TAI DUME
JF-Expert Member
- Feb 20, 2014
- 9,040
- 23,714
Huyo mwamba pichani upande wa kushoto alipata kuwa nabii mkubwa sana huko Nigeria kwenye miaka ya 80 na 90. Anaitwa nabii Daniel Abodunrin. Unambiwa mwamba alikuwa anafanya miujiza mikubwa mikubwa , alitabiri mambo kwa ufasaha na alikuwa na wafuasi wa kutosha ambao walimwamini sana. Yote hayo aliyafnaya kupitia maandiko matakatifu ya kwenye Bibilia.
Ilikuwa mwaka 1991, huko mjini Ibadani ambapo nabii huyu aliamua kuwaaminisha wafuasi wake kwamba ameoneshwa na Mungu kwamba anaweza kufanya miujiza mikubwa kama waliofanya manabii wa kale ikiwemo hata kuingia kwenye kwenye kibanda cha simba (lion den) wenye njaa kali na akatoka salama kama alivyofanya wajina wake nabii Daniel (ile stiory ya Daniel kutupwa kwenye pango la simba na akatoka salama). Kwahiyo huyu mwamba akaitangazia dunia anayetaka kuona miujiza ya Mungu ya nabii kuingia kwenye kwenye banda la simba wenye njaa na akatoka salama basi tukutane kwenye maonesho ya "saba saba" ya Nigeria yanayofanyika katika viwanja vya chuo kikuu cha Ibadan - Nigeria.
Unaambiwa hiyo siku na saa takatifu ilipowadia umati ulikuwa mkubwa sana mpaka kufikia polisi kuzuia watu kuingia viwanjani. Nabii Daniel wa nigeria aliingia hapo viwanjani akiwa amevalia joho jekundu na Bibilia mkononi. Nabii akaoneshwa banda lenye simba sita wakubwa tupu. Uongozi ulijaribu kumzuia lakini kwa kuwa mpaka alisha lipia zoezi hilo na kwa kuwa aliwahakikishia hakuna kitachompata, na endapo kutakuwa na madhara yoyote itakuwa ni juu yake, basi uongozi ukamwacha afanye anachotaka.
Mwamba akalisogelea banda akalizunguka mara saba huku akinena kwa lugha na mambo mengine kama ambavyo tunawaona manabii wa huku wakifanya. Then akaamuru sasa mlango wa cage ufunguliwe, kisha ufungwe kwa kufuli, na asisogee mtu mpaka atakapoita afungulwe baada ya muujuza kutokea, maana Mungu anayemwamini anaenda kutenda makuu sasa.
Nabii akaingia kwenye cage akiwa na bibilia pamoja na msalaba mikononi mwake huku akiwa bado ananena kwa lugha kusifu ukuu wa Mungu. Unaambiwa alipoingia tu mle ndani huku akiwaonyeshea wale simba msalaba walirudi nyuma kwa hofu kuu. Raia zikashangila, nabii akapata kichwa na kwa ujasiri mkuu akatangazia umma show mbona bado, subirini naenda kumpanda simba mmoja mgongoni kama farasi. Watu mayowee. Nabii akaanza kumsogelea simba mmoja, simba akaa standby. Unaambiwa gafla bin vuu simba wakaanza kumshambulia nabii.
Mashuhuda wanasema wale simba walinyang'anyana minofu ya nabii Daniel kama hawana akili nzuri, Unaambiwa wale simba ni kama walijua huyu nabii anataka kupata umaarufu kupitia wao, yaani nabii aliwakera hasa. Simba walisema bora hata angeenda peke yake ila sio kuwadhalilisha mbele ya watu wengi vile. Hawakukubali. Wakang'ata nyama za nabii mpaka alivokufa. Cha ajabu wale simba walifahamu nabii kafa hawakujishughulisha nae tena, maana kwa kawaida wangeanza kutafuna nyama pale pale bali wao wakalala chini wakimuangalia tuu huku kucha na meno yao vikiwa vimejaa damu. Huo ndio ukawa mwisho wa nabii Daniel Abodunrin wa huko Naijeria.
MY TAKE: Nafikiri nabii alijizima data makusudi akijisahaulisha kwamba Mungu hajaribiwi. Mungu huwa hapangiwi cha kufanya kwa kumjaribu, yeye ndie anaamua wakati gani na kwanani ajidhihirishe nguvu zake. Hata kama mimi ningekuwa Mungu ningemkataa.
Wasalaam kwa leo