Miaka 60 ya Muungano, napendekeza kufutwa kwa kombe la Mapinduzi tubakize kombe la Muungano peke yake ambalo kilele chake kitakuwa siku ya Muungano

PAZIA 3

JF-Expert Member
Jan 30, 2018
1,078
1,870
Habari za Leo wapenda soccer?
Natumai kichwa/title ya thread hii imejieleza vizuri. Nimewaza nikaona nitumie platform hii kwenu ili kama itawezekana, tushawishi viongozi wa mpira kuiondoa michuano ya Mapinduzi cup na badala yake tubaki na Muungano cup. Nasema hivi siyo kwa lengo la kisiasa ila nikwasababu ya ratiba za ligi mbalimbali zinazozikabili timu zetu za mpira. Lakini pia ukichunguza kwa kina, utagundua kuwa, Mapinduzi cup inajumuisha timu za Muungano, yaani zinazotoka bara na zile za Zanzibar, kingine, muda wa Mapinduzi cup ni mwezi January na Muungano cup ni mwezi April, hapo tutalaumu timu zetu tu pale zitakaposusia Moja ya mashindano fulani. Kwakuwa viongozi wetu wamelifufua kombe la Muungano, ni vyema sasa tuondoe Mapinduzi cup tubaki na Muungano cup kwa mantiki kwamba kombe la Mapinduzi linataswila ya Muungano.
Cha kuboresha tu katika kulifanya kombe la Muungano, kuwe na timu at least 16, nane zitoke bara na nane zitoke visiwani. Makundi yapangwe mapema na mashindano hayo yaanze mapema ili mpaka kufikia kilele Cha mashindano hayo, tuwe na timu nne tu zitakazocheza nusu fainali na fainali katika wiki ya kilele Cha sikukuu ya Muungano.
Huu ni mtazamo wangu, mnaweza kuboresha mawazo yangu ili kupata wazo Bora zaidi.
Ahsanteni
 
Habari za Leo wapenda soccer?
Natumai kichwa/title ya thread hii imejieleza vizuri. Nimewaza nikaona nitumie platform hii kwenu ili kama itawezekana, tushawishi viongozi wa mpira kuiondoa michuano ya Mapinduzi cup na badala yake tubaki na Muungano cup. Nasema hivi siyo kwa lengo la kisiasa ila nikwasababu ya ratiba za ligi mbalimbali zinazozikabili timu zetu za mpira. Lakini pia ukichunguza kwa kina, utagundua kuwa, Mapinduzi cup inajumuisha timu za Muungano, yaani zinazotoka bara na zile za Zanzibar, kingine, muda wa Mapinduzi cup ni mwezi January na Muungano cup ni mwezi April, hapo tutalaumu timu zetu tu pale zitakaposusia Moja ya mashindano fulani. Kwakuwa viongozi wetu wamelifufua kombe la Muungano, ni vyema sasa tuondoe Mapinduzi cup tubaki na Muungano cup kwa mantiki kwamba kombe la Mapinduzi linataswila ya Muungano.
Cha kuboresha tu katika kulifanya kombe la Muungano, kuwe na timu at least 16, nane zitoke bara na nane zitoke visiwani. Makundi yapangwe mapema na mashindano hayo yaanze mapema ili mpaka kufikia kilele Cha mashindano hayo, tuwe na timu nne tu zitakazocheza nusu fainali na fainali katika wiki ya kilele Cha sikukuu ya Muungano.
Huu ni mtazamo wangu, mnaweza kuboresha mawazo yangu ili kupata wazo Bora zaidi.
Ahsanteni
Hapo 5imba hatapata kombe.
 
Kombe la muungano ni zuri ila nadhani ratiba yake si rafiki hasa kama team zitaenda mbele zaidi mashindano ya caf
Binafsi nadhani ni vema tubaki na makombe haya ambayo ni yana maana NBC CRDB NGAO CAFS basi
Kombe la muungano haliwezi kutoa mwakilishi CAF maana kuna sehemu itakosa uwakilishi hasa znz

Hivyo Kombe la muungano ni la kisiasa tu na kudumisha umoja

Kwasasa tunafaidika maana TFF wanapeleka Timu 4 CAF , huku ZFF inapeleka timu 2 CAF....kwa maana hiyo ZFF na TFF zinapeleka Timu 6 CAF
 
Back
Top Bottom