Kisa cha mwili usojulikana ni wa nani. Hauna jino moja wala kovu lolote

SteveMollel

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
8,534
23,980
Baada ya kutokea kwa mauaji ya watu kadhaa, polisi wanafika eneo la tukio kwa lengo la kufanya uchunguzi.

Katika eneo hilo wanakutana na miili isiyopungua mitatu, yote imelala mfu, wanaikagua na kujiridhisha.

Screenshot_20240413-122641.png

Wanaupata mwili mwingine ndani ya 'basement', mwili wa msichana mzungu, makadirio ya miaka ishirini, wanaukagua na kubaini mwili huo una tofauti na miili mingine yote.
Screenshot_20240413-122543.png

Moja, mwili huu hauna mahusiano yoyote na eneo hili ulipokutwa. Si mkazi, jirani wala rafiki.

Pili, mwili hauna alama yoyote ya majeraha yenye mahusiano na kifo cha marehemu.

Tatu, hamna rekodi yeyote ya kutambua mwenye mwili huo ni nani. Kwasababu hiyo Polisi wanaukatia jina la kubuni: Jane Doe kisha wanaubeba na kuupeleka kwa wataalamu kwaajili ya uchunguzi zaidi. Zoezi hilo linaitwa 'Autopsy'.

Upande wa pili, wataalamu wa kuchunguza miili iliyokufa, Austin pamoja na baba yake mzazi, wapo kazini majira haya ya usiku.
ems.png

Yani wakati wewe unarithi shamba kwa mzee wako, mwenzio anarithi mochwari kupambana na maiti. Uzuri pale bar mhudumu haulizi pesa ya bia umeitolea wapi.

Hapo kazini anakuja msichana mmoja mrembo, 'girlfriend' wa Austin, kwa lengo la kumpitia mpenziwe waende zao mtoko.
Screenshot_20240413-122831.png

Msichana huyo anaona maiti moja imefungwa kengele ndogo mguuni. Anashangaa na kuuliza, hii ni nini?

Baba Austin anamtoa shaka, hiyo ni teknolojia ya zamani. Maiti ilifungiwa kengele ili kama mtu hajafa na ikatokea ameamka basi waliokaribu watasikia kengele na kuja upesi kumsaidia.
Screenshot_20240413-122950.png

Haipiti muda, mwili mpya unaingizwa eneo hili kwaajili ya kutendewa kazi. Kwasababu hiyo, Austin anamwomba mpenziwe arudi baadae kwani kwa sasa kuna kazi ya kufanya.

Mwanamke anaaga na kazi inaanza rasmi.

Kufungua mfuko, ni mwili wa Jane Doe.
Screenshot_20240413-123225.png

Wanaupekua.

Mwili hauna kovu lolote. Maungio ya mikono na miguu yamevunjika. Mdomoni jino moja halipo. Viini vya macho yake vina rangi ya kufifia.

Wanamchana kukagua viungo vyake vya ndani, wanakuta vina ishara na alama za kuungua. Wanastaajabu ameunguaje ndani wakati nje hana hata doa?
Screenshot_20240412-214343.png

Mara wanasikia sauti ya purukushani juu ya paa, Austin kwenda kutazama anamkuta paka wa baba yake amekufa.

Baba anahuzunika maana paka huyu alikuwa ni kumbukumbu ya marehemu mkewe. Anaomboleza kidogo kisha anarejea tena kazini kuendelea na uchunguzi wa Jane Doe.

Mara hii, anakumbana na kitambaa kidogo kilichojifunga. Kukitazama ndani kuna alama na michoro pia kuna lile jino lililong'olewa mdomoni mwa marehemu.
Screenshot_20240413-123604.png

Screenshot_20240413-123639.png

Hii inamaana Jane Doe katika enzi ya uhai wake, alimeza au alimezeshwa kitambaa hicho na jino lake. Kwanini? Hamna anayejua.

Wanakagua ngozi yake kwa ndani, wanaona ina alama zilezile zilizochorwa katika kile kitambaa kidogo.

Wakiwa wanaendelea kupembua, wanashtuka taa zinakonyeza. Mara moja. Mara mbili. Mara tatu. Mara zinapiga shoti na giza totoro linameza chumba kizima kufumba na kufumbua!

Sasa hamna kuonana bali kukisia. Hamna kushika bali kupapasa.

Hata kama ni wewe, tumbo lisingeitika abeeh?

Baba anawasha 'lighter' wapate ahueni ya kutazama japo mwanga wake ni hafifu.
Screenshot_20240413-123836.png

Wanaangaza macho, mwili wa Jane Doe upo palepale walipouacha, ila wanapoangaza kwenye makabati ya kuhifadhi maiti, mambo yapo kinyume.

Milango ipo wazi na miili yote haipo!

Hapa ndo mate yanatawanyika mdomoni, ulimi unabaki kuwa mkavu. Mapigo ya moyo yanahamia tumboni, na baridi lisiloeleweka linakupapasa miguuni mpaka kichwani.

Wanakimbilia kwenye lifti, milango haifungi. Huko nje, mvua kubwa inanyesha, imeangushia mti mkubwa kwenye mlango wa dharura, mlango hauwezi kufunguka.
Screenshot_20240413-124008.png

Tazama simu, mtandao uko chini vibaya mno, ukipiga inajikata tu yenyewe.

Wafanye nini?

Wanarudi kwenye chumba cha maiti kukabiliana na Jane Doe kwani mwili wake ndo' umeleta balaa. Wanaumwagia mafuta na kuupiga kiberiti!

Moto unasambaa. Wanahaha tena kuuzima kwa 'fire extinguisher'. Moto unakata lakini wanashangaa mwili wa Jane Doe uko vilevile, hauna chunusi, harara wala tangotango!
Screenshot_20240413-123150.png

Kidogo wanasikia sauti ya lift, wanakimbilia huko upesi kujiokoa. Kufika lift haipandi wala haishuki.

Wanaangaza ndani ya kiza hiki kinene.

Jasho jembamba linachuruza.

Mara wanasikia sauti ya kengele.

Sauti ya kengele inasogea.

Unaikumbuka kengele hii? Unaikumbuka kazi yake ni nini?

Baba anashikwa na hofu kali, anarusha shoka lake gizani, shoka linakita humo na mara kunakuwa kimya. Kengele inanyamaza.

Wanatoka kwenda kutazama, wanakuta mwili wa mchumba wake Austin umelala chini. Shoka limemgonga na anavuja damu akifa.
Screenshot_20240413-124040.png

Maskini. Alikuja kumpitia mpenzi wake kama walivyoahidiana, sasa yuko chini anakata kauli.

Kuna atakayenusurika humu?

Jane Doe ni nani? Anahusika nini na mauaji haya?

Nisikupotezee muda, kaitazame Movie ya; "The Autopsy of Jane Doe".
b66cfba4f5a06b2cc63bd4d2c95bba08.png
 
UNAFANYA NINI AKIANZA KUFA MTU MMOJAMMOJA KWENYE PICHA MLOPIGA PAMOJA?

Bird ni msichana mmoja mwenye haya. Kitu pekee anachopenda ni kupiga picha watu.

Mbali na masomo aloanza katika shule mpya, Bird anafanya kazi katika duka la kuuza vitu vya kale, huko yupo na mfanyakazi mwenzake anayeitwa Tyler.

Tyler humwambii kitu kwa Bird japo mdomo wake ndo' hivyo tena, kama wa Timbulo, kuongea tatizo. Mdomo kilo tano.

Afanye nini? Anatumia matendo. Anamletea Bird zawadi ya kamera ya toleo la kale ambayo ukipiga picha inatoka papohapo.

Bird anaifurahia sana zawadi yake na picha yake ya kwanza kabisa anampiga Tyler.

Wakiwa wanaitazama picha hiyo, Tyler anaiona hii ndo' nafasi sasa ya kujaribu kumbusu Bird.

Anasogeza lips lakini mdada anakataa na kuondoka zake.

Yani busu kalikataa lakini kamera ya 'mwana' kabeba. Eeh Mungu tuone wanaume na mateso haya. Hatuwezi peke yetu baba.

Bird anaenda zake nyumbani, baadae anaongea na rafiki yake aitwaye Kesie kuhusu party flani hivi.

Huko anakutana na wanafunzi wenzake; Mia na Devin ambao ni wapenzi, pia msichana Avery na jamaa mmoja 'bishoo' anayeitwa Connor.

Huyu Connor sasa ndo roho ya Bird. Dada kajifia kaoza hapa. Yani akimshika hata mkono, hali ya manyunyu inaanza. Jiulize akishikwa kiuno je?

Wanafurahia party, kunywa na muziki. Bird anatazama kwenye mkoba wake, anaiona ile picha ya Tyler aloipiga, anaitazama na kugundua kuna kivuli nyuma ya Tyler.

Anajaribu kufuta kwa vidole lakini hafanikiwi. Anapuuzia na kuendelea na mambo yake.

Anaitumia kamera ile ya zawadi kuwapiga wenzake picha kadhaa lakini muda si mrefu polisi wanawasili eneo la tukio wakimuhitaji msichana huyo kwa mahojiano ya kesi ya mauaji.

Anaongozana na polisi mpaka kituoni anapoelezwa kuwa mfanyakazi mwenzake, yaani Tyler, amefariki kifo tata na hivyo wanataka maelezo yake.

Anajieleza namna anavyomjua Tyler na mara ya mwisho kuonana naye kisha anaenda zake.

Baadae anatazama picha ya Tyler, anagundua kile kivuli kilichokuwepo mwanzo hakipo tena.

Anatazama picha zote alizopiga kwenye party, anabaini picha zote zina vivuli kwa nyuma. Hata ukijaribu kuvifuta, havifutiki.

Kesho yake asubuhi, rafiki yake, Kesie, anampigia simu na kumpa habari za msiba. Mwanafunzi mwenzao, Avery, amefariki usiku.

Bird anatazama picha alompiga Avery, picha ya kwenye party jana usiku, anastaajabu kile kivuli kilichokuwepo mwanzoni hakipo tena!

Hapa sasa Bird anaanza kupata mashaka. Kesi ya Tyler na Avery ni mafiga ya jiko moja.

Anawapa wenzie habari kuwa kuna tatizo na zile picha walizopiga na anahisi zina mahusiano na kifo cha Avery.

Anawaambia mambo ya vivuli katika picha lakini wenzake wanaona hizo ni hekaya. Devin anachukua picha walopiga pamoja kisha anaipiga moto kwa kibiriti chake cha gesi.

Picha inashika moto, na mara Mina naye anaanza kuungua!

Moto umetokea wapi?

Hamna anayejua.

Wanajaribu kuuzima lakini ndo' kwanza unapamba. Mara Kesie naye anadaka moto na sasa inakuwa tafarani ya nyoka kwenye chungu cha jikoni.

Bird anapata akili. Anakimbilia picha inayoungua na kuizima upesi, ajabu moto nao unazima, lakini hali ya Mina inakuwa mbaya maana moto ulishamtafuna sana.

Wanamkimbiza hospitali kupata matibabu na sasa kila mtu anasadiki kile alichokisema Bird.

Kuna kitu katika zile picha.

Kitu kinachopelekea kifo.

Bird na Connor wanaongozana kwenda nyumbani kwa marehemu Tyler kuangaza kama wanaweza kupata kitu kuhusu kamera ile walotumia maana ni ndiyo chanzo.

Kufika, Connor anabakia kwenye gari na Bird anazama ndani ya nyumba kupekua.

Ndani ni kiza kinene na Bird hawezi washa taa maana hiki anachofanya ni uvamizi.

Anapekua hapa na pale. Anashika hiki na kile.

Ndani ya giza totoro.

Mwishowe, kama bahati, anakumbana na mkoba wa kamera lakini kitambo kidogo anabaini humu ndani ya giza hayuko mwenyewe.

Kuna kitu kinataka roho yake.

Anakurupuka upesi ili ajinusuru. Anakimbilia nje anapokwea gari na kutimka haraka.

Njiani, anampigia Mina aliyelazwa hospitalini. Anamtahadharisha asikae mwenyewe na asikae gizani kwani muuaji anamshambulia mtu aliyepo kwenye mazingira hayo.

Wanapofika hospitali, wanapokelewa na habari kwamba Mina amefariki na polisi wamesema amejiua mwenyewe!

Devin, mpenzi wa Mina, anamlaumu Bird kwa kuwaingiza kwenye matatizo makubwa.

Na Bird anajiona ana jukumu la kuwaokoa wenzake kabla wote hawajaisha.

Anaanzia wapi?

Aanzie kwenye ule mkoba wa Tyler.

Kwenye picha, kivuli kinahama kutoka mtu mpaka mtu, na kinapohamia hakitoki bila ya kwenda na uhai.

Watatu washaenda, wengine watapona?

Bird yuko nje ya muda.

Na hajui anachopambana nacho ni nini.

Tazama: "POLAROID".
images.jpg
 
Baada ya kutokea kwa mauaji ya watu kadhaa, polisi wanafika eneo la tukio kwa lengo la kufanya uchunguzi.

Katika eneo hilo wanakutana na miili isiyopungua mitatu, yote imelala mfu, wanaikagua na kujiridhisha.

View attachment 2962443
Wanaupata mwili mwingine ndani ya 'basement', mwili wa msichana mzungu, makadirio ya miaka ishirini, wanaukagua na kubaini mwili huo una tofauti na miili mingine yote.
View attachment 2962445
Moja, mwili huu hauna mahusiano yoyote na eneo hili ulipokutwa. Si mkazi, jirani wala rafiki.

Pili, mwili hauna alama yoyote ya majeraha yenye mahusiano na kifo cha marehemu.

Tatu, hamna rekodi yeyote ya kutambua mwenye mwili huo ni nani. Kwasababu hiyo Polisi wanaukatia jina la kubuni: Jane Doe kisha wanaubeba na kuupeleka kwa wataalamu kwaajili ya uchunguzi zaidi. Zoezi hilo linaitwa 'Autopsy'.

Upande wa pili, wataalamu wa kuchunguza miili iliyokufa, Austin pamoja na baba yake mzazi, wapo kazini majira haya ya usiku.
View attachment 2962446
Yani wakati wewe unarithi shamba kwa mzee wako, mwenzio anarithi mochwari kupambana na maiti. Uzuri pale bar mhudumu haulizi pesa ya bia umeitolea wapi.

Hapo kazini anakuja msichana mmoja mrembo, 'girlfriend' wa Austin, kwa lengo la kumpitia mpenziwe waende zao mtoko.
View attachment 2962448
Msichana huyo anaona maiti moja imefungwa kengele ndogo mguuni. Anashangaa na kuuliza, hii ni nini?

Baba Austin anamtoa shaka, hiyo ni teknolojia ya zamani. Maiti ilifungiwa kengele ili kama mtu hajafa na ikatokea ameamka basi waliokaribu watasikia kengele na kuja upesi kumsaidia.
View attachment 2962449
Haipiti muda, mwili mpya unaingizwa eneo hili kwaajili ya kutendewa kazi. Kwasababu hiyo, Austin anamwomba mpenziwe arudi baadae kwani kwa sasa kuna kazi ya kufanya.

Mwanamke anaaga na kazi inaanza rasmi.

Kufungua mfuko, ni mwili wa Jane Doe.
View attachment 2962452
Wanaupekua.

Mwili hauna kovu lolote. Maungio ya mikono na miguu yamevunjika. Mdomoni jino moja halipo. Viini vya macho yake vina rangi ya kufifia.

Wanamchana kukagua viungo vyake vya ndani, wanakuta vina ishara na alama za kuungua. Wanastaajabu ameunguaje ndani wakati nje hana hata doa?
View attachment 2962453
Mara wanasikia sauti ya purukushani juu ya paa, Austin kwenda kutazama anamkuta paka wa baba yake amekufa.

Baba anahuzunika maana paka huyu alikuwa ni kumbukumbu ya marehemu mkewe. Anaomboleza kidogo kisha anarejea tena kazini kuendelea na uchunguzi wa Jane Doe.

Mara hii, anakumbana na kitambaa kidogo kilichojifunga. Kukitazama ndani kuna alama na michoro pia kuna lile jino lililong'olewa mdomoni mwa marehemu.
View attachment 2962454
View attachment 2962455
Hii inamaana Jane Doe katika enzi ya uhai wake, alimeza au alimezeshwa kitambaa hicho na jino lake. Kwanini? Hamna anayejua.

Wanakagua ngozi yake kwa ndani, wanaona ina alama zilezile zilizochorwa katika kile kitambaa kidogo.

Wakiwa wanaendelea kupembua, wanashtuka taa zinakonyeza. Mara moja. Mara mbili. Mara tatu. Mara zinapiga shoti na giza totoro linameza chumba kizima kufumba na kufumbua!

Sasa hamna kuonana bali kukisia. Hamna kushika bali kupapasa.

Hata kama ni wewe, tumbo lisingeitika abeeh?

Baba anawasha 'lighter' wapate ahueni ya kutazama japo mwanga wake ni hafifu.
View attachment 2962456
Wanaangaza macho, mwili wa Jane Doe upo palepale walipouacha, ila wanapoangaza kwenye makabati ya kuhifadhi maiti, mambo yapo kinyume.

Milango ipo wazi na miili yote haipo!

Hapa ndo mate yanatawanyika mdomoni, ulimi unabaki kuwa mkavu. Mapigo ya moyo yanahamia tumboni, na baridi lisiloeleweka linakupapasa miguuni mpaka kichwani.

Wanakimbilia kwenye lifti, milango haifungi. Huko nje, mvua kubwa inanyesha, imeangushia mti mkubwa kwenye mlango wa dharura, mlango hauwezi kufunguka.
View attachment 2962458
Tazama simu, mtandao uko chini vibaya mno, ukipiga inajikata tu yenyewe.

Wafanye nini?

Wanarudi kwenye chumba cha maiti kukabiliana na Jane Doe kwani mwili wake ndo' umeleta balaa. Wanaumwagia mafuta na kuupiga kiberiti!

Moto unasambaa. Wanahaha tena kuuzima kwa 'fire extinguisher'. Moto unakata lakini wanashangaa mwili wa Jane Doe uko vilevile, hauna chunusi, harara wala tangotango!
View attachment 2962459
Kidogo wanasikia sauti ya lift, wanakimbilia huko upesi kujiokoa. Kufika lift haipandi wala haishuki.

Wanaangaza ndani ya kiza hiki kinene.

Jasho jembamba linachuruza.

Mara wanasikia sauti ya kengele.

Sauti ya kengele inasogea.

Unaikumbuka kengele hii? Unaikumbuka kazi yake ni nini?

Baba anashikwa na hofu kali, anarusha shoka lake gizani, shoka linakita humo na mara kunakuwa kimya. Kengele inanyamaza.

Wanatoka kwenda kutazama, wanakuta mwili wa mchumba wake Austin umelala chini. Shoka limemgonga na anavuja damu akifa.
View attachment 2962460
Maskini. Alikuja kumpitia mpenzi wake kama walivyoahidiana, sasa yuko chini anakata kauli.

Kuna atakayenusurika humu?

Jane Doe ni nani? Anahusika nini na mauaji haya?

Nisikupotezee muda, kaitazame Movie ya; "The Autopsy of Jane Doe".
View attachment 2962461
Mmmh steve embu njoo chemba
 
Nisikupotezee muda, kaitazame Movie ya; "The Autopsy of Jane Doe".
Samahani, kuna story ulisimulia humu ya kutisha kidogo ambayo ilihusu mpangaji mchawi! Ulitumia mazingira ya bongo kuinogesha! Lakini kwa mtazamo wangu ile ni movie! Inaitwaje??
 
Samahani, kuna story ulisimulia humu ya kutisha kidogo ambayo ilihusu mpangaji mchawi! Ulitumia mazingira ya bongo kuinogesha! Lakini kwa mtazamo wangu ile ni movie! Inaitwaje??
Sio movie.

Mtazamo wako umekuja hivyo sababu ya namna nilivyosimulia tu.
 
Back
Top Bottom