Maisha yangu nimeyaharibu mwenyewe

SEHEMU YA SITA (6)

Tulipoishia…

Kipindi hicho matokeo walikua wanaandika majina kama sikosei (mtanirekebisha kama nimekosea) . So yule mtoto wa aunt alikua anajua namba ya shule ya BK SEC, nakumbuka ilikua S.0307/….. ndo namba ya mwanafunzi inafuata.
Nilipokea simu ya aunt na alikua akinipa taarifa za matokeo yangu

Tunaendelea…

Aunt alianza kwa kunisalimia “Hujambo” Mimi: Sijambo shikamoo aunt
Aunt: Nasikia matokeo yametoka
Mimi: (Kwa unyonge sana)ndio nimesikia
Aunt: Hongera mwanangu umefaulu

Baada ya hii kauli nilinyanyuka kitandani kwanza nikaweka bible pembeni,
Mimi: Umejuaje na nimepataje aunt
Aunt: una three (3) ya 24
Mimi: Asante Mungu…
Maongezi mengine yaliendelea pale na aunt na baada ya kunipongeza nilikata simu nikatoka nje speed kwenda kwa rafiki yangu.
Chaaap hao internet cafe… V alipata 3 ya 24 kama mimi na yule rafiki yetu mwimgine alipata 4 ya 26 ila combination zilibalance

Nilipokea simu kadhaa za hongera kutoka kwa Aunt wa Dar, Baba, Bro na wengineo wengi maana tayari hawakua na imani na mimi. Kwa upande wa marafiki zangu Mwanza kule hakuna hata mmoja aliyepata Div 1-3. Wengi walipata 4 wengine walipiga zero.
Nilimshukuru Mungu sana na nikakumbuka kauli ya V kuwa tukaze humu humu Arts.

Wakati nasubiri selection za shule, aunt alinipeleka kijijini kuna shule inaitwa KADEA, nilienda kufanya interview ya kujiunga na kidato cha 5. Na baada ya kuona matokeo yangu walisema nimechaguliwa kujiunga na shule hiyo.

Kwakweli sikutaka kabisa kusoma Bukoba tena, nilikua sijui naonaje mbaya zaidi nikasome bush… Noooh, nilijiambia mwenyewe.

Aunt bado hakunipa ruhusa kurudi Mwanza hivyo niliendelea kukaa pale pale kwake na maisha yaliendelea.

Selection zilitoka na nilipangiwa shule moja iko Mbeya Tukuyu huko ndani ndani (Sitoitaja jina). Sasa changamoto ikawa ni kumshawishi aunt niende Mbeya na sio Bukoba hapo.
Niliwasiliana na bro wa tabora boys, then yule bro mtoto wa aunt wa UDSM. Nikawapanga kabisaa wamwambie aunt faida za kusoma advance shule za serikali.
Maelezo yangu yalijificha kwenye sababu ya mikopo ya chuo. Kwamba nikisoma private chuo sitopata mkopo. Pia tulifuatilia ufaulu wa shule ya mbeya na hiyo KADEA ikaonekana ile shule ya Mbeya wanafaulu sana.

Baada ya siku kadhaa aunt alikubali na mchakato ukaanza. Form 5 nilichaguliwa mchepuo wa HGK.

Wakati wote niliokaa bukoba, nilikua nikipata nafasi naenda kijijini pale kwenye kaburi la Mama kumsalimia. Hata kabla ya kuondoka Bukoba nilienda tena pale alipolala mama.

Kipindi nimemaliza form 4 Aunt alinipa hela nikafungue Acc bank. Hivyo acc yangu ya kwanza ya Bank nilianza kuitumi 2010, ilikua CRDB.

Aunt wa Dar alinipigia na kuniuliza nini nahitaji ili viniwezeshe shuleni, Nilimwambia vitabu.

