Malawi yadai kuishtaki Tanzania kwenye Umoja wa Afrika(AU)

Very wrong! Takwimu hazina mikono na miguu kwenda na kupigana vita. Achana na vita. Nakumbuka wakati wa vita ya Tanzania na Uganda sisi tuishio ukanda wa ziwa licha ya kuwa ni mbali na mpakani tulikuwa hatuna amani. Hata ukiona jani linaelea majini unadhani ni bomu la adui. Tuliacha mikusanyiko na hata kwenda kwenye nyumba za ibada kwa kuhofia kushambuliwa na adui. On top of that, baadhi ya watu walifia kwenye mahandaki kwa kuumwa na nyoka. So, achana na kitu kinachoitwa vita - it's ugly na has neither friend nor relative!
Mkuu ndio mana kwenye comments zangu nyingi kwenye huu uzi nimerudia mara nyingi kusema sitamani vita.

Mimi sio muumini wa vita isiyo kua na lazma...sipendi vita kabisa. Hata pamoja na kwamba kitakwimu tuko superior...bado tutaumia na ni jambo la kuepukwa kwa nguvu zote.
 
Nimesoma koment zao wengi wanaona Malawi iko powerful sana kijeshi kwamba wataipiga tz kirahisi kama vita itatokea. Hawa jamaa wametusumbua sana toka enzi za kamuzu banda nadhani ifike wakati sasa tufanye maamuzi magumu
Hapa Dar wamalawi wengi wamehamia na kufanyakazi za house boy isejekua hivi vijamaa ni viasakari vya malawi kuna haja ya kupitisha operesheni kali ya kuwarudisha wamalawi wote kwao kwa kutumia wenyeviti wa serikali wa mtaa na immigration.Tusije kulianzisha kumbe vijamaa vimejipanga tukaingia aibu.
 
Rais Mutharika akianzisha vita walinzi wake watamkamata na kumkabidhi kwa JPM. Nani anataka anataka vita Malawi. Dunia nzima mpaka ukiangukia majini basi mnagawana. Hata wanyama rukusa kuvuka mipaka. Mutharika anatamaa ameambiwa kuna mafuta ziwani amepanic.
 
Tuliambiwa baada ya vita baina yetu na Uganda tufunge mikanda miezi 18 matokeo yake mpaka leo tupo tumefunga na bado mambo hayajakaa sawa. Usicheze kabisa na vita, unaweza ukakuta hawa jamaa wameanza kujiandaa kupigana na sisi kipindi kirefu sisi hatujui kama ilivyotokea Uganda tukiingiza pua tu gharama yake kuwapiga ikawa kubwa badala ya miezi miwili unashangaa miaka. Sasa ikiwa hivyo na kauchumi ketu haka si itakuwa ndio basi tena. Ikibidi usuluhishi ufanyike ili mradi hawazuii tusiendelee kuyatumia maji yetu. Wapo Maraisi wastaafu kutoka South Africa na Mozambique sijui wamefikia wapi mpaka kusuluhisha shauri hili hawa jamaa wanataka kutushitaki AU. Sisi kijijini kwetu walikuwepo wamalawi wengi na baada ya wazazi wao kufariki tunaendelea kuwalea wajukuu zao na tumeawapa mpaka ardhi na sasa hivi tunawahesabu ni wanakijiji wenzetu, lakini huyu bwana amesahau fadhili yetu sisi watanzania na yeye mwenyewe aliishi muda mrefu kama mkimbizi hapa petu. Shukurani ya punda ni mateke.
 
Hapo ndipo penye mtihani kwa serekali ya Tanzania tuone ni kitu gani kitatokea,kwani raia na wananchi wa Tanzania walioichagua serekali iliopo madarakani,wanapojaribu kupeleka malalamiko na madai yao juu mambo ambayo wanaamini kuwa serekali yao inayakiuka,wanajibiwa kuwa Mimi sijaribiwi,sitaki kusikia fyokofyoko,ningekuwa Mimi ningewatimuwa wote.

Safar hii madai yametoka kwa raia wasiyo kuwa watanzania,ambao hata kura hawakuipa serekali ya Tanzania,Wao na serekali yao,wanataka kuimega ardhi inayomilikiwa na Tanzania kwa njia za halali ama zisizo za halali,Je na wao watapewa majibu Kama yale wanayo pewa wananchi wenye serekali yao,ya Mimi huwa sijaribiwi,sitaki kusikia fyokofyoko?.

