Makonda: Siko tayari kumkatisha tamaa Rais Samia Suluhu kwa kunipa cheo cha RC

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
22,125
18,775
Sote tunafahamu na tunatambua kuwa uchawa (chawaism) upo katika nchi hii na katika ngazi tofauti za uongozi, lakini kitendo cha mtu kuonyesha uchawa uliopitiliza ni zaidi ya uzwazwa. Nilipomsikia Profesa Kabudi akisema kuwa Magufuli ni Mungu wake nilidhani ni masikhara. Kumbe Rais akikuteua kushika wadhaifa fulani, tayari anachukua nafasi ya Mungu wako?

Wakati RC Makonda akiongea kuhusu rushwa huko Arusha, amesema Dr Samia ni Mungu wake, hivyo hayuko tayari kumuumiza. Mambo yasiwe mengi, hebu msikilize wewe mwenyewe kwenye video hapo chini usije ukasema nimemuwekea maneno kinywani mwake.


MAONI YANGU
Hata mtu uwe na njaa au uwe ni mwenye kujikomba kiasi gani, tafadhali sana usimfananishe mwanadamu na Mwenyezi Mungu, Bwana wa majeshi, Muumba wa mbingu na nchi. Hii ni kufuru iliyovuka mipaka. Ifike wakati tutumie akili zetu vizuri tuache kufananisha vitu visivyofanana kwa sababu tu ya kutetea matumbo yetu.

Nawasilisha.

Pia soma
.
RC Makonda: Rais Samia ameipendelea Arusha, amemtoa mwanae wa pekee na kumleta Arusha
 
Hapana hapa unemchomekea bwana. Hapo alipofika kwa Mungu wangu kuna koma/pumziko ndio akamtaja Mh. Rais Dkt Samia

Asieh ningesema hili nalo ni ajabu jingine ingawa kama yeye akikiri kuwa huyo ni Mungu wake sisi wengine tutafanyaje sasa???
 
Kwann mkuu unakataa makondaa kuamini mama samia n MUNGU wakee??

MUNGU unayemwamini ww kunamtu alishakukataza kumwaminii mkuu!!

Naona mwache aamini anachoamini mkuu
Huoni kuwa anakufuru mkuu? Je, Mungu akiamua kumzushia gharika ya adhabu ni nani atamuokoa?
 
Acha uzushi wewe na acha kuandika kwa kukurupuka. Hapo Mheshimiwa Makonda amesema kuwa hayupo tayari kumuumiza Mungu, pia hayupo tayari kumkatisha Tamaa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Msipende kukurupuka na kuleta uchongaishi na uzushi usio na maana.acheni chuki binafsi pamoja na roho mbaya. Mtashindana na Mwamba lakini hamtamuweza maana ameinuliwa na Mungu na analindwa na mkono wa Mungu ambaye uso wake huambatana na Mheshimiwa Makonda popote awapo.
 
"Bongo akili kubwa inaendesha akili ndogo
wajinga ndo wanakimbilia siasa.." -Ney
Ni kweli kabisa mkuu. Akili ndogo itatusumbua sana hadi Mungu atakapofanya muujiza na kuitupilia mbali kutoka nchi hii.
 
Sote tunafahamu na tunatambua kuwa uchawa (chawaism) upo katika nchi hii na katika ngazi tofauti za uongozi, lakini kitendo cha mtu kuonyesha uchawa uliopitiliza ni zaidi ya uzwazwa. Nilipomsikia Profesa Kabudi akisema kuwa Magufuli ni Mungu wake nilidhani ni masikhara. Kumbe Rais akikuteua kushika wadhaifa fulani, tayari anachukua nafasi ya Mungu wako?

Wakati RC Makonda akiongea kuhusu rushwa huko Arusha, amesema Dr Samia ni Mungu wake, hivyo hayuko tayari kumuumiza. Mambo yasiwe mengi, hebu msikilize wewe mwenyewe kwenye video hapo chini usije ukasema nimemuwekea maneno kinywani mwake.

View attachment 2976801
MAONI YANGU
Hata mtu uwe na njaa au uwe ni mwenye kujikomba kiasi gani, tafadhali sana usimfananishe mwanadamu na Mwenyezi Mungu, Bwana wa majeshi, Muumba wa mbingu na nchi. Hii ni kufuru iliyovuka mipaka. Ifike wakati tutumie akili zetu vizuri tuache kufananisha vitu visivyofanana hata kwa sababu tu ya kutetea matumbo yetu.

Nawasilisha.

Pia soma
.
RC Makonda: Rais Samia ameipendelea Arusha, amemtoa mwanae wa pekee na kumleta Arusha
Duuuh
 
Huoni kuwa anakufuru mkuu? Je, Mungu akiamua kumzushia gharika ya adhabu ni nani atamuokoa?
Wapi alipokuru? Kwanini umekurupuka kuanzisha uzi bila kusikiliza vizuri? Au una matatizo ya masikio na kuelewa? Huoni kwamba kuna koma na sentensi mbili zinatojigeemea hapo? Huoni amesema wazi hayupo tayari kumuumiza Mungu, lakini pia hayupo tayari kumkatisha Tamaa Daktari Samia Suluhu Hasssan kwa kumteua ukuu wa mkoa wa Arusha?

