Maarifa ya Kiasili/kienyeji ktk ufugaji

Malila

JF-Expert Member
Dec 22, 2007
5,156
4,684
Kwa wafugaji wa kienyeji wa wanyama na ndege huko vijijini kwetu, kuna vitu au maarifa ya kienyeji ambayo huwa wanatumia, naomba tuyajadili na kujulishana pia tuonyeshane kama kweli yanafanya kazi. Na kama ni muhimu kuyaendeleza kwa manufaa yetu.

Mfano; Kuku mgeni akiletwa nyumbani, nimekuwa nikiona watu wakinyoa manyoya kisha kuyachoma motoni, wanamzungusha kuku na baadae wanamwachia. Mkulima huamini kuwa kwa kufanya hivyo kuku hawezi kutoroka. Juzi nimeipata mpya, eti vitoto vya bata ili visife, wenyewe huwa wanavivuta shingo mapema,wanaamini kwamba vinapona vyote.

Vitu ni vingi vinafanyika huko vijijini, ukikijua tupa hapa ili tujadili.
 
Kwa wafugaji wa kienyeji wa wanyama na ndege huko vijijini kwetu,kuna vitu au maarifa ya kienyeji ambayo huwa wanatumia,naomba tuyajadili na kujulishana,pia tuonyeshane kama kweli yanafanya kazi. Na kama ni muhimu kuyaendeleza kwa manufaa yetu. Mfano; Kuku mgeni akiletwa nyumbani, nimekuwa nikiona watu wakinyoa manyoya kisha kuyachoma motoni, wanamzungusha kuku na baadae wanamwachia. Mkulima huamini kuwa kwa kufanya hivyo kuku hawezi kutoroka. Juzi nimeipata mpya, eti vitoto vya bata ili visife, wenyewe huwa wanavivuta shingo mapema,wanaamini kwamba vinapona vyote. Vitu ni vingi vinafanyika huko vijijini, ukikijua tupa hapa ili tujadili.
Malila kwa hilo la moto sijalisikia bado, ila hili la bata kama utakumbuka mwaka jana niliwahi kuandika hapa nikiomba msaada wa dawa, bata wangu wadogo walipofikisha wiki 2 wakaanza kuanguka miguu juu wanakufa. Nilishauriwa dawa nyingi hapa including OTC plus, lakini waliendelea kufa nilipoteza vifaranga watano. kuna siku nikapita pale Ukonga magereza kuna mzee mmoja amefuga bata wengi sana, nikamfuata akaniambia kila bata wakifikisha wiki moja unawashika huku shingo yake ikiwa imelala katika vidole viwili vya mkono mmoja na vidole viwili yaani gumba na hiki cha shahada unavuta shingo taratibu hadi usikie mlio kama kijiti kikavu kinavunjika. Nikafanya hivyo kwa wale waliobaki, hata wale waliokuwa hoi wakapona na wakaendelea kuzaliana huku nikifanya hivyo kila baada ya vifaranga kutimiza wiki moja. Sijajua kama wakiwa wengi mtu atafanyaje maana zoezi ni kubwa na gumu. KITAALAMU SIJUI NINI KINAFANYIKA NAJUA TU BATA WALIPONA
 
haya mambo ya imani magumu sana

Kuna mambo mengine ni mpaka uwe umefanya ndio unaweza kuamini. Ni nini huwa kinafanywa kwa mnyama mpaka asahau kwao,kumbuka ni just few meters toka ulikomnunua? Kuna watu wanaweza kufanya maarifa hayo. Tuachane na hayo. Kuna mzee mmoja yy, huwa anachukua majani fulani anayatandaza kuzunguka zizi,siafu hawapiti hapo. Kumbe sisi wafugaji wa mjini tunaingia gharama kubwa kununua dawa na ushauri kibao. Ujanja huu wa kutumia malighafi na rasilimali zilizopo ktk mazingira yetu ndio ninao utaka.
 
hiyo ya kumnyonyoa kuku manyoya na kuyachoma ni dodoma.

1. sis kwetu ukinunua ng'ombe wakati wa kumuingiza zizini kwa mara ya kwanza ni lazima aingie kinyumenyume asipoingia hivyo hataweza kuzaa na pia anaweza kuleta mikosi nyumbani

2. babu alikuwa akimpiga kila ng'ombe kofi kabla ya kuingia zizini

3. Huwa hatununui mbuzi/ng'ombe wa kufuga kutoka kwa wagogo.. kwakuwa huwa wanawafanyia mazingara kabla ya kuwauza ili wasizae

4. kuna kijijini ilikuwa ukinunua mnyama ni lazima atoroke na arudi kwao
 
hiyo ya kumnyonyoa kuku manyoya na kuyachoma ni dodoma.

1. sis kwetu ukinunua ng'ombe wakati wa kumuingiza zizini kwa mara ya kwanza ni lazima aingie kinyumenyume asipoingia hivyo hataweza kuzaa na pia anaweza kuleta mikosi nyumbani

2. babu alikuwa akimpiga kila ng'ombe kofi kabla ya kuingia zizini

3. Huwa hatununui mbuzi/ng'ombe wa kufuga kutoka kwa wagogo.. kwakuwa huwa wanawafanyia mazingara kabla ya kuwauza ili wasizae

4. kuna kijijini ilikuwa ukinunua mnyama ni lazima atoroke na arudi kwao

Hii hapo pekundu nimekutana nayo Vingunguti, pale unaweza nunua mbuzi na asizae kabisa. Tumejaribu mara kadhaa,ndio tukapewa siri hiyo kuwa hawa jamaa wa Dom wanafanyizia mbuzi wao.

Hii ya kuingia kinyumenyume inafanya kazi mpaka leo?

Kule home kuna babu alikuwa na uwezo wa kuwazuia ng`ombe wasile mahindi ya mtu. Swali liko pale pale, wanafanyaje hawa wazee?
 
hahaha mmenifurahisha na kuna ile ukimchinja kuku koromeo ama ile wind pipe unarusha inase kwenye ukuta wa jiko kule jikoni................nilikutwa ikifanywa sana maene ya Dabaga kule wilaya ya Kilolo ......mpaka kesho sijawahi jua ni kwa nini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom