Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,899
- 155,954
MFALME CONSTANTINE I WA ROMA
Huwezi kuutaja UKRISTO katika dola ya Roma bila kumtaja Mfalme Constantine I ukifanya hivyo huenda historia yako hiyo isikamilike
Kwa sababu hapo awali Wafalme waliopita kabla yake walikuwa wanaamini katika dini zao za jadi lakini Mfalme Constantine ndio alikuwa mtawala wa kwanza katika dola ya Roma kuukubali ukristo na kuuamini na kisha akafanya kazi kubwa kuhakikisha unasambaa maeneo makubwa ulaya
-alitangaza jumapili kuwa ni mapumziko ya wakristo wote
-Alijenga kanisa takatifu la Sepulchre (The Church of the Holy Sepulchre) linalopatikana katika mji wa Jerusalem
- Aliweza kuwawezesha viongozi wa dini kiuchumi ili waweze kutangaza dini
- Kuifanya ukristo kuwa ni dini rasmi ya dola ya Roma.
Kabla ya hapo ukristo ulikuwepo katika himaya hiyo ya Roma lakini waliishi kwa kunyanyaswa, kunyang'anywa mali zao na uovu mwengine.. hadi pale Mfalme Constantine I alipoukubali na kuipitisha dini hiyo kisheria...Wengine wanasema Constantine I ndio mleta amani wa ukristo ndani ya Roma
JE, CONSTANTINE NI NANI?
Jina kamili la mfalme Constantine I ni Flavius Valerius Constantinus alizaliwa mwaka 280 na kufariki mwaka 337
Mama yake aliitwa Helena yeye aliamua kuwa mkristo mapema kabisa na baada ya mwanae kuamua kuwa mkristo basi alifanya kazi kubwa kuhakikisha ukristo unaenea
Baba ake alikuwa ni mwanajeshi mkubwa alifariki wakati wameenda kuvamia nchi moja ulaya inasemekana ni uingereza lakini baada ya kifo chake wale wanajeshi wakamchagua yeye kuwa kiongozi wao
Alianza kutawala upande wa magharibi kuanzia mwaka 312 hadi 324 na kisha kuitawala dola nzima ya Roma kuanzia 324 had 337
Kwanini tunasema mfalme Constantine ni miongoni mwa wafalme wakubwa duniani?
- Chini ya himaya yake aliufanya mji wa Constantinople kuwa mji wenye nguvu na tajiri zaidi. Mji wa Constantinople ndio hii Istanbul ya sasa inayopatikana uturuki ambao bado ni maarufu duniani
- Wengine wanasema kuwa Mfalme Constantine kuukubali ukristo ni namna ya kujiimarisha kisiasa lakini tukiachana na hayo.... Kupitia ukristo uliifanya himaya ya Roma kuwa ni yenye nguvu zaidi duniani hasa katika karne ya 4
- Ukiachana na mafanikio yake katika Vita na mabadiliko ya kisiasa yalioifanya Roma kuwa kuwa kubwa lakini pia ukimtoa Augustus hakuna mfalme mwengine aliyekaa madarakani muda mrefu kumzidi Constantine
- Ndie muanzilishi wa himaya ya Byzantine ambao mji mkuu wake ndio uliitwa Constantinople ...na hii byzantine iliyokuwa chini ya Roma baadae ilijitenga na ikawa chimbuko la kanisa la Orthodox
Huwezi kuutaja UKRISTO katika dola ya Roma bila kumtaja Mfalme Constantine I ukifanya hivyo huenda historia yako hiyo isikamilike
Kwa sababu hapo awali Wafalme waliopita kabla yake walikuwa wanaamini katika dini zao za jadi lakini Mfalme Constantine ndio alikuwa mtawala wa kwanza katika dola ya Roma kuukubali ukristo na kuuamini na kisha akafanya kazi kubwa kuhakikisha unasambaa maeneo makubwa ulaya
-alitangaza jumapili kuwa ni mapumziko ya wakristo wote
-Alijenga kanisa takatifu la Sepulchre (The Church of the Holy Sepulchre) linalopatikana katika mji wa Jerusalem
- Aliweza kuwawezesha viongozi wa dini kiuchumi ili waweze kutangaza dini
- Kuifanya ukristo kuwa ni dini rasmi ya dola ya Roma.
Kabla ya hapo ukristo ulikuwepo katika himaya hiyo ya Roma lakini waliishi kwa kunyanyaswa, kunyang'anywa mali zao na uovu mwengine.. hadi pale Mfalme Constantine I alipoukubali na kuipitisha dini hiyo kisheria...Wengine wanasema Constantine I ndio mleta amani wa ukristo ndani ya Roma
JE, CONSTANTINE NI NANI?
Jina kamili la mfalme Constantine I ni Flavius Valerius Constantinus alizaliwa mwaka 280 na kufariki mwaka 337
Mama yake aliitwa Helena yeye aliamua kuwa mkristo mapema kabisa na baada ya mwanae kuamua kuwa mkristo basi alifanya kazi kubwa kuhakikisha ukristo unaenea
Baba ake alikuwa ni mwanajeshi mkubwa alifariki wakati wameenda kuvamia nchi moja ulaya inasemekana ni uingereza lakini baada ya kifo chake wale wanajeshi wakamchagua yeye kuwa kiongozi wao
Alianza kutawala upande wa magharibi kuanzia mwaka 312 hadi 324 na kisha kuitawala dola nzima ya Roma kuanzia 324 had 337
Kwanini tunasema mfalme Constantine ni miongoni mwa wafalme wakubwa duniani?
- Chini ya himaya yake aliufanya mji wa Constantinople kuwa mji wenye nguvu na tajiri zaidi. Mji wa Constantinople ndio hii Istanbul ya sasa inayopatikana uturuki ambao bado ni maarufu duniani
- Wengine wanasema kuwa Mfalme Constantine kuukubali ukristo ni namna ya kujiimarisha kisiasa lakini tukiachana na hayo.... Kupitia ukristo uliifanya himaya ya Roma kuwa ni yenye nguvu zaidi duniani hasa katika karne ya 4
- Ukiachana na mafanikio yake katika Vita na mabadiliko ya kisiasa yalioifanya Roma kuwa kuwa kubwa lakini pia ukimtoa Augustus hakuna mfalme mwengine aliyekaa madarakani muda mrefu kumzidi Constantine
- Ndie muanzilishi wa himaya ya Byzantine ambao mji mkuu wake ndio uliitwa Constantinople ...na hii byzantine iliyokuwa chini ya Roma baadae ilijitenga na ikawa chimbuko la kanisa la Orthodox