Kambi ya Upinzani Bungeni IVUNJWE...

ZeMarcopolo

Platinum Member
May 11, 2008
14,019
7,223
Baada ya Mbowe kusema mbele ya watanzania kuwa Zitto Kabwe ni mnafiki, itakuwa ni unafiki zaidi kwa Mbowe kuendelea kufanya kazi na Zitto kama Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Hii ni sawa na siku Kikwete akisema hadharani kuwa Pinda ni mnafiki na kumvua vyeo vyote vya CCM lakini akamuacha kuwa Waziri Mkuu. Jambo hilo haliwezekani!

Kwa mantiki hii, iwapo hotuba ya Zitto ya leo haitatangaza kujiuzuru unaibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mbowe atalazimika kuvunja Baraza kivuli la Mawaziri na kuliunda upya. Asipofanya hivyo atakuwa ni mnafiki mara dufu.

Wakati huohuo, kwa kutumia busara, ingawa sheria hailazimishi, Mbowe au Dr. Slaa anawajibika kumpa Spika taarifa rasmi ya maandishi kuhusu Zitto kuvuliwa uongozi Chadema, Spika wa Bunge baada ya kupata taarifa hiyo anawajibika kumuuliza KUB kwa maandishi iwapo anaridhika na Zitto kuendelea na uenyekiti wa PAC.

Busara inataka hivyo kwa sababu Zitto amepewa uenyekiti wa PAC kutoka upinzani, anawakilisha upinzani. Kwa vile upinzani unamuona Zitto msaliti, Spika akikaa kimya tu ataingizwa kwenye lawama ya kuingiza wasaliti kwenye nafasi za wapinzani. Lakini ili hata yote yatokee ni LAZIMA Mbowe au Dr. Slaa amuandikie barua rasmi Spika kumjulisha msimamo wa Chadema juu ya Zitto.

Iwapo KUB atasema haridhishwi na Zitto kuongoza PAC, basi Spika atawajibika "kumshauri" ajiuzuru nafasi hiyo.

Kama tuko seriuos na utawala bora, hivi ndivyo tunavyotakiwa kufanya...
 
Na chadema watafanya hivo kwani hiki ni chama makin na huwa hawakurupuki ktk maamuzi
 
Hujui kitu wewe, kaa chini ujifunze au ufundishwe sheria, kanuni na taratibu za Bunge JMT. Hizo ni hisia na wishful thinking.

Kama ungekuwa na umakini kidogo tu; ktk press conference CC ya CHADEMA iliagiza mchakato wa kumvua Zitto unaibu kiongozi wa KUB ufanyike.

Ila kama ulivyosema, Zitto ni MNAFIKI na MSALITI, hapo nakuunga mkono 100%
 
Hujui kitu wewe, kaa chini ujifunze au ufundishwe sheria, kanuni na taratibu za Bunge JMT. Hizo ni hisia na wishful thinking.

Kama ungekuwa na umakini kidogo tu; ktk press conference CC ya CHADEMA iliagiza mchakato wa kumvua Zitto unaibu kiongozi wa KUB ufanyike.

Ila kama ulivyosema, Zitto ni MNAFIKI na MSALITI, hapo nakuunga mkono 100%

Wewe ni mlaghaika. Kumvua Zitto unaibu KUB sio mchakato, ni swala la Mbowe tu kunyanyuka na kusema.

Mchakato wa nini sasa? Wabongo mnapenda sana michakato michakato. Hata kufungua mlango wa gari utasema "nimeanza mchakato wa kufungua huu mlango wa gari".
 
mbowe na ZZK kiuwezo wa siasa sawa ulinganishe MESSI(ZZK) na Ngasa(mbowe)-ZZK is a threat to tengeru AISEE
 
Wewe ni mlaghaika. Kumvua Zitto unaibu KUB sio mchakato, ni swala la Mbowe tu kunyanyuka na kusema.

Mchakato wa nini sasa? Wabongo mnapenda sana michakato michakato. Hata kufungua mlango wa gari utasema "nimeanza mchakato wa kufungua huu mlango wa gari".

Ngoja na mimi nianze mchakato wa kukomenti thred yako! teh teh
 
Hujui kitu wewe, kaa chini ujifunze au ufundishwe sheria, kanuni na taratibu za Bunge JMT. Hizo ni hisia na wishful thinking.

Kama ungekuwa na umakini kidogo tu; ktk press conference CC ya CHADEMA iliagiza mchakato wa kumvua Zitto unaibu kiongozi wa KUB ufanyike.

Ila kama ulivyosema, Zitto ni MNAFIKI na MSALITI, hapo nakuunga mkono 100%


WANA MUDA hata wakusoma basi?
 
Baada ya Mbowe kusema mbele ya watanzania kuwa Zitto Kabwe ni mnafiki, itakuwa ni unafiki zaidi kwa Mbowe kuendelea kufanya kazi na Zitto kama Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Hii ni sawa na siku Kikwete akisema hadharani kuwa Pinda ni mnafiki na kumvua vyeo vyote vya CCM lakini akamuacha kuwa Waziri Mkuu. Jambo hilo haliwezekani!

Kwa mantiki hii, iwapo hotuba ya Zitto ya leo haitatangaza kujiuzuru unaibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mbowe atalazimika kuvunja Baraza kivuli la Mawaziri na kuliunda upya. Asipofanya hivyo atakuwa ni mnafiki mara dufu.

Wakati huohuo, kwa kutumia busara, ingawa sheria hailazimishi, Mbowe au Dr. Slaa anawajibika kumpa Spika taarifa rasmi ya maandishi kuhusu Zitto kuvuliwa uongozi Chadema, Spika wa Bunge baada ya kupata taarifa hiyo anawajibika kumuuliza KUB kwa maandishi iwapo anaridhika na Zitto kuendelea na uenyekiti wa PAC.

Busara inataka hivyo kwa sababu Zitto amepewa uenyekiti wa PAC kutoka upinzani, anawakilisha upinzani. Kwa vile upinzani unamuona Zitto msaliti, Spika akikaa kimya tu ataingizwa kwenye lawama ya kuingiza wasaliti kwenye nafasi za wapinzani. Lakini ili hata yote yatokee ni LAZIMA Mbowe au Dr. Slaa amuandikie barua rasmi Spika kumjulisha msimamo wa Chadema juu ya Zitto.

Iwapo KUB atasema haridhishwi na Zitto kuongoza PAC, basi Spika atawajibika "kumshauri" ajiuzuru nafasi hiyo.

Kama tuko seriuos na utawala bora, hivi ndivyo tunavyotakiwa kufanya...

HATUJAWAHI KUWA SERIOUS NA GOOD GOVERNANCE, AND THAT IS BECAUSE OF SILLY SIASA OF OURS.... na zitto bado ni mbunge na mwanachama wa chadema

you degrade yourself kila siku, i am just not sure how low you can go to realise that the government paid money ili ufanye kazi na sio kubwabwaja
 
Wewe ni mlaghaika. Kumvua Zitto unaibu KUB sio mchakato, ni swala la Mbowe tu kunyanyuka na kusema.

Mchakato wa nini sasa? Wabongo mnapenda sana michakato michakato. Hata kufungua mlango wa gari utasema "nimeanza mchakato wa kufungua huu mlango wa gari".

ZeMarcopolo,
Ndio maana nilitangulia kusema hujui. Kwa ufupi sana CHADEMA kumvua Zitto vyeo na hata uanachama ni mchakato na utaratibu tofauti na ule wa kumvua cheo cha unaibu KUB. Hivyo kwa sasa Zitto sio tena Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA wala mjumbe wa CC nk ila kama atavuliwa uanachama basi atapoteza sifa za kuwa Mbunge. Ni lazima uwe Mbunge ndipo uwe mjumbe ktk kamati za Bunge mfano PAC ambayo alipewa na washirika wake kuwa m/kiti. Lazima uihusihe ofisi ya Spika mabadiliko kama hayo nk

Sio kila kitu uchangie na/au kupotosha halafu tunyamaze tu.

CHADEMA wako tayari kupunguziwa ruzuku na/au hata nafasi za viti maalum kwa kumtosa Zitto na/au msaliti yoyote kuliko kuganga njaa na kukumbatia uchafu/unafiki/usaliti.


Halafu mbona hamumtetei Mwigamba na Mkumbo kama mnavyomtetea Zitto? Ni kwa vile ndiye aliyekuwa sterling wa mapinduzi ya kuingamiza CHADEMA sio?
 
HATUJAWAHI KUWA SERIOUS NA GOOD GOVERNANCE, AND THAT IS BECAUSE OF SILLY SIASA OF OURS.... na zitto bado ni mbunge na mwanachama wa chadema

you degrade yourself kila siku, i am just not sure how low you can go to realise that the government paid money ili ufanye kazi na sio kubwabwaja

Kama hamjawahi kuwa serious, ni lini mnataka kuanza kuwa serious?
 
Baada ya Mbowe kusema mbele ya watanzania kuwa Zitto Kabwe ni mnafiki, itakuwa ni unafiki zaidi kwa Mbowe kuendelea kufanya kazi na Zitto kama Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Hii ni sawa na siku Kikwete akisema hadharani kuwa Pinda ni mnafiki na kumvua vyeo vyote vya CCM lakini akamuacha kuwa Waziri Mkuu. Jambo hilo haliwezekani!

Kwa mantiki hii, iwapo hotuba ya Zitto ya leo haitatangaza kujiuzuru unaibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mbowe atalazimika kuvunja Baraza kivuli la Mawaziri na kuliunda upya. Asipofanya hivyo atakuwa ni mnafiki mara dufu.

Wakati huohuo, kwa kutumia busara, ingawa sheria hailazimishi, Mbowe au Dr. Slaa anawajibika kumpa Spika taarifa rasmi ya maandishi kuhusu Zitto kuvuliwa uongozi Chadema, Spika wa Bunge baada ya kupata taarifa hiyo anawajibika kumuuliza KUB kwa maandishi iwapo anaridhika na Zitto kuendelea na uenyekiti wa PAC.

Busara inataka hivyo kwa sababu Zitto amepewa uenyekiti wa PAC kutoka upinzani, anawakilisha upinzani. Kwa vile upinzani unamuona Zitto msaliti, Spika akikaa kimya tu ataingizwa kwenye lawama ya kuingiza wasaliti kwenye nafasi za wapinzani. Lakini ili hata yote yatokee ni LAZIMA Mbowe au Dr. Slaa amuandikie barua rasmi Spika kumjulisha msimamo wa Chadema juu ya Zitto.

Iwapo KUB atasema haridhishwi na Zitto kuongoza PAC, basi Spika atawajibika "kumshauri" ajiuzuru nafasi hiyo.

Kama tuko seriuos na utawala bora, hivi ndivyo tunavyotakiwa kufanya...

Zitto kuongoza PAC sio kuongoza CDM. Endapo Zitto ataendelea kubaki CDM ataendelea kuwa mbunge na sijui ni kwa vipi itamuondolea sifa ya kuongoza PAC
 
Wewe ni mlaghaika. Kumvua Zitto unaibu KUB sio mchakato, ni swala la Mbowe tu kunyanyuka na kusema.

Mchakato wa nini sasa? Wabongo mnapenda sana michakato michakato. Hata kufungua mlango wa gari utasema "nimeanza mchakato wa kufungua huu mlango wa gari".
Wewe bado hujaanza Mchakato wa Kukeketa vijana wetu huko morogoro wewe Ngariba?
 
Halafu mbona hamumtetei Mwigamba na Mkumbo kama mnavyomtetea Zitto? Ni kwa vile ndiye aliyekuwa sterling wa mapinduzi ya kuingamiza CHADEMA sio?

Wewe ni SIFURI kabisa.

Kwenye hii thread napendekeza Zitto avuliwe madaraka ya Unaibu KUB na Uenyekiti wa PAC, lakini kwa vile wewe ni SIFURI unasema namtetea zitto. Hii ni kwa sababu umeshajitengenezea jibu na sasa ndio unalitafutia swali.

Siasa za kilaghai za chadema zimekuathiri. Inabidi tuanzishe MCHAKATO wa kukukomboa...
 
Kwenye press walishasema aondolewe kuwa naibu KUB. Hivyo hili kamati kuu imeweka wazi.
 
Wewe ni mlaghaika. Kumvua Zitto unaibu KUB sio mchakato, ni swala la Mbowe tu kunyanyuka na kusema.

Mchakato wa nini sasa? Wabongo mnapenda sana michakato michakato. Hata kufungua mlango wa gari utasema "nimeanza mchakato wa kufungua huu mlango wa gari".
kuna mtoto wa rafiki yangu huku anaitwa Mchakato Sanga
 
Back
Top Bottom