Mbunge Dkt. Joseph Mhagama: Maandalizi ya Uchaguzi Mkuu Kutumia Fedha za Ndani

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,988
960

Mbunge Dkt. Joseph Mhagama: Maandalizi ya Uchaguzi Mkuu Kutumia Fedha za Ndani

“Kamati inapongeza jitihada za Serikali kuendelea kupanga bajeti ili kutekeleza miradi mingi zaidi kwa kutumia fedha za ndani. Kwa umahususi, Kamati inaipongeza Serikali ya awamu ya sita chini ya usimamizi mahiri, hodari na shupavu wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mara ya kwanza kutenga fedha za maandalizi ya uchaguzi Mkuu kwa kutumia fedha za ndani bila utegemezi wowote wa fedha za nje.”

“Hata hivyo, katika uchambuzi wake, Kamati imebaini kwamba, ipo haja ya Serikali kutenga fedha za ndani katika mradi wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi kwani hadi kufikia Februari 2024 mradi huo ulipokea asilimia 57.17 tu ya fedha za nje zilizoidhinishwa. “

Amesema Dkt. Joseph Mhagama, Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati akitoa taarifa ya Kamati hiyo kuhusu Utekelezaji wa Bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu.

IMG-20230208-WA0266.jpg
mfuko-pic-data.jpg
 
Chaguzi za Africa ni matumizi mabaya ya Kodi za wananchi shida ya afrika sio chaguzi.Ni mfumo.
Uchaguzi ni njia ya kubadilishana wezi WA Kodi za wananchi linatoka kundi fulani linaingia jingine kuiba
 
Chaguzi za Africa ni matumizi mabaya ya Kodi za wananchi shida ya afrika sio chaguzi.Ni mfumo.
Uchaguzi ni njia ya kubadilishana wezi WA Kodi za wananchi linatoka kundi fulani linaingia jingine kuiba
Hujaishi Ulaya au Marekani wewe. Huko ndio kwenye madanguro ya wezi wa kodi za Wananchi. Wanatoka wale, wanaingia wengine
Ushasikia drain the swamp....

Una hasira sana na Afrika. Ati unajaribu kutatua matatizo ambayo hayatatuliki?

Wacha kujistress
 
Hujaishi Ulaya au Marekani wewe. Huko ndio kwenye madanguro ya wezi wa kodi za Wananchi. Wanatoka wale, wanaingia wengine
Ushasikia drain the swamp....

Una hasira sana na Afrika. Ati unajaribu kutatua matatizo ambayo hayatatuliki?

Wacha kujistress
Kule cheza na pesa yako na sio kodi za wananchi unapotea hakuna aliyejuu ya sheria kama afrika huku jela ni kwa ajili ya watu masikiini
 
Kule cheza na pesa yako na sio kodi za wananchi unapotea hakuna aliyejuu ya sheria kama afrika huku jela ni kwa ajili ya watu masikiini
Wewe bongo dili , haya maneno ungekuwa unayatamka 1980's labda, ningesema 'ah Ulaya bana' na sio nyakati hizi kila mtu anaweza pata taarifa kwa kukohoa tu...Hivi unataka kuudanganya umma wa Watanzania kwamba huko Marekani na Uingereza na Asia jela ni kwaajili ya watu Matajiri? Au Kwamba pesa za kodi zao Hazichezewi? Masafi ya mtuuumeee , eh?

Haya.
 
Back
Top Bottom