Au tutegemee kupata jambo tofauti kabisa kutoka kwenye serekali yetu ambalo kwa raia mwenye serekali hajawahi kulipata la serekali yetu kukubali kukaa meza moja na wamalawi Ili kulimaliza suala hilo kwa amani?wakati raia watanzania wamekuwa wakiomba fursa Kama hiyo lakini wanachoambulia ni lugha za kejeli na zenye maudhi.
 
Hawa dawa yao tuwazamishe kwenye ziwa Nyasa wanywe maji wakitoka humo wanakuwa wamevimbiwa
 
Mm nimeishi nao,kwa miaka miwili,tena nimeishi nao ndani ndani kabisa,huko kwenye mitaa ya kiswahili kama ndirande,Zambia,majiga,chinseu hapo Blantyre na Lilongwe pia,najua wanakasirika wakisikia habari hizi za ziwa Nyasa/lake Malawi,wana hasira haswa,walishawafukuza watanzania kwenye masoko yao makuu kama Blantyre market na mengineyo mwaka 2013..na mwaka huo huo walikua wanamlaumu Rais Joyce Banda kwamba alikua anamchekea kikwete,so walitaka Rais mwanaume ambae ni bingu mutharika....ndo mana wamempata na wanaanzisha tena..ngoja tuone.
 
Em naomben mnijuze.. kwanini wanasema ziwa n lao. Kwan mkanganyiko ulianzia wap?
 
Wakuu lakini Vita ni determination na purpose kumbukeni Israel ni kanchi kadogo ila waarabu wote wame surrender pale Malawi kanchi kadogo je ni dhaifu hivo?
 
Mm nimeishi nao,kwa miaka miwili,tena nimeishi nao ndani ndani kabisa,huko kwenye mitaa ya kiswahili kama ndirande,Zambia,majiga,chinseu hapo Blantyre na Lilongwe pia,najua wanakasirika wakisikia habari hizi za ziwa Nyasa/lake Malawi,wana hasira haswa,walishawafukuza watanzania kwenye masoko yao makuu kama Blantyre market na mengineyo mwaka 2013..na mwaka huo huo walikua wanamlaumu Rais Joyce Banda kwamba alikua anamchekea kikwete,so walitaka Rais mwanaume ambae ni bingu mutharika....ndo mana wamempata na wanaanzisha tena..ngoja tuone.
Kwa hiyo inaonekana matatizo yao ya kiuchumi yanasababisha ku put blame kwa waTz??
 
malawi ana watu nyuma wanaompa kiburi,nashangaa watu kuitazama malawi kama ka nchi kadogo. bora ufanyike usuruhishi tusije ongea mengine humu.
Wala usihofu kiburi alikuwa nacho Kamuzu Banda miaka ile kwa msukumo wa Makaburu na bado Nyerere ali muadhibu hebu tizama nchi zinazo izunguka malawi ni ipi inaweza kuwa against Tanzania na ikampa jeuri,kuna yule Bibiye Joyce Banda baada ya kelele zake kwa awamu iliyopita Viongozi wetu wa kijeshi walipita mpakani kufanya survey tu kuona hali ilivyo na zile zikawa salamu tosha na hakutia neno mpaka anaondoka.
 
Hivi vita na malawi nayo kweli itaitwa vita? Mbona kwa JWTZ hii ni kazi ya siku mbili tu. Hata hatuhitaji kupeleka vikosi vya ziada huko...walio huko wanatosha. Sema tu sisi ni taifa ambalo linapenda amani.
Usimbeze MTU kwa udogo wake maana naona sisi watanzania tunawazalau sana hawa wanyasa inabidi tuwenao making isije ikawa hadithi ya Saudi na Goliath
 
Yaani Ramani ya Mkoloni ndiyo iwatoe ufahamu hawa jamaa zetu? . Nimeicho ramani yetu toka nikiwa msingi na mpaka wetu ukiwa ndani ya Ziwa toka enzi hizo. Hawa jamaa Wamalawi nadhani wanataka tuishi nao kama Wapalestina na Waisraeli.
Mkuu hilo ndo linalonishangaza. Hii ramani tumeichora kama inavyotakiwa iwe. Itabidi "watuformat" akili zetu zote ndo hilo lifanikiwe
 
Back
Top Bottom