Mjadala wa Wachangiaji M1 JF Jukwaa la Historia 2013

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,928
30,279
MJADALA WA WACHANGIAJI M1 JF Jukwaa la Historia 2013

Yericko Nyerere (pichani) miaka 11 iliyopita alifungua uzi JF kwa nia ya kupinga historia ya uhuru wa Tanganyika kama nilivyoieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

Huu ukawa mjadala mkali, mrefu uliokwenda kwa miezi sita mfululizo bila ya kusimama, uliopitiwa na wasomaji milioni moja.

Wasomaji waliosimama kama kundi moja wakimuunga mkono Yericko Nyerere walikataa kuwa Waislam na Uislam hauna cha kujivunia katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hawa walikuwa wakali kwa lugha na wakati mwingine walitoa vitisho na matusi.

Wachangiaji wachache hawajai kiganjani waliniunga mkono wakishikilia kuwa nimeandika historia ya kweli ambayo imefuta historia iliyokuwa haina ithibati.

Mimi nilisimama kwenye ukweli kuwa historia niliyoandika ndiyo historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika na historia ya kweli ya Julius Kambarage Nyerere katika uhusiano wake na wenyeji wa Dar es Salaam.

Mjadala kama huu haujapata kutokea tena na umeweka rekodi ya pekee sasa muongo mmoja umefika.

Leo nimeshangaa kuona uzi huu umewekwa JF Jukwaa la Historia na mwanachama anaejiita "Ubongokid," akiomba mnakasha ule wa watu milioni moja ufanywe kitabu.

1713468407465.png

Yericko Nyerere
1713468461384.png



 
Nakumbuka sana Ila Yericko alikushinda Kipindi hicho maana Alikuwa na watu wengi Sana..

Japo ninaunga Mkono hoja ya mnakasha huo kuwekwa kwenye kitabu maana pia unanikumbusha ID yangu ya Zamani..maana mlikutana ma "Nguli wa Historia"...

Japo Yericko alikuwa na Hoja nyingi sana kukuzidi maana Alionyesha vingi sana..
Hivi ule uzi bado upo??
 
Nakumbuka sana Ila Yericko alikushinda Kipindi hicho maana Alikuwa na watu wengi Sana..

Japo ninaunga Mkono hoja ya mnakasha huo kuwekwa kwenye kitabu maana pia unanikumbusha ID yangu ya Zamani..maana mlikutana ma "Nguli wa Historia"...

Japo Yericko alikuwa na Hoja nyingi sana kukuzidi maana Alionyesha vingi sana..
Hivi ule uzi bado upo??
Dr. Mambo...
Si kama nataka kujisifu ila nataka kukueleza ukweli.

Hakuna wa kunishinda katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Na sababu yake ni moja tu.
Mimi nimeandika historia ya wazee wangu ambao ndiyo walioasisi African Association 1929 na wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika 1933), wakampokea Julius Nyerere 1952 na wakaunda chama cha TANU 1954.

Niliyoandika hakuna aliyekuwa anayajua katika hao wote watu milioni moja ila wachache sana.

Kuwa na watu wengi wanaokuunga mkono si ushindi.

Ushindi ni kuwa na historia ambayo hakuna aliyekuwa anaijua.

Vipi Yericko anishinde mimi?

Wala hao unaowaita manguli wa historia hawakuwa wameandika lolote katika si paper wala kitabu.

Mimi nimeingia katika mjadala nikiwa na "track record," nzito.

Nimeandika vitabu kadhaa, nimezungumza vyuo vikuu kadhaa Afrika, Ulaya na Marekani na nimechapwa katika Cambridge Journal of African History na nikiwa mmoja wa waandishi 500 walioandika Dictionary of African Biography (DAB).

Naamini umeelewa.
 
Dr. Mambo...
Si kama nataka kujisifu ila nataka kukueleza ukweli.

Hakuna wa kunishinda katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Na sababu yake ni moja tu.
Mimi nimeandika historia ya wazee wangu ambao ndiyo walioasisi African Association 1929 na wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika 1933), wakampokea Julius Nyerere 1952 na wakaunda chama cha TANU 1954.

Niliyoandika hakuna aliyekuwa anayajua katika hao wote watu milioni moja ila wachache sana.

Kuwa na watu wengi wanaokuunga mkono si ushindi.

Ushindi ni kuwa na historia ambayo hakuna aliyekuwa anaijua.

Vipi Yericko anishinde mimi?

Wala hao unaowaita manguli wa historia hawakuwa wameandika lolote katika si paper wala kitabu.

Mimi nimeingia katika mjadala nikiwa na "track record," nzito.

Nimeandika vitabu kadhaa, nimezungumza vyuo vikuu kadhaa Afrika, Ulaya na Marekani na nimechapwa katika Cambridge Journal of African History na nikiwa mmoja wa waandishi 500 walioandika Dictionary of African Biography (DAB).

Naamini umeelewa.
Hahahaaaa... Mzee Said kipenzi cha mtume Muhammad (s.a.w). Mtetezi wa uislam. Usie na mswalie mtume dhidi ya makafir. Mfia dini mmoja. Mwarabu wa roho. Mwanahistoria isiyotamatika bila kuchomekea uislam na mchango wake chanya. Mwandishi na mwanaharakati nguli wa historia ya Tanganyika. Unalianzisha tena? Kitu pekee nakusifu, huna mihemko. Huna majibu mabaya kwa mtu.
 
Hahahaaaa... Mzee Said kipenzi cha mtume Muhammad (s.a.w). Mtetezi wa uislam. Usie na mswalie mtume dhidi ya makafir. Mfia dini mmoja. Mwarabu wa roho. Mwanahistoria isiyotamatika bila kuchomekea uislam na mchango wake chanya. Mwandishi na mwanaharakati nguli wa historia ya Tanganyika. Unalianzisha tena? Kitu pekee nakusifu, huna mihemko. Huna majibu mabaya kwa mtu.
Raia...
Mbona unaandika kwa kejeli?

Mjadala huu ni wa kisomi ukiingiza lugha hizo utauharibu.

Mimi si nilieurejesha tena mjadala huu.

Rejea kuisoma post.
 
Dr. Mambo...
Si kama nataka kujisifu ila nataka kukueleza ukweli.

Hakuna wa kunishinda katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Na sababu yake ni moja tu.
Mimi nimeandika historia ya wazee wangu ambao ndiyo walioasisi African Association 1929 na wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika 1933), wakampokea Julius Nyerere 1952 na wakaunda chama cha TANU 1954.

Niliyoandika hakuna aliyekuwa anayajua katika hao wote watu milioni moja ila wachache sana.

Kuwa na watu wengi wanaokuunga mkono si ushindi.

Ushindi ni kuwa na historia ambayo hakuna aliyekuwa anaijua.

Vipi Yericko anishinde mimi?

Wala hao unaowaita manguli wa historia hawakuwa wameandika lolote katika si paper wala kitabu.

Mimi nimeingia katika mjadala nikiwa na "track record," nzito.

Nimeandika vitabu kadhaa, nimezungumza vyuo vikuu kadhaa Afrika, Ulaya na Marekani na nimechapwa katika Cambridge Journal of African History na nikiwa mmoja wa waandishi 500 walioandika Dictionary of African Biography (DAB).

Naamini umeelewa.
Kaka Mohamed said!

Nakufahamu Vizuri sana Kaka Yangu,
Nimekuwa Nikikufatilia na Nimenunua Vitabu vyako na ninavisoma,

Na kuna Baadhi ya Vitabu vyako nilivikuta Library ya vyuo Mbalimbali England..

Na kwenye Andiko langu Nimekiri kwamba wewe ni nguli wa Historia..

Nakiri kufahamu Isnad yako (Sanadi) ya Hadithi ni safi na haina Mushkeli kabisa..Kwa hiyo sina hofu na Historia Zako..

Nilichokizungumza Ni Hoja na kwamba Yericko Nyerere alitoa Hoja Nyingi sana ambazo wengi waliziamini..

Wakati wewe Hoja zako zilikuwa Chache na wachache Waliziamini ikiwemo Mimi..
Ila Sikuwa na Lengo wa Kudisqualify wala kudefame kazi yako kubwa...

Natamani Ule Uzi uwepo nionyeshe ninachosema!

Ni kama tu Mahakamani Haijalishi Mtuhumiwa Ni mkweli Kiasi gani ila ana ushahidi na hoja kiasi gani ndo kitakachomuokoa..

Asante
 
Kaka Mohamed said!

Nakufahamu Vizuri sana Kaka Yangu,
Nimekuwa Nikikufatilia na Nimenunua Vitabu vyako na ninavisoma,

Na kuna Baadhi ya Vitabu vyako nilivikuta Library ya vyuo Mbalimbali England..

