tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 22,125
- 18,775
Sote tunafahamu na tunatambua kuwa uchawa (chawaism) upo katika nchi hii na katika ngazi tofauti za uongozi, lakini kitendo cha mtu kuonyesha uchawa uliopitiliza ni zaidi ya uzwazwa. Nilipomsikia Profesa Kabudi akisema kuwa Magufuli ni Mungu wake nilidhani ni masikhara. Kumbe Rais akikuteua kushika wadhaifa fulani, tayari anachukua nafasi ya Mungu wako?
Wakati RC Makonda akiongea kuhusu rushwa huko Arusha, amesema Dr Samia ni Mungu wake, hivyo hayuko tayari kumuumiza. Mambo yasiwe mengi, hebu msikilize wewe mwenyewe kwenye video hapo chini usije ukasema nimemuwekea maneno kinywani mwake.
MAONI YANGU
Hata mtu uwe na njaa au uwe ni mwenye kujikomba kiasi gani, tafadhali sana usimfananishe mwanadamu na Mwenyezi Mungu, Bwana wa majeshi, Muumba wa mbingu na nchi. Hii ni kufuru iliyovuka mipaka. Ifike wakati tutumie akili zetu vizuri tuache kufananisha vitu visivyofanana kwa sababu tu ya kutetea matumbo yetu.
Nawasilisha.
Pia soma
. RC Makonda: Rais Samia ameipendelea Arusha, amemtoa mwanae wa pekee na kumleta Arusha
Wakati RC Makonda akiongea kuhusu rushwa huko Arusha, amesema Dr Samia ni Mungu wake, hivyo hayuko tayari kumuumiza. Mambo yasiwe mengi, hebu msikilize wewe mwenyewe kwenye video hapo chini usije ukasema nimemuwekea maneno kinywani mwake.
MAONI YANGU
Hata mtu uwe na njaa au uwe ni mwenye kujikomba kiasi gani, tafadhali sana usimfananishe mwanadamu na Mwenyezi Mungu, Bwana wa majeshi, Muumba wa mbingu na nchi. Hii ni kufuru iliyovuka mipaka. Ifike wakati tutumie akili zetu vizuri tuache kufananisha vitu visivyofanana kwa sababu tu ya kutetea matumbo yetu.
Nawasilisha.
Pia soma
. RC Makonda: Rais Samia ameipendelea Arusha, amemtoa mwanae wa pekee na kumleta Arusha