#COVID19 Kenya yapokea zaidi ya dozi laki 8 za Moderna

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,038
9,928
Kenya imepokea dozi nyingine 880,320 za chanjo ya Moderna.

Hii ni awamu ya pili ya dozi milioni 1.76 zilizotolewa na serikali ya Marekani nchini Kenya , kupitia kituo cha Covax.

Chanjo hizo zimewasili nchini Kenya Jumatatu asubuhi. "Kundi la 2 la dozi 880,320 za chanjo ya Moderna # COVID19 imewasili Kenya leo asubuhi. Msaada wa Serikali ya Marekani kupitia #COVAX," WHO Kenya iliandika ujumbe kwenye tweeter.

Kundi la kwanza la chanjo 880,460 za Moderna ziliwasili nchini Jumatatu, Agosti 23, 2021. Hatua hii inakuja kama kichocheo katika kupambana dhidi ya ugonjwa wa Covid-19.

Kenya sasa ina kipimo cha chanjo 2,284, 292 ambazo zinapatikana kwa matibabu.

Ijumaa ya wiki iliyopita, Kenya ilipokea kundi la kwanza la chanjo moja ya Johnson Johnson Covid-19.
 
Back
Top Bottom