Na kwenye Andiko langu Nimekiri kwamba wewe ni nguli wa Historia..

Nakiri kufahamu Isnad yako (Sanadi) ya Hadithi ni safi na haina Mushkeli kabisa..Kwa hiyo sina hofu na Historia Zako..

Nilichokizungumza Ni Hoja na kwamba Yericko Nyerere alitoa Hoja Nyingi sana ambazo wengi waliziamini..

Wakati wewe Hoja zako zilikuwa Chache na wachache Waliziamini ikiwemo Mimi..
Ila Sikuwa na Lengo wa Kudisqualify wala kudefame kazi yako kubwa...

Natamani Ule Uzi uwepo nionyeshe ninachosema!

Ni kama tu Mahakamani Haijalishi Mtuhumiwa Ni mkweli Kiasi gani ila ana ushahidi na hoja kiasi gani ndo kitakachomuokoa..

Asante
Dr. Mambo,
Unaandika vizuri sana.
Watanzania waliamini historia iloyokuwepo kwa miaka mingi historia iliyowafuta wazalendo wengi na muhimu katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mimi siwalaumu kwa hilo.

Nilichofanya niliandika kitabu ambacho ndani yake nilieleza historia ya hawa ambao hawakutajwa kwenye historia pamoja na Julius Nyerere.

Hamkuwa mnawajua waaasi wa African Association 1929 wala kisa cha Dr. Aggrey na Kleist Sykes 1924.

Dr. Aggrey ndiye aliyemtia hamasa Kleist Sykes kuunda African Association.

Mimi nilikuwekeeni mpaka majina ya waasisi wa African Association: Cecil Matola (President), Kleist Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Suleiman Majisu, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima, Rawson Watts na Raikes Kusi.

Na nikaeleza kwa ushahidi madhubuti kuwa historia hii kaiandika Kleist mwenyewe kwa mkono wake kabla hajafariki 1949 ukitaka kuisoma ipo Maktaba ya Chuo Kikuu East Africana "The Life of Kleist Sykes," (Ref. No. JAN/HIST/143/15 (1968) na mwandishi ni mjukuu wa Kleist, Aisha "Daisy" Sykes binti ya Abdul Sykes.

(Daisy alikuwa mwanafunzi Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki 1968 akisoma Education na History).

Mwalimu wake wa historia alikuwa John Iliffe.

Halikadhalika historia hiyo ni sura katika kitabu alichohariri John Iliffe, "Modern Tanzanians," (1973).

Nikaeleza na mengine mengi kuwa mipango ya kuunda TANU ilianzabm 1950 na TAA Political Subcommittee na wajumbe wake ni hawa: Dr. Vedasto Kyaruzi (President), Abdul Sykes (Secretary), Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Hamza Mwapachu, Steven Mhando na John Rupia.

Ati nina hoja chache.
Mimi nina ukweli.

Mimi ndiye mtafiti pekee niliyefunguliwa Nyaraka za Sykes na kutoka nyaraka hizo ndiyo nikaanfika historia ya uhuru wa Tanganyika nikianza na mazungumzo ya Dr. Aggrey na Kleist Sykes mwaka wa 1924.

Mimi sina tatizo la kuaminiwa.

Mtu anaweza akaamini kuwa Nyerere ndiye aliyeunda TANU lakini mimi najua Nyerere kaikuta TANU nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu mwaka wa 1952.

Baba yangu kaona haya yote kwa macho yake na kwa mara ya kwanza kamuona Nyerere nyumbani kwa Abdul Sykes 1952 na kamuona Nyerere akiishi nyumba hiyo alipoacha kazi ya ualimu.

Naijua historia ya TANU kwa kuwa ni historia ya wazee wangu na mimi ni sehemu ya historia hii.

Unajua kuwa babu yangu Salum Abdallah ni muasisi wa TANU Tabora 1954 na muasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) akiwa President na Secretary Kassanga Tumbo?
 
Kaka Mohamed said!

Nakufahamu Vizuri sana Kaka Yangu,
Nimekuwa Nikikufatilia na Nimenunua Vitabu vyako na ninavisoma,

Na kuna Baadhi ya Vitabu vyako nilivikuta Library ya vyuo Mbalimbali England..

Na kwenye Andiko langu Nimekiri kwamba wewe ni nguli wa Historia..