Niliondoka Bukoba kwenda Dar lakini aunt safari hii aliniruhusu nipite Mwanza kumsalimia Baba na alinipa siku 2 tu then niende Dar

Ilikua 2011 tayari na nilirudi Mwanza kwa mbwembwe sana, safari nzima nawaza namna ntamwona Crush wangu wa tangu utotoni.

Niliwasili Mwanza mapema tu na shughuli kubwa ilikua ni kutembelea marafiki zangu. Jioni yake nilionana na Crush wangu ( Clara tumwite hivyo) na tulikubalina siku nnayoondoka nikalale Lodge pale Nyegezi na yeye angetoka kwao ili tulale wote. Nami nilikubali ukizingatia nilikua na visent kwenye Acc yangu.

Mzee alifurahi sana na hakuna mkali tena hadi leo hii. Kesho mchana nilinunua simu mpya ya mchina nakumbuka niliweka ringtone nyimbo ya 20%.
Jioni nilijiandaa vyema na safari kwenda Nyegezi ikaanza, tulipanga kukutana na Clara maeneo ya Ghana then tuondoke wote na ilikua hivyo.

Nilimpend Clara ila Jane alikua mzuri sana. Basi tulipata Lodge pale Nyegezi na tukaenda kununua vyakula tukarudi ndani.
Clara alikua Bikra kabisaaa na hiyo siku ndo nilitoa usichana wake.
Alimia sana ila hatukua na namna maana alikua tayari kwa kile kilichokua kinaendelea.

Asubuhi niliondoka na Clara alisubiri hadi bus liondoke ndo akaondoka ila alikua na maumivu makali mno na hata tembea yake haikua kawaida.
Wakati niko njiani tulikua tukichat na alinijulisha kuwa anaumwa sana, amepata hadi homa. Nilimpa pole nyingi na kumwambia ajikaze home wasijue.

Kwa upande wa Jane baada ya kumaliza form 4 alienda Dar kwa mpenzi wake baadae akaenda mwanza kwa dada yake (niliambiwa na mwenzake) lakini taarifa niliyokuwa nayo wakati naenda Advance ni kuwa Jane tayari ana mimba kubwa tu.


TUTAENDELEA…..

Kama bado tuko active niandike epsode moja ya mwisho kwa leo

NB: This is my true story, sijacopy mahali… Nimeileta hapa maana huko mbeleni nahitaji ushauri wenu muhimu
Tupo active mkuu weka episode hiyo
 
Nakupa elimu ndogo kabisa, Ni baba yenu ndie alikuwa anatafuta hela za kuwalipia ada shuleni, nguo, chakula, n.k. mama yenu alikuwa anapewa ila mkimuona anavyowalipia / kuwapa mnadhani ni zake.

Nani kama mama ni misemo ya watoto / vijana ambao bado hawana familia zao kujua mfumo kamili wa jinsi mambo yanavyokwenda
Nimekuwa nikitoa pesa kwa mwanangu ili apewe ajab siku nakanwa kuwa sijatoa kitu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kwanini baba asiwape mwenyewe hivyo vitu kama nguo au aseme nitampa mama yenu atawapa? Mambo hayo ndio wababa hua mnakosea halafu baadae watoto wakilipa fadhila kwa mama mnaumia.
Ni watoto wajinga tu ndio huvuka hiyo hatua bila kujua kilichokua kikiendelea
 
SEHEMU YA SABA (7)

Tulipoishia…


Asubuhi niliondoka na Clara alisubiri hadi bus liondoke ndo akaondoka ila alikua na maumivu makali mno na hata tembea yake haikua kawaida.
Wakati niko njiani tulikua tukichat na alinijulisha kuwa anaumwa sana, amepata hadi homa. Nilimpa pole nyingi na kumwambia ajikaze home wasijue.

Kwa upande wa Jane baada ya kumaliza form 4 alienda Dar kwa mpenzi wake baadae akaenda mwanza kwa dada yake (niliambiwa na mwenzake) lakini taarifa niliyokuwa nayo wakati naenda Advance ni kuwa Jane tayari ana mimba kubwa tu.

