maana ni mtihani. (Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI fuatilia suala hili Kwa waalimu wa Wilaya ya Magu utathibitisha maneno yangu)

Nina hakika kabisa JOHARI MWASHA anamkwaza sana Mkuu wake wa Idara, hata kama huyo binti hasemi; maana unapovuruga waalimu na kuwavunja moyo ambao ndio watenda kazi shambani unategemea mavuno gani? Mwisho wa siku lawama zote zinatupwa Kwa DEO Msingi, ambaye anajitahidi kuwa shock absorber kati ya waalimu na Johari; kwa nini iwe hivyo?

Kama ninyi TAMISEMI mnampenda sana JOHARI MWASHA, labda ana ma-godfather huko wizarani, basi mpeni u-DEO Wilaya nyingine aendelee kuwafurahisha ninyi, au mpeni u-DEO hapohapo Magu mmuhamishe Glory ambaye naamini anateseka sana hapo Magu sababu ya huyo maushungi!! Mkuu Msonde fuatilia hilo; naamini network yako iko super na wewe ni intelligent sana.
 
BigWanyamela hawa mabosi wa Magu DC kama wanakubabaisha na pesa zako dawa ni kuwashtaki tu kwa mabosi wao TAMISEMI ilimradi una ushahidi...
Maushungi yake yameingiaje? Walimu mna majungu sana, shida ni wavivu hampendi Kazi....mkisimamiwa mfanye Kazi mnaanza majungu na fitina.
 
Maushungi yake yameingiaje? Walimu mna majungu sana, shida ni wavivu hampendi Kazi....mkisimamiwa mfanye Kazi mnaanza majungu na fitina.
Mwalimu au mtumishi yeyote mvivu awajibishwe tu kwa taratibu za kazi zilizopo; lakini asinyanyaswe!

Ipo mamlaka ya nidhamu ya waalimu inaitwa TSD; kama mwalimu amethibitika ni mvivu, mzembe, hatekelezi majukumu yampasayo basi ashtakiwe kwenye mamlaka husika ili achukuliwe hatua zinazostahili, lakini kumnyanyasa, kumpuuza na kumdhalilisha siyo njia sahihi kumwadhibu.

Wewe unayesema waalimu ni wavivu huenda ni kilaza tu, hujui majukumu wanayoyatekeleza waalimu katika mazingira magumu, lakini badala ya kutiwa moyo wanaishia kuvunjwa moyo na kunyanyaswa na watu wenye tabia za ovyo kama wakina JOHARI MWASHA anayewanyanyasa mpaka Maofisa Elimu Kata ambao Wana majukumu mapana sana kielimu wilayani.

Kwa JOHARI MWASHA, Afisa Elimu Kata anayefaa kwake ni MBOCHI tu kwa sababu ana mahusiano naye ya ziada; wengine wote walie tu!!
 
Lutengano now yupo bukombe ni mkurugenzi wetu, mbona Hana hati chafu?

Hata Mimi ni mtaalamu wa ujenzi, kinachofanyika mfano fedha ya EP4R ikiletwa say 40mil kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya wanafunzi. Huwa tunaangalia kama Kuna maboma ya wanachi yapo na kuyacheki kama yanakidhi kiwango. Na kama yanakidhi tunayaendeleza Hadi mwisho lengo ni kupana bajeti walau ipatikane fedha ya kutengeneza madawati au viti na meza.

Kwa uzoefu wangu 40mil inajenga vyumba viwili vya madarasa ila sasa changamoto inakula kwenye meta na viti, idadi ya meza na viti kwa vyumba viwili ni 100 seti kwa fedha hiyo mala nyingi hupelea kupata meza na viti kwa idadi inayotakiwa.kwa njia ya kukamilishaa maboma hapo ndipo unaweza toboa.

Mleta hoja inatakiwa utuambie hilo jengo lilikuwa limefika hatua Gani? Kabla ya kuendelezwa ili nikupe tadhimini ya harakaharaka kama kweli hizo 40mil ziliisha au laaa!

Kingine chukuwa bank statement ya shule , certificate za malipo,LPO zote za manunuzi uje actual costs ilikuwa shingapi, hapo ndipo utajua 40mil imepigwa au laaa!

Kwa uzoefu wangu kupiga 10mil kwenye hiyo pesa ni kazi sanaa,lazima tu mradi uyumbe.

Mkuu unatakiwa utupe documents zote, hapa tujilizishee.
 
DEDs si ndio wanakuwaga hawa UVCCM....basi kumbe ni ukoo wa panya kila mtu mwizi
 
Jana tarehe 25/1/2022 wazazi wenye watoto Shule ya Msingi Magu walikuwa na kikao ambacho kiliitishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Shule kwa taarifa kupitia kwa watoto.

Kikao kilihudhuriwa na wazazi wengi (japo siyo wote); lakini mwitikio ulikuwa wenye kuridhisha.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mhe. Diwani na Afisa Mtendaji wa kata ya Magu mjini.

Mengi yalizungumzwa kwa mujibu wa agenda zilizokuwepo; na kwa ufupi mengi yalikwenda vizuri isipokuwa mawili matatu ambayo hayakuafikiwa.

Moja ya masuala ambalo lilikuwa mwiba wa kikao hicho ni kuhusu VYUMBA VITATU VYA MADARASA VILIVYOJENGWA KWA NGUVU ZA WANANCHI KUPOKWA NA MKURUGENZI MTENDAJI H/W MAGU NA KUFANYIA UMALIZIAJI (FINISHING & FURNISHING) KWA KUTUMIA FEDHA SHS MILIONI 40 ZA EP4R

Kwa faida ya wote, EP4R ni kifupi cha Education Program for Results. Hii program inafadhiliwa na Benki ya Dunia (WB), ambapo fedha kwa ajili ya maendeleo ya shule (kupitia mfumo wa fedha wa kiserikali), zinaelekezwa moja kwa moja kwenye eneo husika ili kuepusha uchepushaji.

Shule nyingi zimenufaika na program hii ikiwa ni pamoja na urekebishaji wa ikama (idadi ya waalimu vituoni), ujenzi wa vyumba vya madarasa, vyoo vya wanafunzi na waalimu n.k.

Kwa bajeti ya EP4R, chumba kimoja cha darasa lililokamilika kuanzia ujenzi mpaka kuweka madawati ni Tshs milioni 20, hivyo kwa vyumba viwili vya madarasa Shule ya Msingi Magu zililetwa Tshs milioni 40 ambazo zilikadiriwa kukamilisha ujenzi wa vyumba hivyo viwili vya madarasa mpaka kuweka madawati.

CHA KUSHANGAZA, baada ya fedha hizo milioni 40 kupokelewa, badala ya kujengwa madarasa mapya mawili, Mwalimu Mkuu aliyekuwepo wakati ule Mary Maganga kwa kushirikiana na viongozi wa ofisi ya Elimu (W) Magu pamoja na DED aliyekuwepo wakati huo Lutengano Mwalwiba akishauriwa na Mhandisi wa wilaya ya Magu, waliamua kutumia fedha hizo za EP4R milioni 40 kumalizia vyumba viwili vya madarasa kati ya vyumba vitatu ambavyo tayari vilikuwa vimejengwa KWA NGUVU NA MICHANGO YA WANANCHI KWA 100% mpaka hatua ya kukamilika kwa maboma.

Walibomoa kona mbili na ukuta wa upande mmoja, wakaongeza upana kidogo, wakapunguza idadi ya madirisha, wakaongeza pavement, wakapiga lipu, wakaweka tiles, wakapaua, wakapiga rangi, wakaweka milango na madirisha; milioni 40 kwisha!!😮😮

Hayo yakifanyika, Mwalimu Mkuu aliiweka pembeni Kamati ya Shule, akawa anafanya kazi ya kusimamia mafundi mwenyewe na baadhi ya waalimu wake, huku akipata backup ya ofisi ya Elimu (W) na ofisi ya DED Magu, hususani Mhandisi wa wilaya; na baada ya kumaliza kazi hiyo, madarasa hayo mawili yakaandikwa "DONATED BY EP4R 2021"

Huo ni wizi wa kimachomacho, ambao umefanywa na huyo Mwalimu Mkuu aliyekuwepo kwa kushirikiana na viongozi wa wilaya wa idara ya Elimu na ofisi kuu ya DED Magu.

Diwani wa Kata ya Magu mjini Mhe. Mashaka amelipambania sana suala hili, maana nguvu za wananchi wake zimepokwa na hao niliowataja hapo juu; wametumia kiasi kidogo cha pesa kupoka kazi ya wananchi, badala ya kuanzisha kazi yao mpya kwa pesa ambazo walipokea kama utaratibu wa EP4R unavyoelekeza.
Darasa moja limetelekezwa kati ya hayo matatu.