Nakiri kufahamu Isnad yako (Sanadi) ya Hadithi ni safi na haina Mushkeli kabisa..Kwa hiyo sina hofu na Historia Zako..

Nilichokizungumza Ni Hoja na kwamba Yericko Nyerere alitoa Hoja Nyingi sana ambazo wengi waliziamini..

Wakati wewe Hoja zako zilikuwa Chache na wachache Waliziamini ikiwemo Mimi..
Ila Sikuwa na Lengo wa Kudisqualify wala kudefame kazi yako kubwa...

Natamani Ule Uzi uwepo nionyeshe ninachosema!

Ni kama tu Mahakamani Haijalishi Mtuhumiwa Ni mkweli Kiasi gani ila ana ushahidi na hoja kiasi gani ndo kitakachomuokoa..

Asante
Uzi ni huu Hapa:


Bado niko Nausoma.Naamni kabisa ni Uzi ambao unahitaji kufanywa kitabu ama na Mzee wetu Mohamed Said ama na Yericko Nyerere.Au Wanaweza Kufanya JOINT PROJECT.Kwamba Waandike Historia ya Uhuru wetu katika MFUMO wa CRITICAL ANALYSIS.

Muhimu ni Facts zilizomo kule zifanyiwe tafiti zaidi na ziwekwe katika namna ambayo vizazi vijavyo vinaweza sasa kusoma HISTORIA ya TANGANYIKA kwa KUONA nafasi wazee walivyoshiriki katika IMANI zao za KIDINI,UKABILA,UBIN,n.k.

Wanaweza PIA kufanya HISTORIA HII IWE na MUUNGANIKO wa HISTORIA YA BAADA ya UHURU MPAKA nyakati hizi kwa kuzingatia Malalamiko ya Waislamu,Nafasi za Wakristu,Ishu za Zanzibar,Mpaka Nyakati ZETU.TUNAWEZA KUKIPA KITABU JINA ambalo LITAFAA-HISTORIA ya TANZANIA-TOLEO LA MILENIA. au HISTORIA ya TANZANIA na MTAZAMO wa JAMII.Naamini kabisa Maxence Melo Mello anaweza KUSPONSOR KITABU kupitia JAMII FORUM JUKWAA La Stories of CHANGE au JUKWA la HISTORIA.
 
Uzi ni huu Hapa:


Bado niko Nausoma.Naamni kabisa ni Uzi ambao unahitaji kufanywa kitabu ama na Mzee wetu Mohamed Said ama na Yericko Nyerere.Au Wanaweza Kufanya JOINT PROJECT.Kwamba Waandike Historia ya Uhuru wetu katika MFUMO wa CRITICAL ANALYSIS.

Muhimu ni Facts zilizomo kule zifanyiwe tafiti zaidi na ziwekwe katika namna ambayo vizazi vijavyo vinaweza sasa kusoma HISTORIA ya TANGANYIKA kwa KUONA nafasi wazee walivyoshiriki katika IMANI zao za KIDINI,UKABILA,UBIN,n.k.

Wanaweza PIA kufanya HISTORIA HII IWE na MUUNGANIKO wa HISTORIA YA BAADA ya UHURU MPAKA nyakati hizi kwa kuzingatia Malalamiko ya Waislamu,Nafasi za Wakristu,Ishu za Zanzibar,Mpaka Nyakati ZETU.TUNAWEZA KUKIPA KITABU JINA ambalo LITAFAA-HISTORIA ya TANZANIA-TOLEO LA MILENIA. au HISTORIA ya TANZANIA na MTAZAMO wa JAMII.Naamini kabisa Maxence Melo Mello anaweza KUSPONSOR KITABU kupitia JAMII FORUM JUKWAA La Stories of CHANGE au JUKWA la HISTORIA.
Shukrani sana..
Na Naunga Mkono hoja..
CC: Yericko Nyerere na Mohamed Said
 
Uzi ni huu Hapa:


Bado niko Nausoma.Naamni kabisa ni Uzi ambao unahitaji kufanywa kitabu ama na Mzee wetu Mohamed Said ama na Yericko Nyerere.Au Wanaweza Kufanya JOINT PROJECT.Kwamba Waandike Historia ya Uhuru wetu katika MFUMO wa CRITICAL ANALYSIS.

Muhimu ni Facts zilizomo kule zifanyiwe tafiti zaidi na ziwekwe katika namna ambayo vizazi vijavyo vinaweza sasa kusoma HISTORIA ya TANGANYIKA kwa KUONA nafasi wazee walivyoshiriki katika IMANI zao za KIDINI,UKABILA,UBIN,n.k.

Wanaweza PIA kufanya HISTORIA HII IWE na MUUNGANIKO wa HISTORIA YA BAADA ya UHURU MPAKA nyakati hizi kwa kuzingatia Malalamiko ya Waislamu,Nafasi za Wakristu,Ishu za Zanzibar,Mpaka Nyakati ZETU.TUNAWEZA KUKIPA KITABU JINA ambalo LITAFAA-HISTORIA ya TANZANIA-TOLEO LA MILENIA. au HISTORIA ya TANZANIA na MTAZAMO wa JAMII.Naamini kabisa Maxence Melo Mello anaweza KUSPONSOR KITABU kupitia JAMII FORUM JUKWAA La Stories of CHANGE au JUKWA la HISTORIA.
Ubongokid,
Kama kuchapwa kitabu isiwe ati unatafutwa ukweli.

Kitabu kichapwe kwa madhumuni ya kuonyesha yaliyochangiwa na wasomaji ili kudhihirisha jinsi historia ya uhuru ilivyokuwa imevurugwa.

Kuna picha ya Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bibi Titi Mohamed na Tatu bint Mzee wamepiga na Nyerere uwanja wa ndege wakimsindikiza safari ya kwanza UNO, Yericko amewakanusha na kusema wale ni "airhostess" wa East African Airways.

Vichekesho kama hivi visomwe.
Yericko anadai kuwa African Association iliasisiwa 1927 wakati ukweli kwa ushahidi iliasisiwa 1929.

Yericko anasema ofisi ya African Association ilitolewa na serikali kuwapa Waafrika wakati ukweli ni kuwa ilijengwa kwa kujitolea kati ya mwaka 1929 hadi 1933.

Miaka 10 hii toka mjadala ule nimeandika mengi JF Jukwaa la Historia katika historia ya uhuru kupita mwandishi yeyote yule na wasomaji wameielewa historia ya kweli.

Kuchapwa mjadala ule kama ulivyokuwa utabainisha ukweli.

Ukweli wa kitabu cha Abdul Sykes uko bayana msomaji ni khiyari yake kuukubali au kuukataa.
 
Kuna picha ya Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bibi Titi Mohamed na Tatu bint Mzee wamepiga na Nyerere uwanja wa ndege wakimsindikiza safari ya kwanza UNO, Yericko amewakanusha na kusema wale ni "airhostess" wa East African Airways.
Alisema walikuwa watawa wa Maryknoll. 😆😆
 
Uzuri wa @Yerricko Nyerere alikua anajenga hoja katika mtazamo wa maslahi mapana ya umoja wa kitaifa
Mpaji...
Unajenga vipi umoja kwa kufuta historia ya wapigania uhuru?

Kuna mtu kaniuliza swali mahali fulani na hapo chini ni jibu langu:

"Suala la historia ya uhuru wa Tanganyika lilikuja hadharani kwa njia ya kitabu mwaka wa 1998 kitabu cha Abdul Sykes kilipochapwa London kwa Kiingereza.

Historia ndani ya kitabu hiki iliwashangaza watu wengi sana kwani wasomaji walisoma mambo ambayo hawakupata kuyasikia hata siku moja.

Halikadhalika waliona picha ndani ya kitabu ambazo hawakupata kuziona hata siku moja.

Mfano mdogo waliona picha ya ofisi ya African Association siku ilipofunguliwa na Gavana Donald Cameron mwaka wa 1933.

Katika picha hiyo Kleist Sykes yumo katika kitabu na kaelezwa kama muasisi na mfadhili wa jumuiya hiyo.

Mtu aliyemtia hima kufanya hilo akiwa Dr. Kwegyir Aggrey kutoka Ghana walipokutana Dar es Salaam mwaka wa 1924.

Ndani ya kitabu ipo historia yake na hayo niliyoandika mimi nimeeleza yanatokana na mswada wa kitabu alioandika kabla hajafariki mwaka wa 1949.

Mswada huu ukatolewa hadharani na mwanae mkubwa Abdul Sykes mwaka wa 1968.