Tunaendelea….


Nilifika dar majira ya saa tano usiku, na hii ndo ilikua mara yangu ya kwanza kuja Dar. Aunt alituma mtu aje kunipokea na joto ndo lilinipokea vizuri.

Aunt wa Dar ana maisha yake mazuri tu na sitotaka kuongelea chochote kuhusu maisha ya kwa Aunt ila kwa ufupi sana ni maisha poa na kila mtu na time zake, mtakutana jioni muda wa kuangalia habari na kula labda

Kesho yake kuna Dada yangu alinipeleka Mwenge na Kariakoo kununua vitu vya Shule. Nilikaa Dar kama siku 4 then safari ya Mbey ikaanza.
Wakati natoka Dar nilikua na kila kitu cha shuleni. Aunt wa Dar alininunulia ( aunt wa Dar tumwite B. Mkubwa ili kutofautisha na wa Bukoba)
Account yangu ya CRDB iliwekwa laki 2 na B. mkubwa kama Pocket money ya shule then nikapewa nauli na pesa ya kula njiani. Nilinunuliwa counter Book 12, vitabu 6 na kila hitaji nilipewa. Mzee mwanza pia alinipa hela ila nilikula bata yote nilivyofika Dar ikiwemo kununua nguo mpya.

Safari ya Mbeya ilikua safi tu na nilifika Mbeya Tukuyu majira ya saa nne na nusu hivi usiku. Wakati niko njiani kuna mbaba nilikaa nae alikua ni doctor huko Kyela na alitokea kunikubali sana na tulibadilishana namba.

Changamoto ilikuja pale nilipofika Tukuyu na kujikuta nimebaki na Cash kama elfu 17 tu. Sasa nikauliza bank iko wapi, Dreva tax alinijibu “huku hakuna CRDB, kuwa linakuja gari (Mobile Bank) sijui kama niko sahihi linavyoitwa. Hilo gari huwa linakuja siku ya jumatatu tu na linatoa huduma na kuondoka”. Asee nilichanganyikiwa na sikuwa na mwenyeji yoyote Mbeya kwa wakati huo. Niliomba dreva Tax anipeleke lodge yoyote ya bei ndogo. Jamaa alinifanyia uhuni, Lodge ilikua sehemu ya kutembea kwa dak 2 tu ila jamaa akanizungusha njia ya mbali na akanipela hapo Lodge nikampa buku 3. Pale Lodge nililipa elfu 10 nikalala huku nikiwaza asubuhi naendaje Mbeya mjini maana nilikua mgeni kabisa na mfukoni nna kama elfu 4 tu.

Niliamka asubuhi nikajiandaa then nikaenda mapokezi nikamwomba jamaa aniangalizie mizigo yangu.
Nilipanda costa za Tukuyu - Mbeya nauli ilikua buku 3 kama sikosei. Safari ikaanza nami macho yangu yote yalikua barabarani nikijisemea ntakapoona ATM ya CRDB basi nashukua.
Nilishuka Mwanjelwa pale baada ya kuona ATM then nikatoa pesa kama laki hivi. Nilinunua godoro, blanketi na koti jeusi. Ile shule tulikua tunavaa full black… Yani shati white, suruali black na koti Black… suit kabisa yani.

Nikarudi Tukuyu na kubeba vitu vyangu tayari kwenda shule. Yule dreva tax nilichukua namba yake na tulikuja kuwa washkaji baadae. Alinipeleka hadi stand ya kwenda huko ndani ndani (Mbambo, Itete hadi shuleni penyewe)
Sasa pake stand nilikutana na wanafunzi kibao wanaoenda shuleni ila cha kushangaza usafiri ulikua Canter na sio mabasi… Yani mnaning’inia huko juu kwenye canter.. wanawake ndo wanakaa chini. Asee niliishiwa nguvu baada ya kusikia hivyo.
Canter inajaza balaa na mizigo ni mingi mnoo kwani watu huja Tukuyu kununua mahitaji mengi na wengi ni wafanyabiashara kule kijijini.

Safari ilianza kama baada ya masaa mawili hivi na wanafunzi tulikua tunapiga story nyingi mnoo na swali kubwa ilikua ni kuulizana we umetokea wapi. Peke yangu ndo nilikua natoka Bukoba.
Ile safari ilikua ya mateso sana. Barabara ni vumbi, madaraja ya mbao alafu barabara ina milima na kona balaa (watu wa Mbeya hususani Tukuyu wananielewa vizuri hapa)

Ilikua Gari ikilalia upande wetu nasali sana maana ukiachia zile bomba ndo uko chini hivyo
Nilianza kujuta kwanini sikusoma Bukoba tu. Baada ya masaa matatu na nusu hivi tulifika shuleni… Asee nilihisi kuna kitu kimenikaba kooni kama nataka kulia kama nimebanwa (hii hali mnaijua wengi) kwa ufupi ningekua mtoto ningelia
Shule ilikua mwisho kabisa. Yani kata ya mwisho kabisaa baada ya hapo kuna Mlima Living stone so hakuna namna utaenda kokote.

Tulipokelewa shuleni tukaonyeshwa mabweni then tukaenda kula mtaani siku hiyo maana tulifika watu washapewa chakula cha jioni shuleni pale.
Nilifanikiwa kupata marafiki wengi na maisha ya kuishi mbali na wazazi yakaanza rasmi


Tuishie hapa kwa leo

See you kesho
 
SEHEMU YA SITA (6)

Tulipoishia…

Kipindi hicho matokeo walikua wanaandika majina kama sikosei (mtanirekebisha kama nimekosea) . So yule mtoto wa aunt alikua anajua namba ya shule ya BK SEC, nakumbuka ilikua S.0307/….. ndo namba ya mwanafunzi inafuata.
Nilipokea simu ya aunt na alikua akinipa taarifa za matokeo yangu

Tunaendelea…

Aunt alianza kwa kunisalimia “Hujambo” Mimi: Sijambo shikamoo aunt
Aunt: Nasikia matokeo yametoka
Mimi: (Kwa unyonge sana)ndio nimesikia
Aunt: Hongera mwanangu umefaulu

Baada ya hii kauli nilinyanyuka kitandani kwanza nikaweka bible pembeni,
Mimi: Umejuaje na nimepataje aunt
Aunt: una three (3) ya 24
Mimi: Asante Mungu…
Maongezi mengine yaliendelea pale na aunt na baada ya kunipongeza nilikata simu nikatoka nje speed kwenda kwa rafiki yangu.
Chaaap hao internet cafe… V alipata 3 ya 24 kama mimi na yule rafiki yetu mwimgine alipata 4 ya 26 ila combination zilibalance

Nilipokea simu kadhaa za hongera kutoka kwa Aunt wa Dar, Baba, Bro na wengineo wengi maana tayari hawakua na imani na mimi. Kwa upande wa marafiki zangu Mwanza kule hakuna hata mmoja aliyepata Div 1-3. Wengi walipata 4 wengine walipiga zero.
Nilimshukuru Mungu sana na nikakumbuka kauli ya V kuwa tukaze humu humu Arts.

Wakati nasubiri selection za shule, aunt alinipeleka kijijini kuna shule inaitwa KADEA, nilienda kufanya interview ya kujiunga na kidato cha 5. Na baada ya kuona matokeo yangu walisema nimechaguliwa kujiunga na shule hiyo.

Kwakweli sikutaka kabisa kusoma Bukoba tena, nilikua sijui naonaje mbaya zaidi nikasome bush… Noooh, nilijiambia mwenyewe.

Aunt bado hakunipa ruhusa kurudi Mwanza hivyo niliendelea kukaa pale pale kwake na maisha yaliendelea.

