Kwa katiba hii ya ACT-Wazalendo, uenyekiti wa Mama Mghwira mashakani

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,272
47,276
Katiba ya ACT-Wazalendo sura ya 4 ibara 29 inamtaka kiongozi atakayeshindwa uchaguzi wa kiserikali lazima ajieleze, akishindwa anaondolewa kwenye nafasi yake.


xiv) Endapo Kiongozi wa Chama atashindwa katika uchaguzi wowote wa kiserikali, Halmashauri Kuu ya Taifa itabidi ikutane katika kipindi kisichozidi miezi sita tangu kufanyika kwa uchaguzi huo ili kujadili mazingira ya kushindwa kwake na kupiga kura ya siri ya kuamua kama Kiongozi wa Chama anastahili kuendelea na nafasi yake au la. Kiongozi wa Chama ataendelea na nafasi yake endapo zaidi ya nusu ya wajumbe watapiga kura ya kuwa na imani naye.
 
Ni Kweli Katiba Inasema kabla ya Tarehe 25 April 2016 Zoezi hilo lifanyike
 
Kwa mujibu wa sura ya 4 ibara ya 29 inamtaka kiongozi atakayeshindwa uchaguzi wa kiserikali ajieleze au avuliwe cheo chake.


xiv)Endapo Kiongozi wa Chama atashindwa katika uchaguzi wowote wa kiserikali, Halmashauri Kuu ya Taifa itabidi ikutane katika kipindi kisichozidi miezi sita tangu kufanyika kwa uchaguzi huo ili kujadili mazingira ya kushindwa kwake na kupiga kura ya siri ya kuamua kama Kiongozi wa Chama anastahili kuendelea na nafasi yake au la. Kiongozi wa Chama ataendelea na nafasi yake endapo zaidi ya nusu ya wajumbe watapiga kura ya kuwa na imani naye.
 
Tatizo ni nini?

Huo ndiyo wajibu wa wanachama/viongozi kama walivyokubaliana kwenye katiba.

Kuwa mwanachama ni hiari yako lakini kuendelea kuwa mwanachama lazima ukubaliane na Taratibu, Kanuni na Katiba ya chama.
 
Hapa zitto alikuwa anajisafishia njia ili yeye awe mwenyekiti.

Na akishakuwa mwenyekiti atafuta vipengele vinatakavyombana.

Tunaomba tuone katiba nzima.
 
Katiba ya ACT-Wazalendo sura ya 4 ibara 29 inamtaka kiongozi atakayeshindwa uchaguzi wa kiserikali lazima ajieleze, akishindwa anaondolewa kwenye nafasi yake.

nasikia alikaimu nafasi ya kiongozi mkuu wa chama kwa mda, sijui zzk ashampokonyaa??
 
Mama anna amejitahidi sana, she will make a great leader, with meager resources of act, and a brand new party, less than a year old , she has done what is required, creating awareness. Today act is known in all corners of the country. Viva dada anna
 
Tatizo ni nini?

Huo ndiyo wajibu wa wanachama/viongozi kama walivyokubaliana kwenye katiba.

Kuwa mwanachama ni hiari yako lakini kuendelea kuwa mwanachama lazima ukubaliane na Taratibu, Kanuni na Katiba ya chama.

Mkuu tatizo ni pale Prof Kitila Mkumbo, ambaye ndiye brain of the party anapoanza kutathmini majirani zake wakati nyumba yake inateketea kwa moto. Sasa lini hasa ataanza kukifanyia kazi kipengelele tajwa??
 
hiyo inamaanisha kana angekuwa Zitto, yaani Kiongozi wa Chama. hsisemi Mwenyekiti.
 
Katiba ya ACT-Wazalendo sura ya 4 ibara 29 inamtaka kiongozi atakayeshindwa uchaguzi wa kiserikali lazima ajieleze, akishindwa anaondolewa kwenye nafasi yake.

Lazima kamati kuu ikae. ACT wataonesha utofauti endapo watasimamia katiba yao ipasavyo
 
maanaake sasa wakae wawajadili wabunge pia na madiwani katiba ya chama changu ngumu sanaa
 
Hapa zitto alikuwa anajisafishia njia ili yeye awe mwenyekiti.

Na akishakuwa mwenyekiti atafuta vipengele vinatakavyombana.

Tunaomba tuone katiba nzima.

yeye ni kiongozi mkuu wa chama zaidi ya mwenyekiti. uenyekiti wa nn? ila naanza kuona kwa nini kitila alikimbia fomu ya urais
 
Hizi ni akili za zito tu,alishasema atamuachia ukiongozi mkuu wa chama mtu atakayegombe urais.Sasa alisema hivo akijua katiba itamchomoa mama ana mapema maana lazima ashindwe uchaguzi.
 
for any neutral, ni dhahiri kabisa kuwa when it comes to hekima ya kiuongozi yule mama yupo many miles mbele ya Zitto.

but only if she is able to walk her otherwise very impressive talk....

so ningekuwa mimi ni ACT, mustakabali wa chama ningemkabidhi huyu mama bila kusita.

but again, embu mambo ya Ngoswe tumwachie Ngoswe mwenyewe!
 
hiyo inamaanisha kana angekuwa Zitto, yaani Kiongozi wa Chama. hsisemi Mwenyekiti.
Cheo cha Zitto ni kiongozi mkuu, lakini chama kina viongozi wengine kama m/kiti, katibu nk.
 
Ndugu zangu naomba nifafanue kuwa hicho kipengele kinamhusu Kiongozi wa Chama (Party Leader). Ingetokea Zitto ameshindwa hivyo ndivyo ambavyo ingekuwa. Hii ni kwa sababu Kiongozi wa Chama anapaswa kuwa ndiye mtu wa kusimamia sera za chama katika vyombo vya maamuzi na hivyo itabidi awepo katika hivyo vyombo. Asipokuwemo chama kitapwaya.
 
Ndugu zangu naomba nifafanue kuwa hicho kipengele kinamhusu Kiongozi wa Chama (Party Leader). Ingetokea Zitto ameshindwa hivyo ndivyo ambavyo ingekuwa. Hii ni kwa sababu Kiongozi wa Chama anapaswa kuwa ndiye mtu wa kusimamia sera za chama katika vyombo vya maamuzi na hivyo itabidi awepo katika hivyo vyombo. Asipokuwemo chama kitapwaya.

ahaaaa. kinamhusu kiongozi mkuu wa chama sio kila kiongozi?
 
Ndugu zangu naomba nifafanue kuwa hicho kipengele kinamhusu Kiongozi wa Chama (Party Leader). Ingetokea Zitto ameshindwa hivyo ndivyo ambavyo ingekuwa. Hii ni kwa sababu Kiongozi wa Chama anapaswa kuwa ndiye mtu wa kusimamia sera za chama katika vyombo vya maamuzi na hivyo itabidi awepo katika hivyo vyombo. Asipokuwemo chama kitapwaya.

Prof.....mbona katiba haisemi kiongoz mkuu wa chama inasema kiongoz tu ,mana yake hata katibu Mwigamba aliye shindwa anatakiwa na yeye apigiwe kura??
 
Kipengele kinamuhusu Mwami Kabwe pekee

Profesa tolea ufafanuzi na hili la kusimamisha wagombea ubunge 240 nchi nzima na kuambulia jimbo moja tu nyumbani kwa kiongozi mkuu wa chama. Mnahitathmini vipi kwa resources mlizotumia na matokeo yaliyopatikana?
 
Ndugu zangu naomba nifafanue kuwa hicho kipengele kinamhusu Kiongozi wa Chama (Party Leader). Ingetokea Zitto ameshindwa hivyo ndivyo ambavyo ingekuwa. Hii ni kwa sababu Kiongozi wa Chama anapaswa kuwa ndiye mtu wa kusimamia sera za chama katika vyombo vya maamuzi na hivyo itabidi awepo katika hivyo vyombo. Asipokuwemo chama kitapwaya.
Mkuu Kitila, Zitto ni kiongozi Mkuu wa chama ila chama kina viongozi wengine, kipengele hakijasema Kiongozi Mkuu yaani "party leader" kimetaja kiongozi yeyote labda utuonyeshe kiliposema kiongozi mkuu.

kwa ufafanuzi wako viongozi wengine wa chama wakishindwa kwa sababu zozote zile (mfano kununuliwa) hawatawajibika kwa kipengele hicho, very fun.
 
Back
Top Bottom