Braza Kede
JF-Expert Member
- Nov 1, 2012
- 1,840
- 3,521
Kwa utafiti wangu mdogo hakujawahi kutokea matumizi mabovu ya lugha ya kiswahili kama muda huu tulionao.
Kibaya zaidi hata baadhi ya vyombo vya habari vikubwa vinashiriki dhambi hii.
Maneno mazuri ya kiswahili yamepindishwa kiasi inaleta kichefuchefu hata kusikiliza. Hapa nitaweka baadhi ya maneno.
Alikuwa = alikua
Kwa hiyo = ko
Baadhi = baazi
kufanikiwa = kujipata
sasa = saivi
Ndio hivyo = ndoivo
Ndio nini = ndonini
serikali = serekali/selekale
yaani = yani
mtaa = kitaa/kitaani
kwa sababu = co
Pasipo kuchukuliwa hatua za makusudi lugha hii inaelekea kupotea.
Chanzo kikuu cha haya ni uholela wa vyombo vya habari hasa habari za mtandaoni.
Nashauri mambo makubwa mawili yafanyike kwa haraka.
Kuwe na takwa la lazima kwa waleta habari kwa jamii wote kuwa na ufaulu mzuri wa lugha hii
vyombo vya habari vyote yaani vya kawaida na mitandaoni lazima visajiliwe kwanza na mamlaka za kiserikali kabla ya kuanza kupeleka habari yoyote kwa jamii.
Tuungane pamoja kuinusuru tunu yetu kuu ya lugha ya kiswahili
Kibaya zaidi hata baadhi ya vyombo vya habari vikubwa vinashiriki dhambi hii.
Maneno mazuri ya kiswahili yamepindishwa kiasi inaleta kichefuchefu hata kusikiliza. Hapa nitaweka baadhi ya maneno.
Alikuwa = alikua
Kwa hiyo = ko
Baadhi = baazi
kufanikiwa = kujipata
sasa = saivi
Ndio hivyo = ndoivo
Ndio nini = ndonini
serikali = serekali/selekale
yaani = yani
mtaa = kitaa/kitaani
kwa sababu = co
Pasipo kuchukuliwa hatua za makusudi lugha hii inaelekea kupotea.
Chanzo kikuu cha haya ni uholela wa vyombo vya habari hasa habari za mtandaoni.
Nashauri mambo makubwa mawili yafanyike kwa haraka.
Kuwe na takwa la lazima kwa waleta habari kwa jamii wote kuwa na ufaulu mzuri wa lugha hii
vyombo vya habari vyote yaani vya kawaida na mitandaoni lazima visajiliwe kwanza na mamlaka za kiserikali kabla ya kuanza kupeleka habari yoyote kwa jamii.
Tuungane pamoja kuinusuru tunu yetu kuu ya lugha ya kiswahili