Jaji Warioba akosoa Serikali kutoa elimu ya Katiba Mpya kwa miaka mitatu

Miaka mitatu elimu ya kuandika katiba mpya!!!!!

  • Hi

    Votes: 0 0.0%
  • 1

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    0
Tulianza mchakato wa kuandika katiba mpya mwaka ule wa 2011 tukaenda mpaka 2014, fedha kibao zikatumika kugharamia wajumbe wa katiba mpya, , leo tupewe tena miaka mitatu kupata elimu kisa tuu kuna kizazi hapa katikati kimekuja mnataka kusema kuwa kila kizazi kipya kikizalisha Tanzania tutakuwa tunaandika katiba.. washauri wa mama yetu tunaomba ashauriwe tena na tena miaka mitatu elimu raslimali fedha nyingi tulitumia kuandika iliyokwama, je, kama taifa tutakuwa tuuu tunazungumzia kuhusu katiba miaka yote na kutengenezeana fedha tuu, wajumbe wale kumbukeni walivyokuwa wengi kodi zetu zikatumika zipoteee hivi hivi!!! Aaaaaaaaaahhh nchi hii!! hapana miaka 3 elimu tunachukua digrii!!!!?
 
Tulianza mchakato wa kuandika katiba mpya mwaka ule wa 2011 tukaenda mpaka 2014, fedha kibao zikatumika kugharamia wajumbe wa katiba mpya, , leo tupewe tena miaka mitatu kupata elimu kisa tuu kuna kizazi hapa katikati kimekuja mnataka kusema kuwa kila kizazi kipya kikizalisha Tanzania tutakuwa tunaandika katiba.. washauri wa mama yetu tunaomba ashauriwe tena na tena miaka mitatu elimu raslimali fedha nyingi tulitumia kuandika iliyokwama, je, kama taifa tutakuwa tuuu tunazungumzia kuhusu katiba miaka yote na kutengenezeana fedha tuu, wajumbe wale kumbukeni walivyokuwa wengi kodi zetu zikatumika zipoteee hivi hivi!!! Aaaaaaaaaahhh nchi hii!! hapana miaka 3 elimu tunachukua digrii!!!!?
Labda miaka mitatu ya kula hela tena kama wakati ule.
 
Rasimu yaWarioba imepitwa na wakati

kuna Vijana wengi hivi Leo hawakuweza kushiriki rasimu ya Warioba ya miaka 10 iliyopita

ni vyema Mchakato ukaanza upya kwa kuelimisha Umma walau kwa miezi 36 kabla ya kuanza rasmi mchakato

Jambo zito kama hili hatuna haja ya kulikimbiza na kuharakisha
Kumbe wewe ndio mshauri mkuu wa Mama.
 
Waziri Mkuu, mstaafu Jaji Joseph Warioba ameeleza wasiwasi wake kuhusu hatua ya Serikali ya kutaka kuanza kutoa elimu ya Katiba Mpya kwa miaka mitatu, akisema ni muda mrefu kwa mchakato huo.

“Tumefikia mahali kama kuna utashi wa kisiasa, tunaweza kuamua juu ya haya mabadiliko, inanipa wasiwasi, ni kama tunataka kuanza upya mchakato huu. Unaona mijadala hii ya Katiba inavyoingilia shughuli zetu za maendeleo, nadhani imefika wakati tufanye uamuzi,” amesema Jaji Warioba.

Jaji Warioba ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, ameeleza hayo Ijumaa Agosti 31, 2023 katika mahojiano wa Azam TV yaliyofanyika nyumbani kwake wilayani Kinondoni, mkoani Dar es Salaam.

Juzi aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro, alisema watatoa elimu ya mabadiliko ya katiba kwa miaka mitatu, akisema kwamba utafiti walioufanya umeonekana kuwa zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania hawaifahamu Katiba na hata wengine hawajawahi kuiona.

Kauli hiyo, Dk Ndumbaro iliwaibua wadau mbalimbali wakiwemo Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) na Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), waliokosoa hatua hiyo, wakisema inalenga kuchelewesha mchakatao huo.

Katika maelezo yake, Jaji Warioba amesema wakati akiwa mwenyekiti wa tume hiyo, wananchi walishiriki na walitoa elimu ya kutosha kuhusu Katiba Mpya, akisema walisambaza nakala za Katiba za Tanzania na Zanzibar.

Mbali na hilo, walifanya machapisho kueleza yaliyo katika Katiba na kusambamba katika maeneo mbalimbali ikiwemo vijijini, akisema kwa namna yanayoendelea hivi sasa huwezi kusema wananchi hawana elimu kuhusu mchakato huo.

“Kwa jinsi walivyoipanga sioni kama wanaweza kutoa mwanga zaidi kuliko walionao hivi sasa, Kamati ya Mukandala (Profesa Rwekiza), imechukua maoni ya kutosha na wananchi wanajua. Mimi natafsiri Serikali ingesema hatuwezi kupata Katiba Mpya sasa hivi, waseme mapema kuliko hivi,” amesema na kuongeza;
expand...
Wandugu ambia huyo mtawala mwanamke, amuogope "MUNGU" kwani si-niyeye kwa kinywa chake? Alitamka ya kwamba atafanya mabadiliko makubwa ht yakimgharimu ki-siasa? Sasa anapambana na nani tena? Ashasahau yeye ndo alitamka?!!!! KITI alichokalia kina DAMU, uovu ni mwingi mno kwa hicho KITI... vilio juu ya hicho KITI ni-vikubwa mno vimefika hadi Mbinguni, ndo maana kila anayekalia hicho KITI mwanzoni huanza vizuri sn, lkn baada ya muda roho za uovu ndani ya hicho KITI huanza tena kutenda kazi.... swali rahisi, ni-nani kakashifu/kachambua dini ya mtu mwingine? ukweli hayupo, TEC wametoa waraka wao wamemaliza wako kimya, hizo ni sababu tu za kuhalalisha jambo fulani, sasa nasema MUNGU HADHIHAKIWI anaujua ukweli wote, nasema, bado kuna mambo MUNGU anataka kuyatenda juu ya hii Nchi, mwenye masikio na asikie..............
 
Shida wanasiasa wanaharaka na katiba mpya kuliko hata sisi wananchi kuna watu Wana maslahi binafsi na katiba mpya
 
Shida wanasiasa wanaharaka na katiba mpya kuliko hata sisi wananchi kuna watu Wana maslahi binafsi na katiba mpya
Jaribu kufikiria zaidi katiba kuliko..... Kumfikiria mwana siasa.
Mwana siasa atapita ila Taifa ni endelevu mkuu
 
Back
Top Bottom