BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,482
- 8,336
Mahakama Kuu Kanda ya Iringa imemuhukumu kunyongwa hadi kufa Mwanaume aitwaye Mohamed Njali kwa kosa la kumbaka na kumuua kwa kumkaba Atika Chesco Kivanule (24) September 25, 2022 saa saba usiku wakati Mumewe akiwa kwenye banda la video kutazama pambano la ngumi la Mandonga vs Salim Abeid lililofanyika Mkoani Mtwara.
Katika kesi hiyo ambayo ilisimamiwa na Mawakili wa Serikali WinFrida Mpiwa na Muzna Mfinanga na kutolewa hukumu na Jaji wa Mahakama Angaza Mwipopo, Mahakama imesema siku ya tukio hilo Mshtakiwa alivunja mlango na kuiba simu pamoja na suti na baadae kumbaka Atika na kumkaba shingoni.
Adeline Kileo ambaye ni Mume wa Marehemu ameishukuru Mahakama kwa adhabu iliyotolewa dhidi ya Kijana huyo Mohamed Njali.
Katika kesi hiyo ambayo ilisimamiwa na Mawakili wa Serikali WinFrida Mpiwa na Muzna Mfinanga na kutolewa hukumu na Jaji wa Mahakama Angaza Mwipopo, Mahakama imesema siku ya tukio hilo Mshtakiwa alivunja mlango na kuiba simu pamoja na suti na baadae kumbaka Atika na kumkaba shingoni.
Adeline Kileo ambaye ni Mume wa Marehemu ameishukuru Mahakama kwa adhabu iliyotolewa dhidi ya Kijana huyo Mohamed Njali.