Selection zilitoka na nilipangiwa shule moja iko Mbeya Tukuyu huko ndani ndani (Sitoitaja jina). Sasa changamoto ikawa ni kumshawishi aunt niende Mbeya na sio Bukoba hapo.
Niliwasiliana na bro wa tabora boys, then yule bro mtoto wa aunt wa UDSM. Nikawapanga kabisaa wamwambie aunt faida za kusoma advance shule za serikali.
Maelezo yangu yalijificha kwenye sababu ya mikopo ya chuo. Kwamba nikisoma private chuo sitopata mkopo. Pia tulifuatilia ufaulu wa shule ya mbeya na hiyo KADEA ikaonekana ile shule ya Mbeya wanafaulu sana.

Baada ya siku kadhaa aunt alikubali na mchakato ukaanza. Form 5 nilichaguliwa mchepuo wa HGK.

Wakati wote niliokaa bukoba, nilikua nikipata nafasi naenda kijijini pale kwenye kaburi la Mama kumsalimia. Hata kabla ya kuondoka Bukoba nilienda tena pale alipolala mama.

Kipindi nimemaliza form 4 Aunt alinipa hela nikafungue Acc bank. Hivyo acc yangu ya kwanza ya Bank nilianza kuitumi 2010, ilikua CRDB.

Aunt wa Dar alinipigia na kuniuliza nini nahitaji ili viniwezeshe shuleni, Nilimwambia vitabu.

Niliondoka Bukoba kwenda Dar lakini aunt safari hii aliniruhusu nipite Mwanza kumsalimia Baba na alinipa siku 2 tu then niende Dar

Ilikua 2011 tayari na nilirudi Mwanza kwa mbwembwe sana, safari nzima nawaza namna ntamwona Crush wangu wa tangu utotoni.

Niliwasili Mwanza mapema tu na shughuli kubwa ilikua ni kutembelea marafiki zangu. Jioni yake nilionana na Crush wangu ( Clara tumwite hivyo) na tulikubalina siku nnayoondoka nikalale Lodge pale Nyegezi na yeye angetoka kwao ili tulale wote. Nami nilikubali ukizingatia nilikua na visent kwenye Acc yangu.

Mzee alifurahi sana na hakuna mkali tena hadi leo hii. Kesho mchana nilinunua simu mpya ya mchina nakumbuka niliweka ringtone nyimbo ya 20%.
Jioni nilijiandaa vyema na safari kwenda Nyegezi ikaanza, tulipanga kukutana na Clara maeneo ya Ghana then tuondoke wote na ilikua hivyo.

Nilimpend Clara ila Jane alikua mzuri sana. Basi tulipata Lodge pale Nyegezi na tukaenda kununua vyakula tukarudi ndani.
Clara alikua Bikra kabisaaa na hiyo siku ndo nilitoa usichana wake.
Alimia sana ila hatukua na namna maana alikua tayari kwa kile kilichokua kinaendelea.

Asubuhi niliondoka na Clara alisubiri hadi bus liondoke ndo akaondoka ila alikua na maumivu makali mno na hata tembea yake haikua kawaida.
Wakati niko njiani tulikua tukichat na alinijulisha kuwa anaumwa sana, amepata hadi homa. Nilimpa pole nyingi na kumwambia ajikaze home wasijue.

Kwa upande wa Jane baada ya kumaliza form 4 alienda Dar kwa mpenzi wake baadae akaenda mwanza kwa dada yake (niliambiwa na mwenzake) lakini taarifa niliyokuwa nayo wakati naenda Advance ni kuwa Jane tayari ana mimba kubwa tu.


TUTAENDELEA…..

Kama bado tuko active niandike epsode moja ya mwisho kwa leo

NB: This is my true story, sijacopy mahali… Nimeileta hapa maana huko mbeleni nahitaji ushauri wenu muhimu
Ww jamaa mbona buyekera napajua sana nahistoria napo ...tukuyu pia napajua mwaka 2009 nilikuwa fom six huko

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom