Farolito
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 11,634
- 26,395
Wakuu,
Katika kupita mitandaoni nimekutana na hiki kitabu wanaita "The Urantia book" Urantia inamaanisha "Planet earth".
Hiki kitabu wanasema kina majibu ya mambo mengi sana,na waliokisoma wanasema ni kitabu ambacho kinakufanya uwe mtu bora sana ambacho kinamrudisha mtu katika kuthamini watu, uhusiano wako wewe na Mungu, na kina majibu mengi katika Sayansi, siasa, Philosofia na historia.
Haijulikani ni nani alikiandika ila huyu mtaalamu wa afya ya akili anaitwa W.S Sadler aliyekuwa akifanyia kazi Chicago alitokewa na viumbe fulani kati ya mwaka 1924 na 1935 ndio wakawa wanampa hayo maarifa,baadae ndio akakaa akawasimulia watu kadhaa ndio wakaunganisha hayo maandishi kuwa kitabu ambacho chapisho la kwanza lilitoka mwaka 1955.
Kitabu hiki kipo chini ya Urantia Foundation (www.urantia.org) ambayo ndio inatoa materials,inaandaa matukio na maelezo juu ya Urantia book.
Na ndio kitabu ambacho pia kina majibu ya kina juu ya miaka 18 ya upotevu ya Yesu ambayo haijaandikwa kwenye Bibilia, na katika kitabu hicho hakuna mahali wanasema Yesu alienda India kama ambavyo vitabu kadhaa vilidai.
Kitabu hiki kimegawanyika katika sehemu tatu;
1. The central and Super universe
2. The local universe
3. The history of Urantia
4. The life and teachings of Jesus.
Kitabu hiki hakina uhusiano na dini yeyote kwakuwa kinagusa nyanja tofauti tofauti kama nilivyoandika hapo juu.
Nimevutiwa kusoma kitabu hiki,Je kuna mtu humu JF ameshakisoma ili atueleze kilichomo ndani kwa ufupi?
Katika kupita mitandaoni nimekutana na hiki kitabu wanaita "The Urantia book" Urantia inamaanisha "Planet earth".
Hiki kitabu wanasema kina majibu ya mambo mengi sana,na waliokisoma wanasema ni kitabu ambacho kinakufanya uwe mtu bora sana ambacho kinamrudisha mtu katika kuthamini watu, uhusiano wako wewe na Mungu, na kina majibu mengi katika Sayansi, siasa, Philosofia na historia.
Haijulikani ni nani alikiandika ila huyu mtaalamu wa afya ya akili anaitwa W.S Sadler aliyekuwa akifanyia kazi Chicago alitokewa na viumbe fulani kati ya mwaka 1924 na 1935 ndio wakawa wanampa hayo maarifa,baadae ndio akakaa akawasimulia watu kadhaa ndio wakaunganisha hayo maandishi kuwa kitabu ambacho chapisho la kwanza lilitoka mwaka 1955.
Kitabu hiki kipo chini ya Urantia Foundation (www.urantia.org) ambayo ndio inatoa materials,inaandaa matukio na maelezo juu ya Urantia book.
Na ndio kitabu ambacho pia kina majibu ya kina juu ya miaka 18 ya upotevu ya Yesu ambayo haijaandikwa kwenye Bibilia, na katika kitabu hicho hakuna mahali wanasema Yesu alienda India kama ambavyo vitabu kadhaa vilidai.
Kitabu hiki kimegawanyika katika sehemu tatu;
1. The central and Super universe
2. The local universe
3. The history of Urantia
4. The life and teachings of Jesus.
Kitabu hiki hakina uhusiano na dini yeyote kwakuwa kinagusa nyanja tofauti tofauti kama nilivyoandika hapo juu.
Nimevutiwa kusoma kitabu hiki,Je kuna mtu humu JF ameshakisoma ili atueleze kilichomo ndani kwa ufupi?