Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,803
- 19,913
Kama kuna upigaji wa kura ulifanyika kihalalai unalalamika nini.Ndugu wana bodi.
Kupitia vyanzo vyangu makini vya kimtandao nimepokea taarifa kuwa kamati kuu ya CHADEMA imefanya uamuzi kwa kupiga kura. Uamuzi wa kupendekeza nani awe mpeperusha bendera mkuu wa CHADEMA katika uchaguzi wa mwaka huu 2020. Yaani mgombea Urais.
Ukweli ni kwamba kati ya watu 8 waliorudisha fomu ni watu wawili tu wenye ushindani.
1. Mh Tundu Lissu
2. Mh Lazaro Nyalandu.
Hawa wote ni wenyeji wa mkoa wa Singida na wote ni wajumbe wa kamati kuu ya chadema taifa.
Binafsi nilishitushwa sana kiasi cha kubadilisha mapigo ya moyo wangu baada ya kuona matokeo ya kura za maoni za kamati kuu ya CHADEMA.
Kilichonishitua ni kuona ``think tank`` ya CHADEMA inaamini Mhe Lazaro Nyalandu ni bora kuliko Mhe Tundu Lissu aliyekinga chama kwa damu yake na risasi 16 ambazo mpaka sasa hatujajua Kama kweli zilikuwa zinampiga au malaika walitega migongo yao ndio ikapigwa lisasi kwa niaba yake? Kwasababu mpaka sasa watanzania na wanachadema bado wanajiuliza huyu jamaa aliponaje!!
Bila kutia chumvi yafuatayo ni matokeo ya tatu bora za maoni ya kamati kuu ya CHADEMA
KURA ZA WAGOMBEA URAIS JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KAMA ZILIVYOPIGWA NA KAMATI KUU YA CHADEMA, DAR ES SALAAM, JULY 22, 2020
*IDADI YA KURA ZILIZOPIGWA - 29*
*KURA ILIYOHARIBIKA - 1*
*IDADI YA KURA HALALI -28*
*Lazaro S. Nyalandu - 28* ( 100%)
*Tundu Antipasi Lissu - 24* (86%)
*Dr. Mayrose K. Majinge - 23* ( 82%)
Haya ndiyo majina yatakayo kwenda Baraza Kuu la CHADEMA.
Baada ya matokeo haya nikaanza upelelezi kujua nini kimejiri Kaka Tundu Lissu azidiwe kura na mh Lazaro Nyalandu.
Uchunguzi wangu umebaini kuwa Mhe Aikael Mbowe na Nduguye Mhe Godbless Lema ndiyo walikua nyuma kuhakikisha kuwa Lazaro Nyalandu anamzidi kura za maoni Mhe Tundu Lissu katika maoni ya Kamati kuu.
Kwa ufupi naambatanisha chat za Whatsapp kati ya Mhe Lema na Mhe Mbowe baada ya matokeo ya kura hizo.
Na nina ushahidi thabiti watu wanne waliomnyima kura Lissu ni wafuatao.
1. Freeman Mbowe.
2. Godbless Lema.
3. Halima Mdee.
4. Esther Bulaya.
Pia nichukue wasaa huu kuwajulisha Mhe Esther Matiko na kaka Patrick Ole Sosopi kuwa makini katika siasa zao ndani ya chadema Mwamba hawatazami kwa jicho rafiki.
Wajumbe wa baraza kuu na mkutano mkuu wa chadema taifa wanaopinga mpango wa Mwamba kumuunga mkono Lazaro Nyarandu na ambao wanamuunga mkono mh Tundu lissu,mjiandae pia kisaikolojia yajayo yanafurahisha.
Sasa nimeanza kuamini kwanini wanachama wa chadema na viongozi wengi walikuwa wanatimkia vyama vya Nccr mageuzi na ccm wakisema Kuna tatizo naona sasa linaanza kuwa dhahiri machoni kwa watanzania na wanachama wa chadema.
Ni wenu.