CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 5,012
- 4,118
Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika ukurasa wake wa Whatsapp ameandika haya,
๐๐
====
" Mapema leo jijini Nairobi nchini Kenya nikihutubia katika Mkutano wa Shirikisho la Maendeleo la Kimataifa (IDA). Pamoja na miradi mingine, kwa ushirikiano na IDA nchi yetu imeweza pia;-
1. Kuboresha eneo la afya ya mama na mtoto tukiwa na moja ya mifumo bora zaidi kwa ukanda wa Afrika,
2. Kuimarisha usambazaji umeme vijijini, eneo ambalo pia Tanzania ni moja ya nchi bora zaidi kwenye ukanda huu wa bara letu,
3. Kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama, na
4. Kuanza kwa miradi mikubwa ya kudhibiti mafuriko hasa katika Jiji la Dar es Salaam ikiwemo mpango wa uboreshaji wa Bonde la Mto Msimbazi ili kudhibiti mafuriko ya mara kwa mara (Msimbazi Basin Development Project).
Katika hotuba yangu nimesisitiza kuwa na sera bora za kifedha toka mashirika ya kimataifa kwa bara letu, zenye masharti na gharama nafuu, zinazotazama kuongeza uwekezaji katika kukuza rasilimali watu na teknolojia na kujikita zaidi katika kukuza uwezo wa kuongeza idadi ya mipango inayotekelezwa kati yake na nchi washiriki"
Pamoja na hayo pia ametuma salamu zake za meimosi kwa Watanzania,
Hivi ndivyo alivyosema
,๐๐
"Kheri ya Siku ya Wafanyakazi kwenu nyote. Siku hii ni ya mambo makubwa mawili. Jambo la kwanza ni kwa sote kuwashukuru wale ambao kwa kazi zao sisi kama Taifa tunaweza kusonga mbele; kuanzia dada wa kazi hapo nyumbani anayeamka mapema alfajiri kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa, hadi daktari anayehakikisha tunapata tiba pale tunapokuwa na changamoto ya maradhi. Tunawashukuru nyote katika kila kona ya nchi yetu. Ahsanteni kwa kazi.
Jambo la pili, leo pia ni siku ya kurudia ahadi yetu kwenu. Ahadi ambayo kila wakati tumekuwa tukiitoa na kuitekeleza kadiri tuwezavyo. Ahadi kwamba kama Serikali tutaendelea kutekeleza jukumu letu la msingi kuhakikisha mazingira ya kazi yanazidi kuwa bora zaidi kwa kila mmoja si tu mishahara, bali pia haki katika maeneo ya kazi, kupanda madaraja kwa wakati, kupata stahiki sahihi na uboreshaji wa mifumo yetu ya pensheni."
๐๐
====
" Mapema leo jijini Nairobi nchini Kenya nikihutubia katika Mkutano wa Shirikisho la Maendeleo la Kimataifa (IDA). Pamoja na miradi mingine, kwa ushirikiano na IDA nchi yetu imeweza pia;-
1. Kuboresha eneo la afya ya mama na mtoto tukiwa na moja ya mifumo bora zaidi kwa ukanda wa Afrika,
2. Kuimarisha usambazaji umeme vijijini, eneo ambalo pia Tanzania ni moja ya nchi bora zaidi kwenye ukanda huu wa bara letu,
3. Kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama, na
4. Kuanza kwa miradi mikubwa ya kudhibiti mafuriko hasa katika Jiji la Dar es Salaam ikiwemo mpango wa uboreshaji wa Bonde la Mto Msimbazi ili kudhibiti mafuriko ya mara kwa mara (Msimbazi Basin Development Project).
Katika hotuba yangu nimesisitiza kuwa na sera bora za kifedha toka mashirika ya kimataifa kwa bara letu, zenye masharti na gharama nafuu, zinazotazama kuongeza uwekezaji katika kukuza rasilimali watu na teknolojia na kujikita zaidi katika kukuza uwezo wa kuongeza idadi ya mipango inayotekelezwa kati yake na nchi washiriki"
Pamoja na hayo pia ametuma salamu zake za meimosi kwa Watanzania,
Hivi ndivyo alivyosema
,๐๐
"Kheri ya Siku ya Wafanyakazi kwenu nyote. Siku hii ni ya mambo makubwa mawili. Jambo la kwanza ni kwa sote kuwashukuru wale ambao kwa kazi zao sisi kama Taifa tunaweza kusonga mbele; kuanzia dada wa kazi hapo nyumbani anayeamka mapema alfajiri kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa, hadi daktari anayehakikisha tunapata tiba pale tunapokuwa na changamoto ya maradhi. Tunawashukuru nyote katika kila kona ya nchi yetu. Ahsanteni kwa kazi.
Jambo la pili, leo pia ni siku ya kurudia ahadi yetu kwenu. Ahadi ambayo kila wakati tumekuwa tukiitoa na kuitekeleza kadiri tuwezavyo. Ahadi kwamba kama Serikali tutaendelea kutekeleza jukumu letu la msingi kuhakikisha mazingira ya kazi yanazidi kuwa bora zaidi kwa kila mmoja si tu mishahara, bali pia haki katika maeneo ya kazi, kupanda madaraja kwa wakati, kupata stahiki sahihi na uboreshaji wa mifumo yetu ya pensheni."