Abdull Kazi
JF-Expert Member
- Dec 29, 2012
- 326
- 255
Kwanza hujazana kwa wingi Kituoni iwe Mwenge Tazara,Mwananchi Relini
Tabata Baracuda,Segerea,Temeke,Mtoni Madafu Chanika,Mbande na kwingineko ambako ni rahisi kusimamisha daladala
Na wanakuwa wengi kuliko daladala.
Roho mtakatifu wao kawapa ufunuo wa kujua jina la dereva na konda, kuliko namba za gari.
Daladala ikisimamishwa anashuka konda, gari inapaki mbali.,roho mtakatifu wao hataki kuonana na dereva hata kidogo labda washindwane na Kondakta
Baada ya dakika moja utaona konda anarudi na kuruhusu gari iendelee na safari.
Roho mtakatifu wa matrafiki kawapa uwezo wa kuona kosa la gari kupitia mwili, uso, sauti ya kondakta na kupeana mikono tu.
Wakiitazama sura ya konda na zile sare zao. Wanajua gari ina vibali, ina taa, breki, bima na shokapu imara.
Ndio maana hawana muda mchafu wa kukagua zaidi ya kuongea na konda.
Tena roho mtakatifu wao alielekeza wakamate daladala tu.
Roho mtakatifu wao kawapa muda maalum wa kuwepo eneo la kazi kuwa kuanzia alfajiri na kuondoka saa nne asubuhi, siyo zaidi ya hapo.
Bila shaka roho mtakatifu anakuwa kawaelekeza wakanywe supu haraka.
Bahati nzuri roho mtakatifu wao kawapa sharti rahisi sana juu ya kupokea karatasi zenye zisizozidi 2000,labda uwe na kesi maalum
Kwa hakika Jambo hili ni la kipekee sana nchini mwetu, inafaa wazungu waje kuiga kwetu
Tabata Baracuda,Segerea,Temeke,Mtoni Madafu Chanika,Mbande na kwingineko ambako ni rahisi kusimamisha daladala
Na wanakuwa wengi kuliko daladala.
Roho mtakatifu wao kawapa ufunuo wa kujua jina la dereva na konda, kuliko namba za gari.
Daladala ikisimamishwa anashuka konda, gari inapaki mbali.,roho mtakatifu wao hataki kuonana na dereva hata kidogo labda washindwane na Kondakta
Baada ya dakika moja utaona konda anarudi na kuruhusu gari iendelee na safari.
Roho mtakatifu wa matrafiki kawapa uwezo wa kuona kosa la gari kupitia mwili, uso, sauti ya kondakta na kupeana mikono tu.
Wakiitazama sura ya konda na zile sare zao. Wanajua gari ina vibali, ina taa, breki, bima na shokapu imara.
Ndio maana hawana muda mchafu wa kukagua zaidi ya kuongea na konda.
Tena roho mtakatifu wao alielekeza wakamate daladala tu.
Roho mtakatifu wao kawapa muda maalum wa kuwepo eneo la kazi kuwa kuanzia alfajiri na kuondoka saa nne asubuhi, siyo zaidi ya hapo.
Bila shaka roho mtakatifu anakuwa kawaelekeza wakanywe supu haraka.
Bahati nzuri roho mtakatifu wao kawapa sharti rahisi sana juu ya kupokea karatasi zenye zisizozidi 2000,labda uwe na kesi maalum
Kwa hakika Jambo hili ni la kipekee sana nchini mwetu, inafaa wazungu waje kuiga kwetu