Ndani ya kitabu wasomaji wamesoma mengi mageni pamoja na historia ya Dome Okochi Budohi Mluya kutoka Kenya mwanachama wa African Association na mmoja wa waasisi wa TANU kadi yake ya TANU No. 6.

Ndani ya kitabu kuna picha nimepiga na Dome Budohi nyumbani kwake Ruiru, Nairobi mwaka wa 1972 mimi nikiwa na umri wa miaka 20.

Dome alinifahamu mimi Dar-es-Salaam nikiwa mtoto mdogo miaka ya mwanzoni 1950s.

Haya ni machache katika mengi ya kushangaza.

Kitabu kiliwashtua watu wengi wakisema hiyo haikuwa historia waliyokuwa wakiifahamu.

Watu wengi wakaniomba kitabu kifasiriwe kwa Kiswahili ili Watanzania wengi wanufaike.

Mwaka wa 2002 kitabu cha Kiswahili kikachapwa Nairobi.

Mpaka sasa kitabu kimechapwa mara nne tunakwenda toleo la tano.

Kitabu kimevutia wengi khasa kwa kueleza mchango wa Waislam katika kuunda mikakati ya siasa kupambana na ukoloni na jinsi walivyomuunga mkono Julius Nyerere.

Hapa ndipo unapokutana na historia ya Abdul Sykes na ndugu zake Ally na Abbas na rafiki zake Dossa Aziz na Hamza Mwapachu.

Hapa ndipo unapokutana na masheikh wanasiasa waliopigania uhuru wa Tanganyika: Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.

Kitabu kinaeleza wazalendo wengine waliokuwa majimboni kama Ali Migeyo, Haruna Taratibu, Sued Kagasheki, Paul Bomani, Yusuf Olotu kwa kuwataja wachache.

Kitabu kinaeleza historia za wanawake waliopigania uhuru kama Tatu bint Mzee, Shariffa bint Mzee, Dharula bint Abdulrahman, Amina Kinabo, Lucy Lameck kwa kuwataja wachache.

Kitabu kimependwa sana.

Lakini wakatokea watu wakataabishwa na kitabu hiki na sababu ni Uislam.

Hawa kila kukicha kwa karibu miaka 11 sasa wananiuliza maswali mengi kuhusu historia ya uhuru.

Watu wanauliza imekuwaje historia hii haitambuliki?

Na wewe umeniuliza nini kusudi langu?

Swali la kuwa kwa nini historia hii haikupata kuandikwa naulizwa kila siku na jibu langu ni kuwa swali hilo si muhimu tena kwani nimeandika tayari historia hiyo na kitabu kipo huu mwaka wa 25.

Swali la nini kusudio la kitabu kusudio ni kuandika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa manufaa ya kizazi kijacho ili tusiwe jamii isiyokuwa na historia.

Kwa kazi hii nimepokea tuzo tano hadi hivi sasa."
 
Mtu anaweza akaamini kuwa Nyerere ndiye aliyeunda TANU lakini mimi najua Nyerere kaikuta TANU nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu mwaka wa 1952.
Mwenyewe umeandika humu mara kadhaa kwamba kadi namba 1 ya TANU alipewa Nyerere, aliipaje hiyo kadi kama TANU aliikuta kwa kina Sykes! Haikuwa na wanachama hadi Nyerere alipopata uongozi?
 
Mwenyewe umeandika humu mara kadhaa kwamba kadi namba 1 ya TANU alipewa Nyerere, aliipaje hiyo kadi kama TANU aliikuta kwa kina Sykes! Haikuwa na wanachama hadi Nyerere alipopata uongozi?
Gagnija,
TANU Card No. 3, Abdulwahid Kleist Sykes, Card No. 2 Ally Kleist Sykes na Card No. ni ya TANU Territorial President Julius Kambarage Nyerere.

Kadi 1000 za kwanza za TANU alichapisha Ally Sykes kutoka mfukoni kwake.

Kadi ya Nyerere iliandikwa na Ally Sykes.

Usajili wa TANU ulikabidhiwa kwa Abdul na Ally Sykes na Julius Nyerere.

Kuna historia ya kusisimua sana katika usajili wa TANU.

Nitaweka video In Shaa Allah.

Kuikuta TANU kwa Sykes maana yake ni kuwa fikra na harakati za kuunda chama alikuwanayo Abdul Sykes toka alipokuwa Burma katika Vita Kuu Vya Pili Vya Dunia.


View: https://youtu.be/vpcen88eGJs
 
Back
Top Bottom