Je, Nyerere alikuwa mshamba kutokutaka Mali za umma iitwe Jina lake?

Bado Miradi ilioanzishwa wakati tumepata Uhuru na kuendelea ni mingi sana nchi hii ukilinganisha na sasa hivi. Ila chakushangaza wakati huo wa utawala wa Baba wa Taifa hakuna hata project moja ilio itwa jina Nyerere.

Ni Juzi kati baada ya yeye kufariki ndio kidogo vitu vikaanza kuitwa majina yake.

Ila kuanzia awamu hasa ya Tano na hii ya sasa ni kila project wanataka iitwe majina yao, kila kitakacho anzishwa wanataka jina lao ndio litokelezee pale. Sasa je Nyerere alikuwa mashamba wa kiwango cha juu kabisa kuto kubali kutukuzwa? Kuto kubali vitu au mali za umma zipewe jina lake?

Kwa nini sasa hawa viongozi wa sasa wanataka kutukuzwa kupindikia na kuna chawa wanawachukulia kama ndio Mungu, viongozi wana sujudiwa kwa sasa.

Wanataka kujienzi wakiwa madarakani? waonekane kana kwamba walio tangulia hawakufanya chochote kile au walikuwa washamba sana?
Dębe tupu haliishi kufanya nini vile?
 
Zamani tulitumia majina ya wazee waliolikomboa taifa hili kwa heshma yao!! Ilikaa vyema
Sasa saivi mambo yameharibika tumeharibu ile heshma kwa viongozi. Kwasasa hata fyongoz wasio na umuhimu nchini majina Yao yanatumika...mf. soko kuuubwa Dom linaitwa jobu eti mropokaji alolazimishwa kujiuzulu kutokana na miropoko,kuelewa uspwika naviubabe vyakishamba!!!
 
Nyerere aliuishi ujamaa halisi ndio maana hata alipoona nchi inapoteza uelekeo kwa sera za ujamaa hakutaka kuonekana kinyonga kuuvaa ubepari akatumia busara ya "kung'atuka"

Ujamaa una element kama hizo za kutopenda vikubwa.
 
Hii ni mada muhimu sana

Nyerere aliitwa kufungua uwanja wa michezo Sumbawanga uliopewa jina la Nyerere.
Siku ilipofika Nyerere alikataa na kusema uitwe Nelson Mandela, hadi leo

Rais Mwinyi akafuta nyayo, hakupenda vitu viitwe majina yake
Rais Mkapa ndiyo kabisa hata noti (fedha) alikataa picha na Uwanja wa Mkapa ni kama alilazimishwa
Rais Kikwete hakutaka pia kama Watangulizi wake

Rais Magufuli akaharibu taratibu zote na kuanza kutoa majina ya ' Landmark' akijisikia bila hata kuuliza
Aliita maeneo ya alama za nchi kwa rafiki zake na yeye akipenda sana kutukuzwa

Rais Samia ameingia katika mtego huo. Nimeshangaa sana Uwanja wa michezo wa Arushwa kuitwa jina lake.

Uwanja wa Arusha upo kimkakati kutangaza utalii. I
Ni fursa adhimu ya kutangaza vivutio vya nchi kama ,Mlima Kilimanjaro, Serengeti, Ngorongoro na Arusha kama HQ ya E.A.Comunity. Rais SSH alipaswa kuliona hili, ametumiwa na ''chawa '' si kwa masilahi mapana ya nchi.

Kenya wakiamua kutumia Mlima Kilimanjaro na vivutio vingine tunalalamika, ukweli ni kwamba hatujui inabaidi tuwaache tu waendelee. Uchawa umekuwa sehemu ya maisha na kusahau yaliyo muhimu kwa nchi.

Ujumbe kwa Mh Rais SSH, tenda yako kwa weledi, hekima na busara jina lako litaandikwa kwa wino wa dhahabu hata miaka 10,20 au 100 ijayo. Haya yanayofanywa sasa hivi ni 'Chawa' na yanakuharibia.

Miaka 25 tangu Nyerere afariki lakini bado ''anawakusanya'' viongozi Adis Ababa kumuenzi.
Anatajwa na kutamkwa na dunia. Hakuwa na chawa!

JokaKuu Pascal Mayalla Mag3
Kuna Samia Complex pia inayojengwa Dodoma. Ubinafsi ni tatizo kubwa sana nchini.
 
Back
Top Bottom