Uchaguzi 2020 Magufuli aliwasema na kuwadhalilisha watu barabarani, leo naye anasemwa vibaya barabarani huko huko

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
9,238
33,979
Pamoja na mapungufu ya awamu zilizopita kiutawala, lakini awamu hii ya tano haikufuata kabisa utawala Bora.

Watu wamekuwa wakifokewa hovyo hadharani, watu wamekuwa wakidhalilishwa hovyo hadharani, watendaji wa Serikali wamefukuzwa kazi mabarabarani, kwa kile kinachoitwa kutumbuliwa.

Wafanyakazi waliambiwa hatawaongeza Mishahara, madaraja Wala increment kwa sababu anajenga miundo mbinu na kuwaambia kuwa wafanyakazi kwanza sio wengi sana nchi hii,yeye anashughulikia miundombinu kwa ajili ya Watanzania wote. (Sasa hapa sijui watangulizi wake walikosea kuwapandisha Mishahara na wakati huohuo kuendelea kujenga miundombinu?)

Aliona kwamba wafanyakazi ni wachache kura zao hata wakimnyima hatoshindwa Uchaguzi wakati hali halisi ni kwamba kila mfanyakazi mmoja wa Tanzania ana watu kumi wanaohitaji msaada wake na wanajua machungu yake.

Sasa umefika wakati na yeye anasemwa hadharani. Tena anasemwa vibaya,mbele ya wananchi, kwa maneno ambayo nadhani hapendi kuyasikia, wapambe wake hawapendi kuyasikia. Yanamchoma, yanamkera, yanamchafua na yanamuaibisha.

Tundu Lissu Ni Mtundu kwelikweli, anapohoji habari za Ben Sanane hadharani anamuumiza sana, anapohoji kuhusu waliompiga risasi anamchoma sana Mzee ambae hajawahi kusemwa hadharani kwa miaka mitano.

Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa na Mzee Kikwete walipojaribu kumsema walidhalilishwa sana kwa kuambiwa Wazee hao waache kuwashwawashwa. Akina Kinana, Membe na akina Makamba walipojaribu kumsema faraghani walidukuliwa na maneno yao yakawekwa hadharani Aibu ikawapata.

Leo hii Tundu Lissu anamsema hadharani asiyesemwa, kiasi cha kuwa mpole kuliko mtoto mchanga. Lissu anamsema kwelikweli tena kwa nguvu, tena mbele ya halaiki na mbele ya makamera na waandishi.

Yale yaliyokua yanaongelewa kwa kificho na kwa uoga, Lissu anayasema waziwazi. Kwa kifupi “mzee baba” ana hali ngumu. Hakufuata utawala wa sheria, sasa anaonja joto la jiwe.

Watanzania wenzangu, mtu huyu msifanye makosa ya kumrudisha tena madarakani, kwani awamu hii ni ya mwisho kuja kuomba kura. Akirudi hana cha kupoteza, mateso mliyopata awamu yake ya kwanza yatakuwa mara mbili na hayatakuwa na kikomo. Huyu hana tabia za kujuta kama Mkapa na Kikwete, hajali, mjivuni.

Kura yangu nitampa Tundu Lissu, jamaa zangu wameniahidi watampa kura Lissu, nakuomba na wewe mpe kura yako Lissu ajenge utawala wa sheria. Utawala Bora wenye kuheshimu utu wa kila mtu.
Uhuru, Hali na maendeleo ya watu.

Chagua Diwani CHADEMA, Mbunge CHADEMA na Rais Lissu.
 
CV yake haitabadilika hata kama ni u Rais wa miaka mitano lakini alishawahi kuwa Rais wa JMT. Mzee mpishe Tundu Lissu arudishe heshima na hadhi ya cheo cha Rais.
Tatizo sio upinzani, Tatizo hamna mgombea sahihi

Magufuli ataongoza tena
 
Mheshimiwa badala ya kuifanya ofisi ya Rais kama taasisi imara ya uongozi wa nchi yetu, yeye kwa kujua ama pasipo kujua kajikuta anaigeuza kuwa ni kama "private office" yake, yenye maslahi binafsi. Yeye akawa ndiye mjuaji wa kila kitu.

Kusema ukweli ampishe tu TAL ili arudishe hadhi ya ofisi hii nyeti ya uongozi wa Taifa letu ktk misingi ile ya awali ya Mwl. Nyerere. Kiu ya kila Mtanzania kwa sasa ni Uhuru, Haki na Maendeleo kwa watu wote, na wala si vinginevyo.
 
Lissu anajisumbua tu!

Yani utundu wa huyo mtu wenu hata sioni.

Hushindi urais sasa huo utundu wako utakusaidia nini?
 
Lisu anajisumbua tu,!

Yani utundu wa huyo mtu wenu hata sioni.

Hushindi urais sasa huo utundu wako utakusaidia nini?

Angalau ana uthubutu wa kuyasema mabaya ya Rais, siyo wale wa kusifu na kuabudu kwa mapambio, nyimbo na vigelegele.

Kwangu Mimi, najua Lisu hatashinda, lakini kwa Jambo Hilo tu la kumwambia mkuli mabaya yake, yanaweza kumfanya ajitathimi(kama ana akili hiyo) na akabadilisha naadhi ya mienendo na mwisho kulifaidisha zaidi taifa letu.
 
Angalau ana uthubutu wa kuyasema mabaya ya Rais, siyo wale wa kusifu na kuabudu kwa mapambio, nyimbo na vigelegele.

Kwangu Mimi, najua Lisu hatashinda, lakini kwa Jambo Hilo tu la kumwambia mkuli mabaya yake, yanaweza kumfanya ajitathimi(kama ana akili hiyo) na akabadilisha naadhi ya mienendo na mwisho kulifaidisha zaidi taifa letu.
Kwa miaka mitano tuliishi kwa amri ya “usilitaje bure jina la yesu wa Chato” na wengine wako jela kwa kuvunja amri hii. Tundu Lissu ameweza kututoa kwenye hii dhana.
 
Lisu anajisumbua tu,!

Yani utundu wa huyo mtu wenu hata sioni.

Hushindi urais sasa huo utundu wako utakusaidia nini?
Maneno ya kipumbavu kama haya ndiyo yanayomgharimu bwana huyu sasa hivi, alikuwa mjuvi wa kila kitu, dharau, maneno machafu, kufukuzwa watu kwa kejeli, aliwasema watu bila staha leo yanamkumba.

Dharau kama hizi alikuwa nazo Daudi Albert Bashite leo anazomewa kila mahala kipindi yupo madarakani alipenda kuwa mubashara akitamba lakini leo anaziogopa kamera na watu wanamtafuta wajue hivi saa yu hali gani.

Yawezekana hujui historia KANU ilikuwa na dharau zaidi ya hizi sasa hivi chama kipo makumbusho.

Unamchukulia poa Lissu na akati alipotamka kuwa akiingia madarakani pamba haitakopwa siku tatu baadae Magufuli akailazimisha benki fulani itoe bilion 2 ili kulipa wakulima ambao hawajalipwa na sasa wanalipwa chezea Lissu weye.
 
Pamoja na mapungufu ya awamu zilizopita kiutawala, lakini awamu hii ya tano haikufuata kabisa utawala Bora.

Watu wamekuwa wakifokewa hovyo hadharani, watu wamekuwa wakidhalilishwa hovyo hadharani, watendaji wa Serikali wamefukuzwa kazi mabarabarani, kwa kile kinachoitwa kutumbuliwa...
Usinifokee ni mtazamo wako wewe na familiy yako utamchagua lisu,mm namuchagua magufuri kwakua nimejionea kwa macho kazi kubwa alizo fanya na kwa mda mfupi,hayo mambo ya uhuru sielewi kabisa kwamba kuna rais atakuja kuendesha inchi bila utaratibu? Mungu mwenyewe katuwekea utaratibu tuishi kwa kuzifuata amri 10 wewe utataka uhuru upi kwamba ukikosea wakuchekee tu au?

Nikukumbushe tu kipindi cha nyuma majambazi walitamba sana mabasi yalitekwa kila mara, umeme ulikatika ukawa wa mgao watumishi wa uma walijifanya miungu watu, ile kauli iliyojizolea umaarufu kwa baadhi ya watu ya unanijua mimi ninani imefutika tumeeshimiana wote hayo ni baadhi tu.
 
Acha kufoka!

Huyo mtu wako aliekuja na beberu wake Masterdam hafiki popote nadhani mapikezi anayopata huko anakopita yatakuwa yanampa ujumbe

Ukweli ni kwamba Lisu havuki 20% ya kura sasa huo utundu wake unamsidia kitu gani?

Alafu huyo Makonda ni wapi kazomewa? Hicho cheo alichokuwa nacho aliteuliwa na mamlaka iliyomteua imemtoa na mwakani baada ya Magu kuapishwa anaweza kuteuliwa hapohapo tena au kwenye mafasi ya juu zaidi na ukabaki huna la kusema zaidi ya kukejeli tu huku wenzio maisha yanasonga!

Mwambie Lisu kushinda urais kunahitaji kupitia taasisi strong na mikakati imara,
Mwambie kabisa kushinda urais siyo sawa na kushinda u monitor wa darasa la nne B
 
Erythrocyte haja like huu uzi!!?
itakuwa hajaamka bado si kawaida yake
kuchelewa ku-fuel na kupiga gia nyuzi za mlengo huu....
 
Hahahaa, yale matusi ya kilaza na lipumbavu yanamrudia mwenyewe. Katika historia ya nchi tangu Uhuru, wajukuu zetu watamsoma na kumshangaa sana huyu rais kwa kutoheshimu utawala wa sheria, na matumizi ya mabavu, na kutembea na vikosi vya majeshi vya kumlinda ndani ya nchi yenye amani. Ukifanya uovu unakuwa mwoga wa kulipizwa kisasi.
 
Pamoja na mapungufu ya awamu zilizopita kiutawala, lakini awamu hii ya tano haikufuata kabisa utawala Bora.

Watu wamekuwa wakifokewa hovyo hadharani, watu wamekuwa wakidhalilishwa hovyo hadharani, watendaji wa Serikali wamefukuzwa kazi mabarabarani, kwa kile kinachoitwa kutumbuliwa...
Alijiona yeye ndio kila kitu alisahau kuwa 2015 alipitishwa na tume na wasio wananchi
 
Hahahaa, yale matusi ya kilaza na lipumbavu yanamrudia mwenyewe. Katika historia ya nchi tangu Uhuru, wajukuu zetu watamsoma na kumshangaa sana huyu rais kwa kutoheshimu utawala wa sheria, na matumizi ya mabavu, na kutembea na vikosi vya majeshi vya kumlinda ndani ya nchi yenye amani. Ukifanya uovu unakuwa mwoga wa kulipizwa kisasi.
Hayo majeshi yanayomlinda ni ya nchi gani?Mbona wanabeba bunduki za kivita tofauti na walinzi wa Marais waliomtangulia?Je,ni miongoni mwa majeshi yetu ya akiba?
 
Back
Top Bottom