Jana kikao cha wazazi kimempa DED Magu siku 7 akamilishe umaliziaji wa darasa hilo.
Tunajua DED aliyeko Magu sasa siye aliyekuwepo wakati madudu haya yakifanyika; lakini kwa sababu hiyo ni kazi ya kiofisi ni lazima achukue hatua, bila kujali mtangulizi wake alijikoroga vipi.
Tunajua pia kwamba TAKUKURU Magu wanachunguza suala hilo; lakini pamoja na uchunguzi huo ukiendelea, ni lazima DED Magu achukue hatua ili kuepuka kuwavunja moyo wananchi.

Lakini pia, mamlaka zinazohusika na uchunguzi huo wakiwemo TAKUKURU na Wakaguzi wa OR TAMISEMI ambao walifika kuangalia hali halisi na kubaini kwamba ni kweli wahusika ambao wote ni watumishi wa umma akiwemo Mwalimu Mkuu aliyekuwepo (Mary Maganga) na baadhi ya watumishi wengine wa idara ya Elimu na ofisi kuu ya DED Magu, ni lazima wawajibishwe.

Madudu ni mengi sana ofisi ya Elimu Magu, lakini kwa leo niishie tu hapa. Povu ruksa!!😏
 

Attachments

  • A964508B-4C8B-4B1B-9871-6199531810F7.jpeg
    A964508B-4C8B-4B1B-9871-6199531810F7.jpeg
    71.1 KB · Views: 1
Huwajui watu wa huko wewe, ukute huo ushungi wake ndio unawakera, wanataka maviminii chupi nje🤣

Mimi ushauri wangu awanyooshe tu.
Mbona vimini ni vingi tu tena kwenye pisi kalikali?
Wewe mchombeze tu huyo mwenzio kwamba awanyooshe tu!! Ukijua huu mwenzako anajua ule; ukijua ule, mwenzako anaruka!!
 
Lutengano now yupo bukombe ni mkurugenzi wetu, mbona Hana hati chafu?

Hata Mimi ni mtaalamu wa ujenzi, kinachofanyika mfano fedha ya EP4R ikiletwa say 40mil kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya wanafunzi....
Wewe jamaa; unamtaka mleta uzi akupe documents za ujenzi wa madarasa hayo yeye ndiye mkandarasi au Mwalimu Mkuu au DED Magu?

Anacholalamikia mleta mada ni kuwa, serikali ilitoa milioni 40 za EP4R kwa DED Magu kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mawili pamoja na madawati yake; kwa BOQ ambayo kiasi hicho cha pesa zingetosha kufanya kazi hizo kwa viwango ambavyo serikali iliviweka.

Hizo pesa za EP4R hazikutolewa kwa DED Magu peke yake; ni Halmashauri nyingi zilipewa fedha hizo kwa kiasi hichohicho na kazi ilifanyika kwa kiwango kama kilivyoonyeshwa kwenye BOQ.

Wananchi walichangishwa fedha za ujenzi wa madarasa mawili na yalikuwa yamekamilika mpaka ngazi ya boma.

Kama DED Magu alikusudia kukamilisha madarasa hayo kama ambavyo serikali hufanya kwa miradi mingine ya wananchi, basi angeyamalizia tu kwa vyanzo vingine vya mapato; halafu hayo mawili ya EP4R ambayo ni programu maalum angeyajenga pia, maana hayo yalikuwa na BOQ yake na fedha zake; hata vipimo vya madarasa vilikuwa tofauti na vipimo vya madarasa hayo yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi.

DED Magu na timu yake kweli waliwapiga wananchi kwa sababu walifanya modifications tu kwenye hayo maboma ya wananchi, kwa kuongeza kidogo upana na urefu wa vyumba hivyo ili viweze kulingana na vipimo vilivyoainishwa kwenye vipimo vya madarasa ya EP4R; ambapo upanuzi huo mdogo walioufanya, hauwezi kulingana na thamani ya pesa kwa kazi ambayo hawakuifanya kabisa!

Hizo unazoleta hapa ni porojo tu; DED aliyekuwepo, Engineer, na wahusika wengineo kwenye mnyororo walikula hizo pesa; WALIJIPIMIA WAKALA KILA MMOJA KWA UREFU WA KAMBA YAKE!! Mwizi ni mwizi tu hata kama hatakamatwa!

Wewe ukivunjiwa nyumbani kwako vitu vyako vikaichukuliwa bila ridhaa yako na usimkamate wala kumshtaki aliyevipora hataitwa mwizi?

Acha siasa kwa kuwaambia wananzengo wakuletee LPO, mara Certificates, mara EFD Receipts n.k; wao siyo custodians wa nyaraka hizo; hayo yanawahusu wakaguzi ambao nao kwa vyovyote walilambishwa asali; NANI ATAMFUNGA PAKA 🐈 KENGELE?
 
Wacha wapige ww unajua hali ilivyo mtaani mwalimu tu anazidiwa na mchimba mchanga
Mchimba mchanga ni mfanyakazi aliyejiajiri; anaendesha maisha yake na familia yake.

Mwalimu (wa serikali) ni mtumishi kama mtumishi mwingine yeyote wa umma; wana ngazi mbalimbali za mishahara kulingana na elimu na uzoefu wao.

Kuna waalimu wana raslimali kubwa tu kama mashamba, nyumba, magari, biashara n.k; bado wana guarantee ya serikali kwenye vyombo vya fedha ambapo anaweza kupata mkopo mkubwa akafanya mambo yake.

Miongoni mwao wapo wenye matatizo mbalimbali kama walivyo watumishi wa kwenye kada zingine kama manesi, askari na watumishi wengine, kutokana na historia ya utumishi wao na mienendo yao ya kimaisha.
Wapo maaskari matapeli, wapo manesi, wapo bankers na watumishi wengine wengi watovu wa maadili na wabadhirifu ambao hata wanafukuzwa kazi na wengine wanafungwa, hujawahi kuwaona au hata kusikia?
Wewe unamwona Mwalimu tu kwamba ndiye cheap material ambaye unaweza kumbeza na kumfananisha na mchimba mchanga!

Ok; hata kuchimba mchanga ni kazi, na si ajabu wewe ukaolewa na mchimba mchanga (kama hujaolewa)na akakutunza vizuri akaishi maisha ya furaha kuliko labda hata ungeolewa na afisa wa TRA, banker, Polisi, mwanajeshi n.k ambao ninyi mnawaita husband materials; lakini ukawa umeingia kwenye manyanyaso na majuto ambayo utaishia kuwa mtu wa huzuni kila mara.

Usidharau kazi za watu wengine, maana kazi yako, ya babaako ama ya mamaako; haiwasaidii wengine inakusaidia wewe labda na nduguzo!!
 
Mchimba mchanga ni mfanyakazi aliyejiajiri; anaendesha maisha yake na familia yake.

Mwalimu (wa serikali) ni mtumishi kama mtumishi mwingine yeyote wa umma; wana ngazi mbalimbali za mishahara kulingana na elimu na uzoefu wao...

Kazi ni matendo yoyote HALALI anayoyafanya mtu ili ajipatie riziki yake na wale wanaomtegemea.

kazi ni kazi bora mkono uende kinywani.
Huyo mrembo WrestlerRSF254 aache kudharau wachimba mchanga; hao ndio wanaowezesha madereva wote wa matipa kuwa na kazi, wanawawezesha wenye matipa yao kuwa barabarani, wanawezesha matofali kufyatuliwa, wafyatuaji wanapata kazi, wenye viwanda vya kufyatua matofali wanafanya kazi, simenti inauzwa, nyumba zinajengwa, mafundi mbalimbali na vibarua wao wanapata kazi n.k.

Ni mtu mwenye akili ndogo tu ndye anayeweza kudharau kazi ya mtu mwingine, maana haelewi maana ya multiplied effect!! Achaneni nae huyo; lete pombe 🍻.....!!
 
Mkuu Msonde fuatilia hilo; naamini network yako iko super na wewe ni intelligen
Mheshimiwa Msonde; Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI yawezekana kweli Magu DC ofisi ya Elimu kuna shida, jaribu kuwahoji baadhi ya waalimu na waratibu; unaweza ukapata majibu yanayoweza kukuongoza kufanya masahihisho kwenye hiyo ofisi.
Mbona hiyo JOHARI MWASHA analalamikiwas sana?
 
Back
Top Bottom