mshamba_hachekwi
JF-Expert Member
- Mar 3, 2023
- 17,122
- 53,118
Kama unatumia sana youtube utakuwa umekutana na matangazo ya mikopo mtandao.
Mimi sikuwa nayazingatia mpaka yakaanza kuwa ya ajabu ajabu kama hivi;
Basi nikaamua kufuatilia kidogo, nikatafuta makampuni yanayomiliki haya matangazo.
Cha kushangaza utakuta vikampuni vingi vingi viko chini ya kampuni moja kubwa.
Mfano Singularity Microfinance Limited ina matangazo ya PesaX na CashX.
Dexintec Global Limited inamiliki kwanzaloan, hewamkopo, twigaloan, finiloan, na jiachie cash.
Dexintec wamechapisha matangazo 40+ ndani ya huu mwezi mmoja tu kutoka April.
Dexintec ni kampuni ya kichina, wana fanya kazi kwenye nchi maskini kama Nigeria na Pakistan
Huko mitandaoni watu wanalalamika mikopo yao inawakandamiza.
Hawa majamaa ni loan sharks. Huu ni uhalifu kabisa, kunyonya maskini kupitia mikopo.
Nimesikia mwigulu alisema bungeni huduma za mobile money kama Airtel timiza, Vodacom songesha hazina leseni, kama hao hawana, hawa kausha damu vipi?
Na wakati huo huo BOT wanasema watoa mikopo mtandao wapo chini ya makampuni yenye leseni. Ingekuwa hivyo, wangenyonya watu?
Nimewaza tu, nakaribisha wenye mawazo/maoni mbalimbali.
Mimi sikuwa nayazingatia mpaka yakaanza kuwa ya ajabu ajabu kama hivi;
Basi nikaamua kufuatilia kidogo, nikatafuta makampuni yanayomiliki haya matangazo.
Cha kushangaza utakuta vikampuni vingi vingi viko chini ya kampuni moja kubwa.
Mfano Singularity Microfinance Limited ina matangazo ya PesaX na CashX.
Dexintec Global Limited inamiliki kwanzaloan, hewamkopo, twigaloan, finiloan, na jiachie cash.
Dexintec wamechapisha matangazo 40+ ndani ya huu mwezi mmoja tu kutoka April.
Dexintec ni kampuni ya kichina, wana fanya kazi kwenye nchi maskini kama Nigeria na Pakistan
Huko mitandaoni watu wanalalamika mikopo yao inawakandamiza.
Hawa majamaa ni loan sharks. Huu ni uhalifu kabisa, kunyonya maskini kupitia mikopo.
Nimesikia mwigulu alisema bungeni huduma za mobile money kama Airtel timiza, Vodacom songesha hazina leseni, kama hao hawana, hawa kausha damu vipi?
Na wakati huo huo BOT wanasema watoa mikopo mtandao wapo chini ya makampuni yenye leseni. Ingekuwa hivyo, wangenyonya watu?
Nimewaza tu, nakaribisha wenye mawazo/maoni mbalimbali.