#COVID19 Kenya: Chanjo ya Covid lazima kwa watumishi wa Umma

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
28,182
36,169
Kuwa na dhamana ya maisha ya watu ni pamoja na kuwajibika zaidi hata dhidi ya ujinga wao.

Babu wa Loliondo angekuwa hai Kenya lakini si Tanzania.

IMG_20210811_081245_498.jpg


Heko rais Kenyatta kwa maana heri lawama kuliko fedheha. Kenya kwa mtumishi wa umma, chanjo ni lazima.

Pole pole tutafika tu.

Kwanza Janssen zenyewe zimekuja 1m peke yake.

----
Kenya pc

Summary

  • Serikali ya Kenya imetoa siku 13 kwa watumishi wote wa umma kuchanjwa dhidi ya maambukizi ya corona.
By Anna Potinus

Nairobi:
Serikali ya Kenya imetoa siku 13 kwa watumishi wote wa umma nchini humo kuhakikisha wanapata chanjo dhidi ya virusi vya corona na kwamba watakaokiuka agizo hilo hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao.

Taarifa iliyotolewa na mkuu wa utumishi wa umma nchini humo imesema agizo hilo limetokana na idadi ndogo ya watumishi waliopata chanjo hasa waalimu na wale walio katika sekta ya usalama.

“Baadhi ya watumishi wa mma wamekwepa chanjo hiyo kwa makusudi ili wasihudhurie kazini hatua ambayo imezorotesha utoaji wa huduma,” amesema.

Hadi kufikia jana Jumatatu Agosti 9, 2021 Kenya iliripoti maambukizi mapya 745 na kufanya idadi ya maambukizi iliyothibitshwa nchini humo kufikia 212,573 tangu kuanza kwa janga hilo.

Wiki iliyopita serikali ilisema imetoa chanjo milioni 1.7 ya AstraZeneca, nyingi kati ya hizo ni dozi ya kwanza.

Kenya inalenga kuchanja watu milioni 10 mwishoni mwa mwaka huu.

Chanzo: Mwananchi
 
Kenyatta dikteta, sisi mama ameamua tuwe hiari ndio maana hakuna ulazima. Ulazima ni wapinzani wasiongelee katiba mpya na wakae ndani.
Akina Polepole, Gwajiboy et al wanademka na mama hana la kufanya
 
Hizo chanjo mwendokasi matokeo yake ni kuibua variants ambao watakosa chanjo na tiba kabisa. Na hapo ndipo kila mtu ataanza kumsakama daktari wake. It's now proven that these ineffective false vaccines ndizo zinazosababisha SARS-COVID-2 iwe kaa la moto ulimwenguni.
 
Hamna cha heko Kenyatta wala nini. Sasa wale wa sekta binafsi ndiyo hawakufii. Wahudumu wa matatu, wauza vitu sokoni, mama ntilie, wafanyakazi wa kampuni au taasisi zisizo za kiserikali je? Hao hawapigwi na uviko 19?
 
Hamna cha heko kenyata wala nini. Sasa wale wa sekta binafsi ndiyo hawakufii. Wahudumu wa matatu, wauza vitu sokoni, mama ntilie, wafanyakazi wa kampuni au taasisi zisizo za kiserikali je?? Hao hawapigwi na uviko 19?

Mambo huenda pole pole na heri ya nusu shari kuliko shari kamili.

IMG_20210811_081245_498.jpg


Kwani upumbafu huo wewe una uona je?

NB: Upumbafu siyo upumbavu.
 
Hamna cha heko Kenyatta wala nini. Sasa wale wa sekta binafsi ndiyo hawakufii. Wahudumu wa matatu, wauza vitu sokoni, mama ntilie, wafanyakazi wa kampuni au taasisi zisizo za kiserikali je? Hao hawapigwi na uviko 19?
Una hoja za kitoto sana. Umeambiwa hao uliowataja wamenyimwa chanjo? Wanahamishwa kila siku wakaipokee na wengine wao tayari wameitikia wito, ila ni kwa hiari yao.
Hawa wanaoshurutishwa na bosi wao ni kwasababu serikali ndio mwajiri wao. Mleta mada tafadhali chora kibonzo, ili watu wa sampuli kama hii waelewe ujumbe wako kwa urahisi.
 
Una hoja za kitoto sana. Umeambiwa hao uliowataja wamenyimwa chanjo? Wanahamishwa kila siku wakaipokee na wengine wao tayari wameitikia wito, ila ni kwa hiari yao.
Hawa wanaoshurutishwa na bosi wao ni kwasababu serikali ndio mwajiri wao. Mleta mada tafadhali chora kibonzo, ili watu wa sampuli kama hii waelewe ujumbe wako kwa urahisi.

Kunywa maji utulie, ndiyo uje tena.
🤣 🤣 🤣
 
Acha upumbavu kwenye masuala nyeti kama haya, yanayohusu uhai wa binadamu wenzako. Grow up!

Siku hizi (ndiyo maana) sipendi sana kujadiliana na nyie hapa. Nimegundua wengi mnakuja kujadiliana wakati hamjala, mna njaa. Ndiyo maana mnarusha mitusi kwa kila aliyeko mbele yako.
🤣 🤣 🤣
Ongeza maji kidogo.
 
Back
Top Bottom