Kama una chuki zako binafsi basi ondoa hapa na usifikiri kuwa wote ni wajinga kama wewe
 
Acha uzushi wewe na acha kuandika kwa kukurupuka. Hapo Mheshimiwa Makonda amesema kuwa hayupo tayari kumuumiza Mungu, pia hayupo tayari kumkatisha Tamaa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Msipende kukurupuka na kuleta uchongaishi na uzushi usio na maana.acheni chuki binafsi pamoja na roho mbaya. Mtashindana na Mwamba lakini hamtamuweza maana ameinuliwa na Mungu na analindwa na mkono wa Mungu ambaye uso wake huambatana na Mheshimiwa Makonda popote awapo.
Sikiliza kwa makini usikurupuke. Mungu aliyekuwa amemlenga ni Daktari Samia Suluhu Hassan. Hebu msikilize vizuri. Hapo alikuwa anaweka msisitizo ndio maana akaongezea hayo maneno. Nenda shule ukasome upya mkuu.
 
Kuna chawa mmoja yeye alisema Mungu ni mwanamke sasa huyo Bashite labda baada ya kutafakari ameona mwanamke mwenyewe anayezungumziwa na yule chawa mwenzake ni huyo aliyempa cheo kwa sababu yeye ameona ametendewa muujiza ambao hakuutarajia hivyo akaamini huyo ndiyo Mungu mwenyewe.
 
Sote tunafahamu na tunatambua kuwa uchawa (chawaism) upo katika nchi hii na katika ngazi tofauti za uongozi, lakini kitendo cha mtu kuonyesha uchawa uliopitiliza ni zaidi ya uzwazwa. Nilipomsikia Profesa Kabudi akisema kuwa Magufuli ni Mungu wake nilidhani ni masikhara. Kumbe Rais akikuteua kushika wadhaifa fulani, tayari anachukua nafasi ya Mungu wako?

Wakati RC Makonda akiongea kuhusu rushwa huko Arusha, amesema Dr Samia ni Mungu wake, hivyo hayuko tayari kumuumiza. Mambo yasiwe mengi, hebu msikilize wewe mwenyewe kwenye video hapo chini usije ukasema nimemuwekea maneno kinywani mwake.

View attachment 2976801
MAONI YANGU
Hata mtu uwe na njaa au uwe ni mwenye kujikomba kiasi gani, tafadhali sana usimfananishe mwanadamu na Mwenyezi Mungu, Bwana wa majeshi, Muumba wa mbingu na nchi. Hii ni kufuru iliyovuka mipaka. Ifike wakati tutumie akili zetu vizuri tuache kufananisha vitu visivyofanana hata kwa sababu tu ya kutetea matumbo yetu.

Nawasilisha.

Pia soma
.
RC Makonda: Rais Samia ameipendelea Arusha, amemtoa mwanae wa pekee na kumleta Arusha
unapotosha kwa maandishi, halafu halafu tena unaweka video ya muhusika inayobainisha ukweli dhidi ya upotoshaji wako wa kimaandishi :pedroP:
 
Wapi alipokuru? Kwanini umekurupuka kuanzisha uzi bila kusikiliza vizuri? Au una matatizo ya masikio na kuelewa? Huoni kwamba kuna koma na sentensi mbili zinatojigeemea hapo? Huoni amesema wazi hayupo tayari kumuumiza Mungu, lakini pia hayupo tayari kumkatisha Tamaa Daktari Samia Suluhu Hasssan kwa kumteua ukuu wa mkoa wa Arusha?

Kama una chuki zako binafsi basi ondoa hapa na usifikiri kuwa wote ni wajinga kama wewe
Wapi alitamka hayo maneno? Hayo maneno ameunganisha na yote yanamhusu Dr Suluhu Hassan. Acha kujitoa ufahamu na kupotosha watu. Kama hujui Kiswahili nenda shuleni ukasome.
 
Kuna chawa mmoja yeye alisema Mungu ni mwanamke sasa huyo Bashite labda baada ya kutafakari ameona mwanamke mwenyewe anayezungumziwa na yule chawa mwenzake ni huyo aliyempa cheo kwa sababu yeye ameona ametendewa muujiza ambao hakuutarajia hivyo akaamini huyo ndiyo Mungu mwenyewe.
Possibly! Hawa ndio wale wanaomuona mfalme Zumarid kama Mungu wao. So, akiona sketi yoyote inakatiza mbele yake, anakuwa amemuona Mungu. Nchi hii ina mambo ya kijinga sana.
 
Back
Top Bottom